Mcheza Karate
JF-Expert Member
- Jun 30, 2011
- 690
- 350
Wadau naomba mnisaidie hii. Nilisimuliwa tu wakati naanza maisha ya ukanda huu wa pwani na nikaona baadaye kwa rafiki yangu. Sijui "mila" au utaratibu wa "sheria za nchi" au "sheria za uislamu" hasa upande huu wa pwani utakuta mwanaume anamtaka binti na wakaelewana safi kwa ridhaa yao na binti sio mwanafunzi au mke au mchumba wa mtu lakini baadaye wanakuja ndugu zake wakati mko "faragha" wanakuja na kusema wamekufumania. Hivyo kutakiwa binti kumwoa au kulipa fidia ya pesa Je huu mbona utaratibu ambao ndo mosi nimeuona ukanda huu tu wa pwani je ni sheria ya nchi, sheria ya dini au mila tu? Naomba mnielekeze kisheria zaidi maana hili ni jipya kwangu.