Wanaume hebu tuongee kidogo; TUJIREKEBISHE

sema tuwapende siku zote sio za mimba tu lkn wanawake nao hawapendeki. ikimpenda sana anaona kama uko chini yake na anaanza visa.
 
sema tuwapende siku zote sio za mimba tu lkn wanawake nao hawapendeki. ikimpenda sana anaona kama uko chini yake na anaanza visa.


Mi nadhani kama mnaelewana wala hakutakuwa na maisha haya ya kuviziana viziana ati nikimpenda saa ataniona nipo chini yake.

Nadhani kila kitu kina limits zake. Lazima mtakuwa mmejiwekea mikakati na mipango ya maisha ambapo mtu hawezi akachange

immediately anapooneshwa upendo
 
Matarajio baada ya ndoa ni watoto,so kwanini usimpende?,usimthamini? Vinginevyo there is no need to be with her
 
Ninafanya kazi na wanaume wengi sana wengi wao katika maongezi mke akiwa mjamzito ni kama kero kwao. Mimba inachosha jamani sijui ni wanaume wangapi wanawasaidia wake zao hata kupaka mafuta miguu wanapokuwa wajawazito. unakuta mama miguu imevimba hata mtu wa kumfanyia angalau kamassage kadogo hamna, linjemba lipo baa linaangalia man u, na usiombe uwe mjazito halafu kuna watoto wengine wadogo hapo ndio utaiona dunia ni chungu kama huna msaada wa karibu na wamaana. Kama ni wakati ambao mwanamke anahitaji msaada ni wakati akiwa mjamzito.

Nimeshuhudia wanaume wanalala nje wakati wake zao ni wajawazito tena ujauzito wa kujifungua dakika yoyote na anarudio asubuhi mama ukiumwa usiumwe ni juu yako ukipata pressue kwa kuwaza ukafa na kiumbe chako tumboni ni juu yako.
 
Habari za nyakati hizi wanajamvi! Nimeona niseme machache kwa wanaume wezangu. Pengine yalishasemwa, basi ni

kukumbushana tuu!

1. Mpende Mkeo wakati wa ujauzito! Ulimpenda. Ukamwoa. Ukamwita majina mengi ikiwemo wewe ndio mama wa watoto wangu.

Umefanya vitu na sasa ni mjazito, kwa nini kukimbia kimbia nje? Tumehusika kusababisha ujauzito basi tuoneshe upendo mkubwa

na matunzo ya hali ya juu katika msimu huo.

2. Little surprises work out a lot! Does it make you less a gentleman to prepare a breakfast for her?

3. Does it kill you or make you less a man to say ' Im sorry my wife, please forgive me'?

Basi, pale panapotuhusu, tupachukue, tuparekebishe, tufurahie ndoa zetu. Life is short why kununiana daily ndani wakati nje

unacheka na visekretari pamoja na vihudumu?

Asubuhi njema.

Morning to u too

Imekaa vizuri hiyo kaka...tofauti ya wanaume na wavulana ndo kama huyo alojibu (jirekebishe mwenyewe) hao wapo tu na si kazi hajaoa wala hajui maana ya familia....na kama kaoa ndo wale wanaoona wake zao wana furaha ilhali yeye anamkera daily na haimuingii akilini kwamba furaha hainunuliwi.......

Tuwajali...tuwapende na tuwathamini saaanaaa WAKE zetu..........as you propose to her......indirectly you tell the community that responsibility to mainatain it rests with you in the first place coz yu know better why it is her for marriage
 
Tatizo la wanawake ukiwasaidia kwa upendo wanajisahau na wanafanya kuwa wajibu wako.
 
Mmmh hiyo ngonjera haipo kwenye dictionary ya wanaume wa kiBonGo. Hawajui ni kazi kubeba mimba miezi 9 ontop of that there is alot of biological changes katika mwili wa mwanamke including hormone which may affection her emotionally.

hiyo ipo lakini ni kwa baadhi wanaojua majukumu na maana ya familia
 
Hivi kuna wanaume ambao hawawapendi wake zao wanapokuwa wajawazito?

Sina uhakika kama kweli kuna wanaume hawawapendi wake zao kipindi cha mimba. Wangu nampenda wakati wote hadi imekuwa gumzo mtaani, tunafuatana kama kumbikumbi, jioni nikitoka job, tuko wote kwa kwenda mbele.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom