Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

Mzee/kijana acha hiyo mambo! Acha zipigwe,zirindimeeee. Soma historia vizuri, hakuna nchi imesonga mbele bila damu kumwagika. Acha woga. akiingia sebuleni, ataingia bedroom. Amka!
 
Mwanakijiji nimesoma Maelezo yako, Hizi kauli za viongozi wa Tanzania haziishii Tanzania tu bali hata vyombo vya nje vinanukuu na kufuatilia hizi habari sana...................................Lakini ni kweli hawa viongozi wamekurupuka?............................. Hivi tunajua report ya Inteligence kuhusu hili suala?...............................Tunajua hao Wamalawi wamefikia hatua gani kwenye kusuluisha hili wala? ................ Mwanakijiji umeshawahi kusikia au kuona activities za kijeshi za Malawi kwenye mpaka na ndani ya Ziwa, ...................... Nadhani ungefanya uchunguzi kwanza wa Kuona wa MAlawi wamejiandaa kwa kiasi gani na nini yupo nyuma ya hii chok0choko..................... Kama inavyojulikana huu mgogoro wa mpaka ni wa muda mrefu sasa, lakini kwa sasa Tanzania ianpeleka vifaa mpakani? Tanzania inafanya hivyo kutokana na Wamalawi wanavyofanya........................Kauli za viongozi zimekuja kutokana na Report walizopewa kutoka upande wa pili
 
Nilitamani sana kusikia kauli yako katika hili suala.......

Tamaa nyingine inachipuka katika nafsi yangu natamani kama wale wakubwa tunaodhani wanai backup Malawi natamani iwe kweli na nchi iende vitani ili tuchapwe na wamalawi, ni dhahiri kwa sasa Tanzania hatuna viongozi wa kuweza kutuhamisisha ili tuungane pamoja kwa maslahi ya taifa, wote malengo yao yanafanana ambayo ni kutuunganishe ili watugeuze madaraja kwa manufaa yao binafsi na familia zao.

Ufisadi umelisambaratisha taifa, tumepiga kelele kuwa taifa linasambaratika lakini wakatupuuza, wenyewe walidhani kusambaratika kwa taifa ni mpaka iwepo vita ya wenyewe kwa wenyewe, hawakuwahi kufikiria kuwa ile hali ya kudumaza hali za wananchi inaaibua na kujenga vinyongo, hasira, chuki na kusambaratisha kabisa umoja miongoni mwetu na hivyo kumpa nafasi ya ushindi mkubwa adui yeyote atakayekuja kusimama dhidi yetu hata kama ni dhaifu kwa kiwango kipi.

Wananchi hatuna tena ile spirit ya na uzalendo maana walituambia nchi ina wenyewe na kwa mujibu wa matendo yao na wakadhihirisha hayo kwa kugawana madaraka wao kwa wao, kufisadi nchi, kudumaza elimu, kutupiga mabomu tunawapoandamana kuwakumbusha kuhusu haki zetu.

Hata madai juu ya katiba mpya tukachaguliwa ya kuongea na hao wenye nchi. Kama vita itatokea kushindwa kwetu na Malawi ndiyo utakuwa mwanzo wa Tanzania mpya, lakini kama kwa bahati mbaya tukashinda, basi huo ndiyo utakuwa mwisho wetu wa Tanzania mbele ya hao wenye nchi....maana utakuwa ni ushindi mkubwa kwa mafisadi na mambweha hao.

Ili iote na kuleta uhai mpya mbegu ni lazima ioze kwanza. Nawashauri watanzania wote wenye mapenzi mema na nchi yao, wafunge na kuomba nguvu za kijeshi zitumike katika suala hili kwani tayari tu wadhaifu....na ninaiona Tanzania mpya yenye afya tele ikichipuka baada ya kushindwa kwetu, katika vita hiyo waliyoanza kuihubiri.
 
Kweli kabisa MM,viongozi wasituingize vitani bila sababu za msingi hekima ya kidiplomasia itumike,ni wazi na dalili ya woga kuonesha silaha pasi na kuitumia ni 'kama kuvua nguo' hadharani haifai.Nikupongeze MM kwa maoni yenye kulinda na kujenga taifa letu,serikali iwe inayatendea kazi maoni adimu kama yako
 
Hoja yako imekomaa, imeeleweka. mimi nashindwa kuelewa ni kwa nini baadhi ya wanasiasa wanakimbilia vyombo vya habari na kutoa misimamo mikubwa kama hii tena ya usalama wa taifa. Hawa ndo wale wenye tabia ya kuwaamrisha waandishi wanukuu maneno yao kama vile wao ndo wanawafundisha kazi. utawasikia wakisema; "NA KAMA WAANDISHI MPO ANDIKENI HILI" huko kutamba tamba namna hii ni kwa vile malawi ni nchi ndogo au? ingekuwa mfano ni Kenya ukali wa ungekuwa uleule kweli au ubgepungua kidogo?
 
kweli kabisa mm,viongozi wasituingize vitani bila sababu za msingi hekima ya kidiplomasia itumike,ni wazi na dalili ya woga kuonesha silaha pasi na kuitumia ni 'kama kuvua nguo' hadharani haifai.nikupongeze mm kwa maoni yenye kulinda na kujenga taifa letu,serikali iwe inayatendea kazi maoni adimu kama yako
natamani vita itokee, tupigwe sana tena sana.baada ya hapo tanzania tutakuwa wamoja mali zetu zitakuwa za watanzania wote, na kuwa na demokrasia ya kweli. Jammaaani mafisadi yanahitaji kungolewa na mtutu wa bunduki
 
Umesema vyema sana nakubaliana na wewe asilimia mia. Lakini nikusahihishe kidogo tu kuwa Tanzania haina uwezo wa kuipiga Malawi nina huakika na hilo.
Pili ikitokea vita nina tamani sana Tanzania ishindwe (mimi ni mtanzania ninaipenda sana nchi yangu Tanzania.). Hii inchi ya mafisadi ikipigwa then naamini kabisa itakuwa nchi ya watanzania baada ya Vita.

Tena ikiwezekana jeshi la Malawi litakapoingia nchini ijitahidi kuwamaliza hawa viongozi ili tutakapokabidhiwa hii nchi waipokee wazalendo
 
Kwa mimi naona busara itumike kama itashindikana basi hata tuwekeane terms na wamalawi kama wanachimba mafuta na gesi waishie kwenye nusu yao na nusu ya kwetu wasiingilie mbona diplomasia inayotakiwa hapo ni ndogo sana kuliko kukurupuka na mikauli ya vita?

Malawi ni ndugu zetu na ni waelewa labda wameamua wachokoze makusudi kutokana na sis kuwa na rasilimali nyingi lakini bado tu masikini kama wao, ndio maana wanataka kutuonyesha jinsi ya kutumia rasilimali na kuondokana na umasikini.

Sisapoti vita na sitaki itokee itumike diploamsia pekee kama kuna viongozi hawawezi diplomasia basi watuchukue hata sisi tukaongeze nguvu kuliko kusema tutapeleka jeshi nyasa afu baadae diplomasia ifuate hiyo itakuwa ni dharau na hata kama mimi ni mmalawi nitakataa majadiliano yoyote yale kwani tujadiliane wakati polisi wako nje nikikataa si utaniua?

Kwa hiyo kwa hili tusikurupike period.

Regards;
mzambia wa amani jirani na malawi.
 
duh! Kama ndio hivyo kwanini tusiwaachie tu hilo ziwa mambo yaishe kwasababu mbona maliasili ziko nyingi tu huku Tanzania

Japo hata wamalawi wakiamua kutuachia waTz hatutonufaika nalo zaidi itakuwa ni mafisadi na wawekezaji, basi pale itakapokuwa vita vijana tuwe mstari wa nyuma ili tushindwe na kufanikiwa kuwang'oa hawa mafisadi
 
Mimi tangu waanze kauli zao za kishetani nimekataa kabisa kuingizwa mkenge katika hili, Kikwete amekwenda Uganda kwenye mkutano wa Amani ya maziwa makuu, huku nyumbani vibaraka wake wanahubiri vita!! my self am out of this na niko tayari kuishi uhamishoni kuliko kuifia nchi inayotuuwa huku tukiwa hai.

Anayetaka kuninyooshea kidole mimi siyo Mzalendo na anaipe kwanza tafsiri isiyo na shaka ni nini maana ya neno uzalendo.

Ktk hili mkuu tupo wengi
 
huwezi kujua how correct uko kwenye hili. Msidhani wao watapigana hivyo vita shauri lenu!
The very obvious thing ni kuwa hii Vita imekuwa proveked na powers beyond Malawi. Ni katika kipindi hiki cha mzozo ambapo Malawi wameondolewa vikwazo vya kiuchumi na IMF, na kupewa fungu la kutosha, Marekani naye amewapa fungu fungu alillokuwa amelizuia kama haitoshi waziri wake wa mambo ya nje naye akafunga safari last week kweenda kuitembelea na kuahidi misaada zaidi...yote haya ni katika kipindi hiki kifupi yote hayo yanatokea wakati tangu rais wao ashike madaraka hajakanyaga hata nchi moja kwenda kujitambulisha wala kuomba omba.

Rais wetu anatakiwa atujibu swali hili....Je hiki ndicho alichorudi nacho kwenye bakuli lake? Maana alisema anasafiri huku na huko ili kuhemea tusife njaa, Je rais wa Malawi alienda nchi ipi kuomba omba? mbona anaonekana kupata full support, toka kwa wale wale ambao rais wetu alidai ni marafiki zake?
Malawi ni jezi tu lakini vita hatapigana yeye (Technically and Technologically as well as Economically), but let the war come ili Tanzania mpya iote.
 
Hatupo wamoja kiasi cha kupigana vita, hatuna imani na serikali na watendaji wake kiasi cha kushinda vita.....

Katika mfumo wetu huu uliodhaifu, chini ya taasisi ya urais isiyoweza kuendesha mambo mengi kwa mpigo, ni nani anaweza kukadiria dili za Familia ya Rais chini ya Ridhwan na mtandao kwenye kipindi cha vita??

Lakini pia tunaosema tupigwe, mnaelewa kupigwa ina maana gani kwenye vita??

Itoshe tu kusema.........
:flypig::yield::yield: "HAPANA, HATUHITAJI VITA"
 
Tulimshinda amini inayesadikika alikuwa na vifaa bora vya kivita kuliko sisi kwa kitu kimoja kikubwa.. Amini alitumia jeshi lake kupigana na Watanzania wote. Nyerere aliwatayarisha Watanzania wote, na wote walikuwa sehemu ya ile vita.. Hakika Tanzania ikiingia vitani kipindi hiki nchi ilivyokosa umoja itakuwa ngumu sana. HAWA VIONGOZI SINA UHAKIKA KAMA WANALIONA HILI

Mkuu wangekuwa wameliona hilo sidhani kama wangekurupuka na kuanza kuropoka maneno kama hayo na waombe Mungu isitoke maana wao pia lazima watalia na kusaga meno.
 
Hawana uwezo mkubwa wa kukaa kwenye meza yamajadiliano, kwa mfano wameshindwa kujadiliana na madaktari, waalimu, wazee wa community, wanafunzi kuhusu madai yao ya msingi na aghalabu wamekuwa wakikimbilia FFU kutuliza.

Lakini above all in times of war people make money, isije kuwa wanaombea vita ili wafaidi kwenye expenditure ya dharura wakati wa vita.
Nadhani uko sahihi hasa kwenye hilo la matumizi ya dharula. Usije kuta hapo inatafutwa fedha isiyokagulika kuendeshea kampeni 2015. Au watu wanataka kupata fedha kwa mara ya mwisho maana 2015 imekaa vibaya.
 
WaTz tutambue hata tukilipigania hili ziwa wataendelea kufaidi hao wenye meno basi ni bora tukae pembeni tubaki kuwa watazamaji wa hii vita kwani vita vya panzi furaha kwa kunguru, basi hii vita inaweza kutufanya kuwa kunguru yaani pindi Tz itakapochapwa ipasavyo ikawa mwanzo wa sisi kunufaika na rasilimali nyingine japo tutaipoteza hiyo moja
 
Kuelekea 2015, NITOKE VIPI? hapa hatujamsikia Amirijeshi Mkuu au Waziri wa Ulinzi au hata CDF, bali tunawaona wanasiasa ma-opportunists wakijipanga kutumia hii fursa waonekane wanaweza?

attachment.php
 

Attachments

  • Bounce back by Jacob Zuma.jpg
    Bounce back by Jacob Zuma.jpg
    21 KB · Views: 150
sioni haja ya nchi yetu kuingia vitani kama tumeshindwa kupambana kikamilifu vita vya ndani VITA DHIDI YA MAFISADI tutawezaje kushinda vita dhidi ya malawi? nijuavyo mimi mafisadi ni hatari mno kuliko hata hiyo malawi tunayotaka kupigana nayo.
 
Mmj that's very nice analysis. Jamani point hapa ni tabia ya serikali kutuhamisha mawazo na kubadili dira na kuacha mambo muhimu bila kujadiliwa/kufanyiwa kazi. Tumeshtuka. Ya madaktari yako wapi? Walimu? Achilia mbali mauaji ya raia wasiokuwa na hatia. Hakuna hata siku moja waziri hata rais kutangaza vita dhidi ya zuluma mbalimbali hapa nchini,au ujinga n.k mimi naona adui mkubwa yupo ndani ya nchi na sio nje ya nchi.na adui huyu ni CCM
 
Back
Top Bottom