Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Tangu hotuba ya JK itolewe, nimekuwa nikisikia kupitia vyombo vya habari kuwa wako watu wanashawishi watu waiunge mkono.
Lakini mimi kwa sehemu kubwa sikubaliani na mambo mengi aliyosema kikwete maana alipokuwa akitangaza hotuba yake hiyo yenye majisifu mengi nilikuwa katika ziara ya vijijini katika wilaya ya Muleba huko Kagera.
Nilichoona kwa kweli nilishangaa sana kama kuna sehemu zenye dhiki kiasi hiki. Kwanza sikuwahi kufikiri kwamba kuna sehemu katika nchi hii barabara kwao ni hadithi lakini watu wakiwa wamejaa umasikini usiosemekana. ahaaaaaa ni mambo ya kushanagaza kwamba Tanzania bado kuna hali kama hii huku tukijisifu saaaaaaaaaaaana.
Bado kuna shule za msingi ambazo zimejengwa kwa nyasi na miti, na zingine hazina viwango kwani zinaweza kuwaangukia wanafunzi wakati wowote.
Nimekuwa katika shule ambayo wanafuzi wa darasa la 5 na 6 wanakaa chini kama picha nilizounganisha zinavyoonyesha. Je hapa kuna mategemeo ya kupata wana teknolojia na wanasayansi mahili katika karne hizi kweli?
Kama watoto wetu watasoma katika mazingira haya nakwambia hakuna lolote la kutegemea labda kama watoto wa mafisadi peke yao wataendelea kutawala na kutuibia kama baba zao.
Baadhi ya vijiji wanatembea kilometa 40 kufuata huduma za afya wakati maji salama ni hadithi maana wananyang'anyana na mifugo kama ng'ombe.
Sasa sijui wanaandamana kumdanganya nani?
Tunataka kuwaangalia wote wanaoshawishi watu kuandamana hasa mijini na tunataka tuone kama si hao mafisadi na ndugu zao wanaofahidi pesa zetu za wizi alizowasamehe wasilipe.
Tukatae upuuzi huu wa kuandamana kuunga mkono maneno yasiyokuwa na maana.
Viongozi wa upinzani mko wapi? wakiandamana sisiemu leo nyie nanyi anzisheni ya kwenu kesho. Watu wanadanganywa kweli.
Mungu isaidie Tanzania itoke kwenye dimbwi la viongozi waongo na walaghai. Maana wewe ushindwi na lolote.
Lakini mimi kwa sehemu kubwa sikubaliani na mambo mengi aliyosema kikwete maana alipokuwa akitangaza hotuba yake hiyo yenye majisifu mengi nilikuwa katika ziara ya vijijini katika wilaya ya Muleba huko Kagera.
Nilichoona kwa kweli nilishangaa sana kama kuna sehemu zenye dhiki kiasi hiki. Kwanza sikuwahi kufikiri kwamba kuna sehemu katika nchi hii barabara kwao ni hadithi lakini watu wakiwa wamejaa umasikini usiosemekana. ahaaaaaa ni mambo ya kushanagaza kwamba Tanzania bado kuna hali kama hii huku tukijisifu saaaaaaaaaaaana.
Bado kuna shule za msingi ambazo zimejengwa kwa nyasi na miti, na zingine hazina viwango kwani zinaweza kuwaangukia wanafunzi wakati wowote.
Nimekuwa katika shule ambayo wanafuzi wa darasa la 5 na 6 wanakaa chini kama picha nilizounganisha zinavyoonyesha. Je hapa kuna mategemeo ya kupata wana teknolojia na wanasayansi mahili katika karne hizi kweli?
Kama watoto wetu watasoma katika mazingira haya nakwambia hakuna lolote la kutegemea labda kama watoto wa mafisadi peke yao wataendelea kutawala na kutuibia kama baba zao.
Baadhi ya vijiji wanatembea kilometa 40 kufuata huduma za afya wakati maji salama ni hadithi maana wananyang'anyana na mifugo kama ng'ombe.
Sasa sijui wanaandamana kumdanganya nani?
Tunataka kuwaangalia wote wanaoshawishi watu kuandamana hasa mijini na tunataka tuone kama si hao mafisadi na ndugu zao wanaofahidi pesa zetu za wizi alizowasamehe wasilipe.
Tukatae upuuzi huu wa kuandamana kuunga mkono maneno yasiyokuwa na maana.
Viongozi wa upinzani mko wapi? wakiandamana sisiemu leo nyie nanyi anzisheni ya kwenu kesho. Watu wanadanganywa kweli.
Mungu isaidie Tanzania itoke kwenye dimbwi la viongozi waongo na walaghai. Maana wewe ushindwi na lolote.