bibikuku
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 832
- 495
Vijana CCM wachangamkia Ubunge EAC
Leon Bahati | 22 March 2012 | Mwananchi
WANACHAMA 32 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamejitokeza kuwania nafasi nane za Ubunge wa Afrika Mashariki kupitia chama hicho tawala, wengi wao wakiwa ni vijana.
Kwa kawaida kila nchi mwanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC), hutoa wabunge tisa kwenye bunge hilo maalumu kwa ajili ya kujadili masuala nyeti.
Hapa nchini mchakato wa kuwapata wabunge umeanza na Ofisa Uchaguzi wa CCM, Rojas Romuli alithibitisha kuwa tayari wanachama 32 wameshachukua fomu kuwania nafasi za kuteuliwa na chama kwenye nafasi hizo.
Ingawa Romuli alikataa kuitaja orodha kamili ya waliochukua fomu hizo jana, habari za uhakika zilithibitisha majina ya watu kadhaa ambao walichukua fomu hizo.
Miongoni mwao ni pamoja na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Mkoa wa Arusha, James Ole Milya na Dk Zainab Ghama ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Kibaha Mjini.
Wengine wanaodaiwa kuchangamkia fomu hizo ni Dk Richard Kasunda, Janet Milya, Baraka Kange, John Ng'ongolo na Balozi Christopher Liundi.
Kwenye orodha hiyo pia wapo wabunge wawili wa Afika Mashariki waliojitokeza kutetea nafasi zao ambao ni Dk Aman Kabourou na Janet Mmary.
Romuli alikiri majina hayo kuwamo kwenye orodha hiyo , lakini akasisitiza kuwa chama kinawataka wanachama wengi zaidi kuendelea kujitokeza ili kuongeza ushindani.
Alisema kwenye orodha hiyo ya watu 32, wanaume ni 26, wanawake sita na robo tatu ya waliochukua fomu hizo ni vijana.Alisema mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu ni kesho jioni na mchakato wa kuanza kufanya mchujo "unatarajia kufanyika mapema iwezekanavyo."
Kulingana na bunge lililopita, Romuli alisema, CCM ilitoa wabunge wanane, watano wakitokea Tanzania Bara na watatu visiwani huku miongoni mwao wanawake wakiwa watatu.
Kwenye bunge hilo, vyama vya upinzani vilikuwa na mbunge mmoja na kwamba mpangilio huo unatarajiwa pia kujirudia tena.
MY OPINION!
Dr Kaborou hana tija, ni bora apumzike ama apumzishwe!