kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
WANANDOA wanaoendelea kuishi katika misuguano isiyopatiwa ufumbuzi kwa muda mrefu ni vyema wakajifunza kutokana na matukio yanayoendelea kuibuka maeneo mbalimbali nchini.
Ni hatari kuendelea kuishi katika uhusiano mbaya na mtu uliyeshirikiana naye kwa kiasi cha kupata watoto ambao kimsingi wanahitaji ushirikiano wa wazazi ili wapate malezi na makuzi bora.
Ingawa msingi wa ndoa ni upendo, Watanzania wengi wanaishi katika uhusiano mbaya wa mapenzi kiasi kwamba ndoa nyingi zimejengwa katika misingi tofauti na upendo wa kweli.
Hakuna ubishi kwamba wanandoa wengi wamegeuka waigizaji ambao wakiwa machoni pa jamii wanatambulika kama wanandoa wakati maisha yao halisi siyo hayo.
Jambo hili linasababisha mateso ya kisaikolojia na limeanza kusababisha maafa katika jamii. Ingawa maandiko ya dini kama ya Kikristo yanazuia ndoa kuvunjika, haiingii akilini watu wanaoishi bila chembe ya upendo kati yao, kiasi cha kugeuka maadui kuendelea kuishi chini ya mwamvuli wa ndoa.
Ni jukumu la kila anayeishi katika uhusiano wa aina hiyo, kufanya uamuzi na kuutekeleza kwa dhati. Ikiwa anaamua kuendelea kuishi na mwenzi kama mke na mume ni vyema kufanya hivyo kwa dhati.
Siyo leo mmeachana, kesho unataka kufahamu alichovaa amenunuliwa na nani au anaishi vipi. Ikiwa wewe ndiye mwenye makosa na umebaini hilo, jishushe, omba msamaha ukimaanisha na badili tabia yako.
Sababu nyingi zinatajwa kuwa chanzo cha uhusiano mbaya ndani ya ndoa, lakini moja kubwa ni wanandoa kukosa uaminifu. Tabia hiyo imewavaa wanandoa wa jinsi zote, mke na mume.
Upungufu wa uaminifu katika ndoa za sasa unaoongoza ni wa mtu mmoja au wanandoa wote kuwa na uhusiano wa mapenzi nje ya mwenzake. Lakini pia kuna upungufu wa uaminifu katika umiliki wa mali.
Kukosekana uaminifu ndani ya ndoa kunaibua matatizo mengine ambayo yasipoangaliwa kwa kina yanaweza kudhaniwa kuwa ndiyo chanzo cha ndoa kusambaratika.
Kwa kuwa dhana ya uchambuzi huu siyo aina ya uaminifu katika ndoa, narejea kwenye mada ya kuwataka waliyo ndani ya uhusiano mbaya wa mapenzi kufanya uamuzi na kuutekeleza kwa dhati.
Unakuta mtu ameishi na mwenzake kwa miaka 10 hata 20 anaibuka na kumtwisha mwenzake tuhuma akidai ni mwizi mchawi, mchafu au mzinzi.
Hivi mtu anaweza vipi kuishi chini ya paa moja na mke au mume mwenye tabia hizo kwa miaka zaidi ya 10, zaidi ya hayo akubali kuzaa naye watoto ilhali ikifahamu kufanya hivyo ni kuongeza uzao wenye asili ya tabia mbaya.
Hali hii inaibua hisia sahihi kwamba kiini cha mgogoro wa ndoa nyingi ni mmoja wa wanandoa au wote kujiingiza katika uhusiano wa kimapenzi ya nje jambo linalosababisha imani na upendo kupotea.
Mfano wa kilele cha kulea matatizo ndani ya ndoa ni tukio la usiku wa kuamkia Januari 8, mwaka huu ambapo mkazi wa Kijiji cha Gekrum, Wilaya ya Karatu, Evans Damian (43) aliua watoto wake wanne kabla ya yeye mwenyewe kujinyonga mpaka kufa kwa madai kwamba alikuwa na ugomvi na mke wake.
Watoto waliouawa kwa kukatwa kwa shoka na baba yao vichogoni ni Theophil (10) aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Karatu Mission, Ritha (8), Dibimo (4) na pacha wake Theodory (4) ambao walikuwa wanafunzi wa Shule ya Awali Karatu Mission.
Baada ya maziko ya watoto hao ambao hawakuwa na hatia yoyote, mama yao mzazi Paskaria Sixbelt (30) akazungumzia maisha ya ndoa yake kwamba yalikuwa na mgogoro uliowatenganisha tangu Agosti, mwaka jana.
Katika maelezo yake anasema walikutana na mumewe Karatu Mjini siku ya tukio na baada ya kuonana ugomvi mkubwa baina yao ulizuka. Mama huyo anadai kuwa kisa cha yote hayo ni baada ya mumewe kumuona akiwa amesuka nywele na kuvaa pete ambayo marehemu mumewe alihisi kuwa amevishwa na mwanamume mwingine.
Katika ugomvi huo, mwanamume huyo alimng'ata mkewe kidole cha kushoto mpaka akakikata kisha kukitema alipotoka hapo ndipo likafuata hilo la mauaji ya watoto wote na yeye mwenyewe kujinyonga mpaka kufa.
Inaelezwa kwamba kisa cha kuachana kwao ni madai kwamba mke alikuwa akiiba fedha dukani kwao hayo mengine ya wivu yanatokea wapi hasa ikizingatiwa kwamba walishatengana kwa takriban miezi mitano?
Kwa akili ya kawaida isiyohitaji mafunzo ya saikolojia ni dhahiri kwamba mwanamume huyo alishaathirika kisaikolojia. Asingejiua, angepimwa baada ya kuua watoto wake au hata baada ya kumng'ata mkewe kidole hadi kukikata, hilo lingethibitika.
Sasa kwa nini watu wafikishane huko? Unayeishi na mke, mume au mzazi mwenzako kwa migogoro isiyo na ukomo tena usiyofahamu hatima yake, unafiki nini unaposikia hayo yakitokea?
Wahenga walisema, ukiona mwenzako ananyolewa na wewe za kwako tia maji. Mambo mengi yanatokea katika familia nyingi za nchini ambayo bahati mbaya yanawatesa watoto wasio na hatia.
Ingawa dini zote zinachukia talaka lakini kuliko wanandoa kutesana mpaka kufikia hatua ya kusababisha maafa ni bora uamuzi mbadala ukachukuliwa na kutekelezwa kwa dhati ili wasio na hatia wasiendelee kuumia.
Ni hatari kuendelea kuishi katika uhusiano mbaya na mtu uliyeshirikiana naye kwa kiasi cha kupata watoto ambao kimsingi wanahitaji ushirikiano wa wazazi ili wapate malezi na makuzi bora.
Ingawa msingi wa ndoa ni upendo, Watanzania wengi wanaishi katika uhusiano mbaya wa mapenzi kiasi kwamba ndoa nyingi zimejengwa katika misingi tofauti na upendo wa kweli.
Hakuna ubishi kwamba wanandoa wengi wamegeuka waigizaji ambao wakiwa machoni pa jamii wanatambulika kama wanandoa wakati maisha yao halisi siyo hayo.
Jambo hili linasababisha mateso ya kisaikolojia na limeanza kusababisha maafa katika jamii. Ingawa maandiko ya dini kama ya Kikristo yanazuia ndoa kuvunjika, haiingii akilini watu wanaoishi bila chembe ya upendo kati yao, kiasi cha kugeuka maadui kuendelea kuishi chini ya mwamvuli wa ndoa.
Ni jukumu la kila anayeishi katika uhusiano wa aina hiyo, kufanya uamuzi na kuutekeleza kwa dhati. Ikiwa anaamua kuendelea kuishi na mwenzi kama mke na mume ni vyema kufanya hivyo kwa dhati.
Siyo leo mmeachana, kesho unataka kufahamu alichovaa amenunuliwa na nani au anaishi vipi. Ikiwa wewe ndiye mwenye makosa na umebaini hilo, jishushe, omba msamaha ukimaanisha na badili tabia yako.
Sababu nyingi zinatajwa kuwa chanzo cha uhusiano mbaya ndani ya ndoa, lakini moja kubwa ni wanandoa kukosa uaminifu. Tabia hiyo imewavaa wanandoa wa jinsi zote, mke na mume.
Upungufu wa uaminifu katika ndoa za sasa unaoongoza ni wa mtu mmoja au wanandoa wote kuwa na uhusiano wa mapenzi nje ya mwenzake. Lakini pia kuna upungufu wa uaminifu katika umiliki wa mali.
Kukosekana uaminifu ndani ya ndoa kunaibua matatizo mengine ambayo yasipoangaliwa kwa kina yanaweza kudhaniwa kuwa ndiyo chanzo cha ndoa kusambaratika.
Kwa kuwa dhana ya uchambuzi huu siyo aina ya uaminifu katika ndoa, narejea kwenye mada ya kuwataka waliyo ndani ya uhusiano mbaya wa mapenzi kufanya uamuzi na kuutekeleza kwa dhati.
Unakuta mtu ameishi na mwenzake kwa miaka 10 hata 20 anaibuka na kumtwisha mwenzake tuhuma akidai ni mwizi mchawi, mchafu au mzinzi.
Hivi mtu anaweza vipi kuishi chini ya paa moja na mke au mume mwenye tabia hizo kwa miaka zaidi ya 10, zaidi ya hayo akubali kuzaa naye watoto ilhali ikifahamu kufanya hivyo ni kuongeza uzao wenye asili ya tabia mbaya.
Hali hii inaibua hisia sahihi kwamba kiini cha mgogoro wa ndoa nyingi ni mmoja wa wanandoa au wote kujiingiza katika uhusiano wa kimapenzi ya nje jambo linalosababisha imani na upendo kupotea.
Mfano wa kilele cha kulea matatizo ndani ya ndoa ni tukio la usiku wa kuamkia Januari 8, mwaka huu ambapo mkazi wa Kijiji cha Gekrum, Wilaya ya Karatu, Evans Damian (43) aliua watoto wake wanne kabla ya yeye mwenyewe kujinyonga mpaka kufa kwa madai kwamba alikuwa na ugomvi na mke wake.
Watoto waliouawa kwa kukatwa kwa shoka na baba yao vichogoni ni Theophil (10) aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Karatu Mission, Ritha (8), Dibimo (4) na pacha wake Theodory (4) ambao walikuwa wanafunzi wa Shule ya Awali Karatu Mission.
Baada ya maziko ya watoto hao ambao hawakuwa na hatia yoyote, mama yao mzazi Paskaria Sixbelt (30) akazungumzia maisha ya ndoa yake kwamba yalikuwa na mgogoro uliowatenganisha tangu Agosti, mwaka jana.
Katika maelezo yake anasema walikutana na mumewe Karatu Mjini siku ya tukio na baada ya kuonana ugomvi mkubwa baina yao ulizuka. Mama huyo anadai kuwa kisa cha yote hayo ni baada ya mumewe kumuona akiwa amesuka nywele na kuvaa pete ambayo marehemu mumewe alihisi kuwa amevishwa na mwanamume mwingine.
Katika ugomvi huo, mwanamume huyo alimng'ata mkewe kidole cha kushoto mpaka akakikata kisha kukitema alipotoka hapo ndipo likafuata hilo la mauaji ya watoto wote na yeye mwenyewe kujinyonga mpaka kufa.
Inaelezwa kwamba kisa cha kuachana kwao ni madai kwamba mke alikuwa akiiba fedha dukani kwao hayo mengine ya wivu yanatokea wapi hasa ikizingatiwa kwamba walishatengana kwa takriban miezi mitano?
Kwa akili ya kawaida isiyohitaji mafunzo ya saikolojia ni dhahiri kwamba mwanamume huyo alishaathirika kisaikolojia. Asingejiua, angepimwa baada ya kuua watoto wake au hata baada ya kumng'ata mkewe kidole hadi kukikata, hilo lingethibitika.
Sasa kwa nini watu wafikishane huko? Unayeishi na mke, mume au mzazi mwenzako kwa migogoro isiyo na ukomo tena usiyofahamu hatima yake, unafiki nini unaposikia hayo yakitokea?
Wahenga walisema, ukiona mwenzako ananyolewa na wewe za kwako tia maji. Mambo mengi yanatokea katika familia nyingi za nchini ambayo bahati mbaya yanawatesa watoto wasio na hatia.
Ingawa dini zote zinachukia talaka lakini kuliko wanandoa kutesana mpaka kufikia hatua ya kusababisha maafa ni bora uamuzi mbadala ukachukuliwa na kutekelezwa kwa dhati ili wasio na hatia wasiendelee kuumia.