ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,650
Kuna mdada, miezi mitatu iliyopita alimfumania mumewe na mwanamke ambaye ni rafiki yake ingawa sio kiviiiiiiiiiiile! Kama kawaida ya wadada akalia weeeeeeee mwishowe akaamua kumsamehe mpenzi wake baada ya jamaa kuahidi kutorudia tena na kwamba eti alikuwa ni shetani tu-aisee ktk hili tumshukuru Mungu wanawake kuwa viumbe wenye huruma, kwa kweli wangekuwa kama sisi midume, walahi dunia ingekuwa imekwisha. Basi maisha yakaendelea kwa furaha kana kwamba hakikutokea kitu.
Wiki iliyopita jamaa wakati anapata moja moto moja baridi maeneo ya Sinza Mori, akaona gari inapita mbele kwa siti ya abiria amekaa mkewe. Bila kujali dereva wa gari ana uhusiano gani na mkewe, jamaa akalifuatilia gari hadi liliposimama mbele ya nyumba ya wageni. Geti lilipofunguliwa gari ikaingia ndani ya geti. Wakati jamaa analifukuzia gari, watu wakashangaa nao wakaamua kufuatilia-unajua tena umbea wa mjini. Jamaa alipoingia ndani kupitia geti dogo, akamkuta mkewe kakaa makochini pale reception. Bila kuuliza mwanaume akaanza kumkaripia mkewe eti ni malaya na amekuwa akimsaliti tangu zamani ndiyo maana na yeye aliamua kutoka na mwanamke aliyemfumania mwanzoni. Iweje mke wa mtu aende guest na mwanaume mwingine kama sio umalaya ni nini? Kila mtu alibaki kumshangaa yule mwanaume, kwani si alimkuta reception amekaa iweje adai amemfumania na mwanaume?
Swali kwa wanaume? Hivi kwa nini huwa tunajihesabia haki sana ktk mapenzi kiasi cha kutembea na wanawake lukuki halafu tunageuka mbogo pindi wanawake wanapoamua kuiga yale tunayowatendea wao? Je hii ni matokeo ya mfumo dume au ndo kusema tu kwamba ni kujona kwamba sisi ni bora kuliko wengine ambao hatujali hisia zao na maumivu ya kusalitiwa?
Jamani wanaume, tujiulize na kujirekebisha, suala la mkuki kwa nguruwe ila kwa binadamu....... ni lazima likomeshwe.
Nawasilisha!
Wiki iliyopita jamaa wakati anapata moja moto moja baridi maeneo ya Sinza Mori, akaona gari inapita mbele kwa siti ya abiria amekaa mkewe. Bila kujali dereva wa gari ana uhusiano gani na mkewe, jamaa akalifuatilia gari hadi liliposimama mbele ya nyumba ya wageni. Geti lilipofunguliwa gari ikaingia ndani ya geti. Wakati jamaa analifukuzia gari, watu wakashangaa nao wakaamua kufuatilia-unajua tena umbea wa mjini. Jamaa alipoingia ndani kupitia geti dogo, akamkuta mkewe kakaa makochini pale reception. Bila kuuliza mwanaume akaanza kumkaripia mkewe eti ni malaya na amekuwa akimsaliti tangu zamani ndiyo maana na yeye aliamua kutoka na mwanamke aliyemfumania mwanzoni. Iweje mke wa mtu aende guest na mwanaume mwingine kama sio umalaya ni nini? Kila mtu alibaki kumshangaa yule mwanaume, kwani si alimkuta reception amekaa iweje adai amemfumania na mwanaume?
Swali kwa wanaume? Hivi kwa nini huwa tunajihesabia haki sana ktk mapenzi kiasi cha kutembea na wanawake lukuki halafu tunageuka mbogo pindi wanawake wanapoamua kuiga yale tunayowatendea wao? Je hii ni matokeo ya mfumo dume au ndo kusema tu kwamba ni kujona kwamba sisi ni bora kuliko wengine ambao hatujali hisia zao na maumivu ya kusalitiwa?
Jamani wanaume, tujiulize na kujirekebisha, suala la mkuki kwa nguruwe ila kwa binadamu....... ni lazima likomeshwe.
Nawasilisha!