Wanasiasa: Kwa nini mnaficha majina yenu humu ndani wakati tunajua mpo?

Status
Not open for further replies.
JF siyo jukwaa la siasa pekee, kuna wanasayansi na watu wa fani lukuki humu ndani why wanasiasa pekee, Chamsingi siyo kujuana majina humu ndani, vipi unatafuta ma-WAJINA zako nini KASHESHE.

Lets keep it rolling like this bado mapema watu ku-post majina ya kwenye birth certificate zao.
 
Ni aibu ya hali ya juu mwanasiasa ambaya anasema anatetea wananchi kuficha jina lake halisi akiwemo humu JF!


Binafsi nampongeza Dr. Slaa na Mh. Zitto kwa mara nyingine kuweka majina yao wazi... na hivyo pia kujua maoni yao katika mambo mbalimbali.

Ni heshima wanasiasa kuweka wazi majina yenu ili kuifanya JF kuwa chombo cha habari cha kuheshimika... na kupunguza wale wenzetu wanaofanya hapa ni mahali pa kupiga soga!

Mwanasiasa imara huwa hana woga wa kutoa maoni yake asikike! hata hivyo pia kwa kuwa wazi ana-promote transparency kwenye jamii yake.

Kwa vyovyote vile mnapoingia hapa kuna mnavyopata na tunawasikia mkitoa hoja kule kwenye lile jumba tukufu... tunaona kabisa maoni mumeyatoa hapa... ni wajibu wenu pia kurudishia jamii kidogo (social responsibility) kwa kutoa mawazo yenu ya ujumla na ya namna gani mnapenda JF iwe!

Mukiweka majina yenu... lengo la JF kuwa ya forum/jukwaa la KiJamii itakuwa imekamilika na kwa hakika tutaonekana sisi ni wazalendo wa hali ya juu kwa taifa letu.

Mwisho wenzetu mnaopenda matusi, kejeli na personality tupunguze tena ili kuvuta watu wengi makini.

Hakuna haja ya kutaja majina. Makombora ndio muhimu. Wachukue maoni yanayotolewa huku wayafanyie kazi. Kama wana mada tata waianike wapate mawazo. Sidhani kama jina litasaidia chochote. Hata hivyo wanawezajitokeza watu bandia wakijidai ni wanasiasa fulani. Utajuaje kama wanadanganya? Hoja tu ndio muhimu hapa.
 
Naona kuna wenye sura za Mkapa, Lowasa nk. Nani ana uhakika ndio wenyewe? Wakitaja utathibitishaje ndio haswa na sio bandia? Anza kutaja jina lako kamilin wewe, uliko, unafanya kazi gani nk. Tukutambue.
 
mimi sina haja ya kuwajua kwa lazima, ila ni kama test yao, kama wana double faces, kuna watu wamejikuta wameingia kwny ufisadi kiajabu wanatamani kutoka lakini SYSTEM inawavuta, hawana nguvu ya kushindana nayo wameamua kuside nayo ili japo wafaidi ugali.
Hama wewe bosi wako akikuambia anakupeleka kitengo ambacho utatakiwa kula nae, ukikataa kazi hakuna. utafanyaje?
Waacheni wajipatie nguvu na ushujaa hapa,
vita ikipata mwelekeo na nchi ikabadilika, wengi wataachana na corruption na uvivu, na uzembe
 
MWANAMALUNDI said:
Hilo jina la kasheshe ni la kwako??? Kumbuka mwanasiasa ni binadamu kama wewe. Ina maana na wewe ukijiunga na siasa utaweka jina lako la kweli hapa JF???

Tunachoangalia hapa ni hoja na si nani katoa hiyo hoja.


Nikiingia kwenye Siasa YES... by then I will be Public figure... sasa hivi ni Private figure... kwi kwi kwi

Wewe sio Rostam? Tumia lako la kweli basi... :)
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom