Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Kwa mara nyingine tena nimekutana na lile sakata. Safari hii ni la binti mrembo kabisa wa Kiafrika. Ana kila kitu ambacho kingemvutia mwanaume yoyote rijali. Baada ya kuona yuko karibu sana na binti wa Kizungu aliyekuwa akimkumbatia mara kwa mara kwa ukaribu wa hali ya juu wakati wa kucheza mziki nikahisi labda na yeye ni wale wale. Lakini nikajibishia moyoni kwa matumaini kuwa haiwezekani hasa ukizingatia kuwa hakuwa na dalili zozote - alikuwa amevaa kisichana kabisa, amechana nywele zake vizuri mno kwa staili ya yule mwanamama Angela Davis wa enzi zile za Afro na alionyesha kuvutiwa na mchombezo wangu. Ili kujihahikikishia kuwa siingii mkenge tena nikamchomekea swali hili: Inaonekana wewe na huyu dada ni marafiki sana? Akanijibu kwa kifupi: Akchwale huyo ni rafiki yangu wa kike! Salale, nikajisemea moyoni kwa uchungu, kweli wanaume tumekwisha duniani!