mwakajilae
Member
- Mar 11, 2011
- 58
- 46
Binafsi nimefuatilia kwa kirefu juu ya kauli aliyoitoa Comrade Zitto hivi karibuni kwamba anautaka Urais.
Zitto ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo,aliitoa kauli hiyo wakati Taifa lipo katika hali mbaya ya Uchumi, Siasa na Jamii isiyo na uhusiano wa Kitabaka.Alitoa kauli hiyo huku akichambua kwa kina jinsi ambavyo baadhi ya matatizo ya kitaifa yanavyolitafuna taifa,huku viongozi wakuu waliopewa dhamana wakikosa ujasiri na Uzalendo wa kimaamuzi wa kuyashughulikia ili yalete tija kwa wananchi wa Tanzania.
Kwa kifupi aliweza kudokeza vitu vya msingi ambavyo vinamfanya mtu kuwa Rais,kama uwezo,uzalendo na ujasiri wa kufanya maamuzi yatakayowaudhi wengi wanaojinufaisha na hali hii ya Taifa ilivyo.
Kuna watu ambao wameunga kauli ya Zitto na wengine wamekuja juu wakipinga hata kwa matusi huku wakikosa usitaarabu, hii ni mbaya na tunahitaji kujitafakali upya juu ya fikra hizi.
Binadamu tumeumbwa huku tukiwa tumezaliwa katika mazingira tofauti yenye Utamaduni,siasa na jamii iliyotofauti na jamii nyingine. Mazingira hayo ndiyo yanayomuumba mwanadamu akiwa mwenye fikra tofauti na mwingine, huku binadamu huyo akiwa amefinyangwa na taasisi za kijamii zinazotofautiana kwa ukubwa sana kimtizamo, taasisi kama Familia, shule, Dini na jamii inayomzunguka, hivi ndivyo vinavyomfanya Juma atofautiane kimawazo na Baraka au Daudi kutokana na tofauti ya kuzaliwa kwao na makuzi yao.
Hoja ya Zitto kuutaka Urais,hili ni suala linalojikita katika misingi mikuu ya Demokrasia na Katiba ya nchi.Misingi ya Katiba ni juu ya Haki ya Kupigiwa Kura na Haki ya Kupiga Kura.
Zitto alilifahamu hilo toka mapema, Aliutaka Ubunge toka akiwa Shule ya Msingi, Sekondari na Chuo kikuu, aliwaza kuwatumikia wananchi kupitia Ubunge, akautaka ubunge toka utotoni, alitangaza nia na alitimiza dhamira yake akiwa bado kijana mbichi. Katika historia ya jimbo la kigoma Kaskazini kwa Miaka 50 ya Uhuru amejijengea historia ya pekee kwa wakazi wa jimbo hilo kushuhudia mapinduzi makubwa ya kimaendeleo,ukitaka kubisha,nenda we mwenyewe ukajionee maendeleo ya kigoma Kaskazini,kabla ya Zitto kuongoza kigoma utaijua kigoma kaskazini ilikuwaje na sasa ipoje?huyu ndiye Zitto ninayemjua mimi. Hakuishia tuu kuwa mbunge wa watu wa KIgoma Kaskazini bali alikuwa mbunge wa Watanzani[Seneta] anayebisha afuatiliye Hansard za Bunge ili amfahamu Zitto kwa kazi yake na siyo vinginevyo.
Sasa Zitto anatangaza adhima ya kuomba kuomba kupigania kinyang'anyiro cha Urais,anao Uzalendo,anao Ujasiri na anao uwezo.
Watu wanakuja kwa hoja nyepesi kwamba huko ni kuwagawa wanachama!
Vipi CCM inaposema kwamba kuchagua Upinzani ni kUvuruga amani na umoja wa Kitaifa?kuna ukweli?
Kwanini kwa CCM iwe ni propaganda za hofu halafu CHADEMA tusema ni kukigawa chama?
Vyama vya upinzani vimekuja katika wakati ambao Tanzania tulikuwa tumejinyima haki ya kuamua na kujichagulia nuru au mwanga.Tulilazimishwa kuchaguwa giza huku tukiambiwa ile siyo giza bali ni mwanga?hivyo hata wenye akili waliimba nyimbo moja hata kama walikuwa hawakubaliani.
Vyama vya upinzani vinapaswa kuwa mfano mkubwa wa Demokrasia ya kweli,ambayo tumeihubiri kwa miongo miwili sasa.
Vyama vya Upinzani tunapaswa kuifundisha CCM siasa ya karne ya 21,Tunapaswa tuwafundishe muundo wa uongozi wa kitaasisi na jinsi masuala yanavyoshughulikiwa kiutaalamu.
Hilo ndilo lililo kuwa tumaini la mpambazuko wa Vyama Vingi.
Kijana kama Zitto anapojitokeza kuwania nafasi ambazo utamaduni wa Zamani ulikuwa unawanyima vijana,Inatakiwa tumsifu na kumpa ujasiri na siyo kumkatisha tamaa na dhamira yake kwa Taifa.
Nyerere alichukuwa nchi hii akiwa na umri wa miaka 39 kama sikosei,Nyerere hakuwa na Uzoefu wa Ubunge wala Uwaziri hata ukuu wa wilaya hakuwa nao. Zaidi ya harakati za mapambazuko ya Ukombozi. Lakini aliongoza Taifa hili kwa ufanisi mkubwa.
Aliunda baraza la mawaziri,wakuu wa wilaya na mikoa pamoja na makatibu wakuu wa wizara ambao kwa asilimia 75 walikuwa Vijana.Walifanya maamuzi kwa ujasiri na uzalendo mkubwa, waliwajibika kaadiri ya wakati ulivyo waruhusu.
Tanzania ikang'ara katika Siasa za jamii ya Kimataifa na kitaifa.Watu walitoka dunia nzima wakiwa wanakuja kuitafuta Tanzania na Falsafa ya Taifa la Tanzania.Mshikamano wa kitaifa uliimarika.
Leo hii wanapojitokeza Vijana wa kada mbalimbali kuwania nyadhifa mbalimbali ikiwemo hata ya Urais,wanatukumbusha historia ya miaka 1960's ya Uhuru iliyopita na miaka 25 ya Nyerere ikajenga historia tunayojivunia. Vijana haw wanakuja kwa wakati muafaka wa kuandika tena historia mpya ya miaka 50 ijayo kwa kuanzia, wakija na Falsafa mpya ya kuongoza na kutatua migogoro ya kitaifa juu ya uchumi na siasa yake.
Ujio wa katiba mpya unaenda kuamua swali la muda mrefu kwamba vijana wenye miaka 35 na kuendelea ambao Sera ya taifa haiwatambui kama Vijana,tuwaweke katika kundi lipi la kiuongozi,naamini Sera hiyo inawajua na kuwatambua kwamba wana nafasi ya kuwa marais wa nchi.
Watu wengi walimuogopa sana Kagame alipo chukua nchi mara baada ya mauaji ya kimbari, wakimpuuza kwamba mauaji na vurugu zingetawala uongozi wake.
Majibu tuliyo yapata ni maendeleo na mshikamano wa Kitaifa wa kupigiwa mfano, uadilifu wa kitaasisi ndicho tunachokiona sasa Rwanda, hiyo ni kazi ya Kagame.
Kiufupi nina amini katika demokrasia inayoonekana, demokrasia ya Ushindani, demokrasia ya kuomba kupigiwa kura na kupiga kura na siyo vinginevyo.
CHADEMA Tutasimama kwa kufuata maamuzi ya Kidemokrasia ambayo zao lake ni wanachama walio wajumbe wa Kamati kuu, Baraza kuu na hatimaye Mkutano mkuu na siyo zaidi ya hapo.
Uhuru wa kufikiri ni Uhuru wa kuamua.
Mwakajila ni Mwanachama wa CHADEMA na alikua Mkt wa Baraza la Vijana CHADEMA-Mbeya.
Zitto ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo,aliitoa kauli hiyo wakati Taifa lipo katika hali mbaya ya Uchumi, Siasa na Jamii isiyo na uhusiano wa Kitabaka.Alitoa kauli hiyo huku akichambua kwa kina jinsi ambavyo baadhi ya matatizo ya kitaifa yanavyolitafuna taifa,huku viongozi wakuu waliopewa dhamana wakikosa ujasiri na Uzalendo wa kimaamuzi wa kuyashughulikia ili yalete tija kwa wananchi wa Tanzania.
Kwa kifupi aliweza kudokeza vitu vya msingi ambavyo vinamfanya mtu kuwa Rais,kama uwezo,uzalendo na ujasiri wa kufanya maamuzi yatakayowaudhi wengi wanaojinufaisha na hali hii ya Taifa ilivyo.
Kuna watu ambao wameunga kauli ya Zitto na wengine wamekuja juu wakipinga hata kwa matusi huku wakikosa usitaarabu, hii ni mbaya na tunahitaji kujitafakali upya juu ya fikra hizi.
Binadamu tumeumbwa huku tukiwa tumezaliwa katika mazingira tofauti yenye Utamaduni,siasa na jamii iliyotofauti na jamii nyingine. Mazingira hayo ndiyo yanayomuumba mwanadamu akiwa mwenye fikra tofauti na mwingine, huku binadamu huyo akiwa amefinyangwa na taasisi za kijamii zinazotofautiana kwa ukubwa sana kimtizamo, taasisi kama Familia, shule, Dini na jamii inayomzunguka, hivi ndivyo vinavyomfanya Juma atofautiane kimawazo na Baraka au Daudi kutokana na tofauti ya kuzaliwa kwao na makuzi yao.
Hoja ya Zitto kuutaka Urais,hili ni suala linalojikita katika misingi mikuu ya Demokrasia na Katiba ya nchi.Misingi ya Katiba ni juu ya Haki ya Kupigiwa Kura na Haki ya Kupiga Kura.
Zitto alilifahamu hilo toka mapema, Aliutaka Ubunge toka akiwa Shule ya Msingi, Sekondari na Chuo kikuu, aliwaza kuwatumikia wananchi kupitia Ubunge, akautaka ubunge toka utotoni, alitangaza nia na alitimiza dhamira yake akiwa bado kijana mbichi. Katika historia ya jimbo la kigoma Kaskazini kwa Miaka 50 ya Uhuru amejijengea historia ya pekee kwa wakazi wa jimbo hilo kushuhudia mapinduzi makubwa ya kimaendeleo,ukitaka kubisha,nenda we mwenyewe ukajionee maendeleo ya kigoma Kaskazini,kabla ya Zitto kuongoza kigoma utaijua kigoma kaskazini ilikuwaje na sasa ipoje?huyu ndiye Zitto ninayemjua mimi. Hakuishia tuu kuwa mbunge wa watu wa KIgoma Kaskazini bali alikuwa mbunge wa Watanzani[Seneta] anayebisha afuatiliye Hansard za Bunge ili amfahamu Zitto kwa kazi yake na siyo vinginevyo.
Sasa Zitto anatangaza adhima ya kuomba kuomba kupigania kinyang'anyiro cha Urais,anao Uzalendo,anao Ujasiri na anao uwezo.
Watu wanakuja kwa hoja nyepesi kwamba huko ni kuwagawa wanachama!
Vipi CCM inaposema kwamba kuchagua Upinzani ni kUvuruga amani na umoja wa Kitaifa?kuna ukweli?
Kwanini kwa CCM iwe ni propaganda za hofu halafu CHADEMA tusema ni kukigawa chama?
Vyama vya upinzani vimekuja katika wakati ambao Tanzania tulikuwa tumejinyima haki ya kuamua na kujichagulia nuru au mwanga.Tulilazimishwa kuchaguwa giza huku tukiambiwa ile siyo giza bali ni mwanga?hivyo hata wenye akili waliimba nyimbo moja hata kama walikuwa hawakubaliani.
Vyama vya upinzani vinapaswa kuwa mfano mkubwa wa Demokrasia ya kweli,ambayo tumeihubiri kwa miongo miwili sasa.
Vyama vya Upinzani tunapaswa kuifundisha CCM siasa ya karne ya 21,Tunapaswa tuwafundishe muundo wa uongozi wa kitaasisi na jinsi masuala yanavyoshughulikiwa kiutaalamu.
Hilo ndilo lililo kuwa tumaini la mpambazuko wa Vyama Vingi.
Kijana kama Zitto anapojitokeza kuwania nafasi ambazo utamaduni wa Zamani ulikuwa unawanyima vijana,Inatakiwa tumsifu na kumpa ujasiri na siyo kumkatisha tamaa na dhamira yake kwa Taifa.
Nyerere alichukuwa nchi hii akiwa na umri wa miaka 39 kama sikosei,Nyerere hakuwa na Uzoefu wa Ubunge wala Uwaziri hata ukuu wa wilaya hakuwa nao. Zaidi ya harakati za mapambazuko ya Ukombozi. Lakini aliongoza Taifa hili kwa ufanisi mkubwa.
Aliunda baraza la mawaziri,wakuu wa wilaya na mikoa pamoja na makatibu wakuu wa wizara ambao kwa asilimia 75 walikuwa Vijana.Walifanya maamuzi kwa ujasiri na uzalendo mkubwa, waliwajibika kaadiri ya wakati ulivyo waruhusu.
Tanzania ikang'ara katika Siasa za jamii ya Kimataifa na kitaifa.Watu walitoka dunia nzima wakiwa wanakuja kuitafuta Tanzania na Falsafa ya Taifa la Tanzania.Mshikamano wa kitaifa uliimarika.
Leo hii wanapojitokeza Vijana wa kada mbalimbali kuwania nyadhifa mbalimbali ikiwemo hata ya Urais,wanatukumbusha historia ya miaka 1960's ya Uhuru iliyopita na miaka 25 ya Nyerere ikajenga historia tunayojivunia. Vijana haw wanakuja kwa wakati muafaka wa kuandika tena historia mpya ya miaka 50 ijayo kwa kuanzia, wakija na Falsafa mpya ya kuongoza na kutatua migogoro ya kitaifa juu ya uchumi na siasa yake.
Ujio wa katiba mpya unaenda kuamua swali la muda mrefu kwamba vijana wenye miaka 35 na kuendelea ambao Sera ya taifa haiwatambui kama Vijana,tuwaweke katika kundi lipi la kiuongozi,naamini Sera hiyo inawajua na kuwatambua kwamba wana nafasi ya kuwa marais wa nchi.
Watu wengi walimuogopa sana Kagame alipo chukua nchi mara baada ya mauaji ya kimbari, wakimpuuza kwamba mauaji na vurugu zingetawala uongozi wake.
Majibu tuliyo yapata ni maendeleo na mshikamano wa Kitaifa wa kupigiwa mfano, uadilifu wa kitaasisi ndicho tunachokiona sasa Rwanda, hiyo ni kazi ya Kagame.
Kiufupi nina amini katika demokrasia inayoonekana, demokrasia ya Ushindani, demokrasia ya kuomba kupigiwa kura na kupiga kura na siyo vinginevyo.
CHADEMA Tutasimama kwa kufuata maamuzi ya Kidemokrasia ambayo zao lake ni wanachama walio wajumbe wa Kamati kuu, Baraza kuu na hatimaye Mkutano mkuu na siyo zaidi ya hapo.
Uhuru wa kufikiri ni Uhuru wa kuamua.
Mwakajila ni Mwanachama wa CHADEMA na alikua Mkt wa Baraza la Vijana CHADEMA-Mbeya.