Ndugu wana JF,
Kila anayefuatilia siasa za hapa nyumbani anajua nchi yetu inapitia kwenye mageuzi makubwa ya kisiasa huku CCM ikiangamia, CHADEMA wao wanashamili kwa afya. Kwa sasa Chadema wamekuwa wakivuna wanachama toka CCM, binafsi jambo hili sio zuri kwa chama kinachotaka kuleta mageuzi ya kweli, hizi ndo sababu zangu kwa nini naanza kuona mwisho mbaya kwa CHADEMA:
1. Itashindwa kudhibiti hawa watu wanaokimbilia maana ni watu ambao haijawalea, ni sawa na kuchukua mtoto aliyekulia malezi ya wazazi wengine ukataka kumlea wewe, atakusumbua sana sana. Chadema wameweza kuwazibiti kina Zito, Mnyika na wengine kwa sababu wamewalea tokea utoto wao wa kisiasa.
2. Italeta chuki kwa wanachama ndani ya Chadema ambao wapo muda mrefu maana wengi wa wanaohamia wanataka nafasi za uongozi mfano kugombea ubunge, wale walikitumia chama kwa muda mrefu wanaachwa, hii ni hatari kubwa.
3. Harufu ya U-CCM haijaondoka kwa hawa wanaohamia, mimi naamini mabadiliko ya kweli yatapatikana kwa kuanza upya na watu wapya wasiokuwa na harufu ya enzi tunazozichukia, hawa wahamiaji wana damu za CCM, wana mitandao yao bado inayowaunganisha. Huwezi kushona nguo mpya ukawa unaiwekea viraka vya nguo ya zamani iliyozeeka.
4. Chadema kwa kupokea wakimbizi toka CCM itaonekana haina tofauti kabisa na CCM maana watu ni wale wale ila wamekuja upande wa pili na kubadili mavazi yao tu.
Mwisho nawashauri CHADEMA wawapokee hawa wakimbizi toka CCM ila isiwapatie uongozi bali wawe wanachama wa kawaida na waanzie ngazi za chini kama ilivyo kwa watu wengine wa chini ndani ya chama na si leo tu kahamia kesho anagombea ubunge, kama Chadema wataendelea na tabia hii, basi mie nasema wajiandae kwa kifo cha kisiasa, wao eti wanasema wanapokea watu safi tu kutoka CCM, wanajidanganya sana, haitachukua muda kabla hatujaanza kuona mwisho wa CHADEMA.
Nawasilisha.
Kivipi?. Thibitisha.nadhani hata wewe unahisi
Acha ngonjera zisizo na mantiki wewe mwanzoni unaonyesha wazi hukutaka hao "wageni" wapokelewe mwishoni "wawapokee lakini wasipate vyeo. CDM ni Gwiji la kisiasa TZ na Africa huwezi kutoa utabiri wa ajabu kama huu.Ndugu wana JF,
Kila anayefuatilia siasa za hapa nyumbani anajua nchi yetu inapitia kwenye mageuzi makubwa ya kisiasa huku CCM ikiangamia, CHADEMA wao wanashamili kwa afya. Kwa sasa Chadema wamekuwa wakivuna wanachama toka CCM, binafsi jambo hili sio zuri kwa chama kinachotaka kuleta mageuzi ya kweli, hizi ndo sababu zangu kwa nini naanza kuona mwisho mbaya kwa CHADEMA:
1. Itashindwa kudhibiti hawa watu wanaokimbilia maana ni watu ambao haijawalea, ni sawa na kuchukua mtoto aliyekulia malezi ya wazazi wengine ukataka kumlea wewe, atakusumbua sana sana. Chadema wameweza kuwazibiti kina Zito, Mnyika na wengine kwa sababu wamewalea tokea utoto wao wa kisiasa.
2. Italeta chuki kwa wanachama ndani ya Chadema ambao wapo muda mrefu maana wengi wa wanaohamia wanataka nafasi za uongozi mfano kugombea ubunge, wale walikitumia chama kwa muda mrefu wanaachwa, hii ni hatari kubwa.
3. Harufu ya U-CCM haijaondoka kwa hawa wanaohamia, mimi naamini mabadiliko ya kweli yatapatikana kwa kuanza upya na watu wapya wasiokuwa na harufu ya enzi tunazozichukia, hawa wahamiaji wana damu za CCM, wana mitandao yao bado inayowaunganisha. Huwezi kushona nguo mpya ukawa unaiwekea viraka vya nguo ya zamani iliyozeeka.
4. Chadema kwa kupokea wakimbizi toka CCM itaonekana haina tofauti kabisa na CCM maana watu ni wale wale ila wamekuja upande wa pili na kubadili mavazi yao tu.
Mwisho nawashauri CHADEMA wawapokee hawa wakimbizi toka CCM ila isiwapatie uongozi bali wawe wanachama wa kawaida na waanzie ngazi za chini kama ilivyo kwa watu wengine wa chini ndani ya chama na si leo tu kahamia kesho anagombea ubunge, kama Chadema wataendelea na tabia hii, basi mie nasema wajiandae kwa kifo cha kisiasa, wao eti wanasema wanapokea watu safi tu kutoka CCM, wanajidanganya sana, haitachukua muda kabla hatujaanza kuona mwisho wa CHADEMA.
Nawasilisha.
Tutajie ufisadi wa walio hamia Chadema...
Kweli,cha muhimu ni KUFUATA kanuni za CHADEMA,lakini under DR.WILLBROD SLAA wamechemka mapema mno watastukiwa,wamuulize Shibuda ambaye anabye time kidogo waachane naye. MUHIMU NI MBOWE,ARFI,DR.SLAA,ZITTO NA NAMAKAMANDA WA UKWELI WAPOKEENI MAANA NI HAKI YAO KUJIUNGA CHADEMA,LAKINI KUWENI MAKINI HASA WASIJE WAKAWAKUTA VIJANA HALISI WA CHADEMA AFU MKAANZA KUWAPUUZA,HAPO ITAKUWA NI MBAYA SANA.WAJE LAKINI WAHESHIMU CHAMA NA MUWAANGALIE MIENENDO YAO MAANA WANAMARAFIKI MAFISADI WATOKAKO NA HATA WAO WANA ELEMENT HIZO MSIPOWAZIBITI. WATAWEZA KUSEMA KWELI "SISI TUNA MUNGU WAO WANA PESA" AU NDO WANATAKA KUGEUZA KAULI WAKIJA CHADEMA. WACHUNGUZWE KWA MAKINI SANA.
Hivi Chadema ndio kitu gani hasa.
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".
CHADEMA ni Alfa na Omega ktk mapinduzi ya siasa ya kweli ktk kupigania haki za walipa kodi, Na bado, 2015 ndo hasa gharika kuu la CCM, Yanayotokea Arusha na maeneo mengine ni mvua za rasharasha. Its total M4C