Wanaume sio ATM!!!

Dr Lizzy

Platinum Member
May 25, 2009
30,770
59,118
Hii mtindo wa kuwaita wanaume ATM unawaboa sana kusema ukweli...hata mimi kama mdada siufagilii.Achili mbali huwaita hata kuwatumia kama ATM nayo inatufanya wadada tunadharauliwa wakati mwingine.

Kuna marafiki zangu wawili niliwatambulisha wiki chache zilizopita.Mkaka wa watu akawa amedata haswa....kila saa kumuulizia binti.Kiukweli kaka alikua anataka mahusiano yanayoeleweka na sio kuchezeana.Wakakutana mara mbili tatu mkaka akaendelea kudata.

Siku ya siku kaka akamwalika mdada chakula cha jioni ali wapate muda wa kuongea kidogo...mdada akaja na shoga yake.Yule kaka akaboreka ila akapotezea tu.Hata akijaribu kuongea na mambo ya maana mdada akili yote kwenye mambo ya starehe tu...nayo akapotezea.Alipokuja kuharibu ni kuanza kuulizia vocha...tena kwa kudemand....yani yule kaka alichoka.Kwasababu kumpigia hampigii...akitaka kuongea nae anaweka utoto mwingi ila wakati akitaka lift na vocha ndo haishi kubeep apigiwe.
Yule kaka alikuja kuniambia yule rafiki yako kwakweli nimemshindwa.Naweza kuelewa kwamba bado hajaweka maisha yake kwenye mstari ila atleast angekua anaonyesha nia badala ya kushinda akiomba pesa ningempa muda.

Newayz nnachojaribu kusema hapa ni kwamba wadada fanyeni kazi...na hata kama huna sio mtu hata bado hamjawa karibu sana tayari umeshaanza kua omba omba.Unajipotezea mwenyewe bahati....mwanaume mwenye nia anataka mwanamke mwenye nia na anae eleweka!!Acheni kuwatumia wakaka wa watu...mpende kama umempenda na sio kumendea vijisenti vyake alivyotolea jasho!!!

Nawakilisha!!!
 
Hivi kuna wadada wa hivi siku hizi??? Ai mie siwezi uinitoa out ujue nina pesa ya kula na kunywa (valuer) na tax ya kunirudisha home
 
Huyo kaka asome alama za nyakati asepe zake, aachane nae, huyo bado hajakomaa kiakili, hafikirii mbele wala hajui anachokitaka.

Yani kama ndo kaka angu anakuita halafu unakuja na shoga ako akija kuniadithia tu, imekula kwako!!!!!
 
Hapo umeongea ukweli.. mapenzi sio kukomoana ni kusaidiana sasa unapodemand kitu unaweza ukawa unamuaribia bajeti mwenzako...

Na kweli kama dada anakuwa mstaarabu hata huyo kaka angekuwa anasaidia popote inapobidi, wakati umefika tuone kwamba maisha ni kusaidiana kwa mambo yote na mtu anapotoa kitu bila kuombwa its has got more meaning kuliko kumlazimisha, hapo ni kama unamfanya ananunua hilo penzi...
 
Huyo kaka asome alama za nyakati asepe zake, aachane nae, huyo bado hajakomaa kiakili, hafikirii mbele wala hajui anachokitaka.

Yani kama ndo kaka angu anakuita halafu unakuja na shoga ako akija kuniadithia tu, imekula kwako!!!!!
Lakini hapa sometimes kwa dada zetu ni Security na labda anataka shoga yake na yeye atoe recommendation kuhusu huyo kaka au?
 
Hawa ni wale wadada tunaowaita GOLD DIGGERS wakati mwingine napenda kuwaita SAYONA
 
Kuna wanawake ambao wameshakunywa maji ya bendera, yaani ameshasikia sana wanaume wote ni waongo, sasa wanaamua ku-behave kiuchunaji zaidi, mapenzi wanakuwa wameshayauza
 
Hapo umeongea ukweli.. mapenzi sio kukomoana ni kusaidiana sasa unapodemand kitu unaweza ukawa unamuaribia bajeti mwenzako...

Na kweli kama dada anakuwa mstaarabu hata huyo kaka angekuwa anasaidia popote inapobidi, wakati umefika tuone kwamba maisha ni kusaidiana kwa mambo yote na mtu anapotoa kitu bila kuombwa its has got more meaning kuliko kumlazimisha, hapo ni kama unamfanya ananunua hilo penzi...

Voice naomba unitumie vocha kuna mtu nataka niongee naye mara moja. Sasa hivi please!!
 
Voice naomba unitumie vocha kuna mtu nataka niongee naye mara moja. Sasa hivi please!!
Nakutumia sababu mimi kama rafiki na unahitaji na mimi ninayo nitatuma lakini na mimi kesho nikiomba msaada wowote usininyime, sababu maisha ni kusaidiana kwenye shida, A Friend in Need is A Friend Indeed.... Lakini hapa anachosema Lizzy huyu dada kamfanya huyo kaka ndio kama ka mradi ka yeye kumalizia shida zake (sometimes hata kama hana shida..., basi tu kutumbua jasho la mwenzake)
 
Lakini hapa sometimes kwa dada zetu ni Security na labda anataka shoga yake na yeye atoe recommendation kuhusu huyo kaka au?

Hakuna hata cha security mwenzangu Voice, kama hivo amwambie basi nitakuja na rafiki yangu unasema je? Yani mtu mwenye nia ya kuanzisha urafiki wenye malengo mazuri hawezi kuja kwa mkao wa kukuchuna ndugu yangu. Waulize kina kaka wakwambie na wakifika hapo wanakunywa na kula vya gharama mpaka unajuta. Na maisha ya bongo haya mwenyewe una ka elfu 30 hapo mfukoni. Unaletewa bill elfu 60 watu wa tatu tu!! Duu bado unatakiwa uwarudishe walikotoka!!!
 
Yaani my first date with u unaniijia na rafiki zako kisa security no way.
Depend mnakutana wapi..., from what I think kama dada hajakujua vizuri, atakuwa ameshaongea na marafki zake kuhusu wewe kwahiyo anataka kuwaonyesha alafu wengine ile fear ya kwamba wewe utataka kupeleka mambo kwa kasi ile inakuwa ni kama (TUTA KWENYE BARABARA) ili uslow down na usitake advantage... thats what I think lakini I might be wrong...
 
Nakutumia sababu mimi kama rafiki na unahitaji na mimi ninayo nitatuma lakini na mimi kesho nikiomba msaada wowote usininyime, sababu maisha ni kusaidiana kwenye shida, A Friend in Need is A Friend Indeed.... Lakini hapa anachosema Lizzy huyu dada kamfanya huyo kaka ndio kama ka mradi ka yeye kumalizia shida zake (sometimes hata kama hana shida..., basi tu kutumbua jasho la mwenzake)

Msaidie then sahau. Usitamke KESHO NA MIMI UNISAIDIE, muache aamue kwa roho yake
 
Siku ya siku kaka akamwalika mdada chakula cha jioni ali wapate muda wa kuongea kidogo...mdada akaja na shoga yake.Yule kaka akaboreka ila akapotezea tu.

Hiyo inaitwa style ya Bata. Yaani hakuna kitu mbaya ka kumdate m2 halafu anakuja na watoto wa bata. Nilimwaga m2 akiwa amaona hv hv. Wakati huo napiga kitabu. Nimejibana kusave kiaina mara bibiye kaja na mwenzie. dah bajeti ishaharibika. Afu omba Mungu usijekutana na wa red bull sijui Heineken mara amarula ndo utakoma.
Thanks Lizzy umeliona hili!
 
Nakutumia sababu mimi kama rafiki na unahitaji na mimi ninayo nitatuma lakini na mimi kesho nikiomba msaada wowote usininyime, sababu maisha ni kusaidiana kwenye shida, A Friend in Need is A Friend Indeed.... Lakini hapa anachosema Lizzy huyu dada kamfanya huyo kaka ndio kama ka mradi ka yeye kumalizia shida zake (sometimes hata kama hana shida..., basi tu kutumbua jasho la mwenzake)

Nimemwelewa sana lizzy, yani hiyo mimi ndo naomba vocha kwako Voice, au hutaki kuwa ATM wangu jamani.
Nitumie ya 10,000 basi!!
 
Hakuna hata cha security mwenzangu Voice, kama hivo amwambie basi nitakuja na rafiki yangu unasema je? Yani mtu mwenye nia ya kuanzisha urafiki wenye malengo mazuri hawezi kuja kwa mkao wa kukuchuna ndugu yangu. Waulize kina kaka wakwambie na wakifika hapo wanakunywa na kula vya gharama mpaka unajuta. Na maisha ya bongo haya mwenyewe una ka elfu 30 hapo mfukoni. Unaletewa bill elfu 60 watu wa tatu tu!! Duu bado unatakiwa uwarudishe walikotoka!!!
Hapana LD sikatai kwamba wachunaji wapo thats why nikasema inategemea mnakutana wapi..., lakini mara nyingi nadhani kwenye hizi dates nyingi mwanzo dada anakuwa muoga kwenda sehemu peke yake anataka company... kwahiyo suala la company on the first day peke yake sio baya sana kama hao dada watakuwa wastaarabu na kunywa maji na sio kubugia pombe kama vile TBL ni ya baba yangu.
 
kweli mwanangu mwenyewe lizzy
hii mi minungaembe ya kisiku hizi sio kabisa yaani,
iko kimitego zaidi ndo maana inapukutishwa na mdudu
 
Nimemwelewa sana lizzy, yani hiyo mimi ndo naomba vocha kwako Voice, au hutaki kuwa ATM wangu jamani.
Nitumie ya 10,000 basi!!

Kumbe kwa lengo la kumgeuza ATM??? Mi hata dada angu akiniomba vocha frequently naanza kumpa majibu ya kisanii
 
Msaidie then sahau. Usitamke KESHO NA MIMI UNISAIDIE, muache aamue kwa roho yake
Mkuu shida ikija haipigi hodi.., yaani hapa ninachosema inabidi ile imani ya kwamba Mwanaume inabidi atoe inabidi iishe, maisha ni kusaidiana kwahiyo siku nikiwa broke hakuna ubaya mwenza wangu akinitreat..., hayo ndio maisha. Yaani yeye akipata shida am the first kuambiwa na mimi nikipata hivyo hivyo na isiwe one sided
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom