Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Ndio, inaweza kutokea wanandoa mkajikuta mna wakati mgumu kifedha. Kama mnavyojua kwamba hali ya uchumi imebadilika na maisha yamekuwa magumu sana, inaweza ikawa imesababishwa na kuyumba kwa biashara zenu, au mmoja wa wanandoa kufukuzwa kazi au labda tu niseme kwa kifupi kuwa familia imekumbwa na mgogoro wa kiuchumi.
Je ninyi kama wanandoa mnafanya nini ili kuondokana na jinamizi hilo la mgogoro wa kiuchumi?
Hapa chini nitajaribu kuainisha hatua tano za kuchukua:
1. Kuwa na matumaini- hata kama hali ni ngumu kiasi gani, kuwa na matumaini ni hatua muhimu sana itakayowawezesha wanandoa kuondokana na msongo wa mawazo. Kuwa na hali ngumu hakumaanishi kwamba ndio mwisho wa maisha na kuwa na matuamaini ni moja ya nguzo muhimu zitakawafanya mfikiri vizuri ili kuondokana na hali hiyo
2. Umoja ni nguvu- Kuna usemi usemao umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, msemo huu una maana pana sana, maisha yetu kwa kiasi kikubwa yanategemea ushirikiano ili kufikia malengo yetu, iwe ni huko makazini kwetu, katika biashara zetu na hata katika ndoa zetu, tunahitaji sana kushirikiana ili kumudu kufikia malengo yetu. Kama wanandoa wanakumbwa na hali ngumu kiuchumi halafu kila mmoja akawa anajali maisha yake itawachukua karne kuondokana na hali hiyo au ndoa hiyo inaweza kukumbwa na mgogoro mkubwa na hata kuvunjika.
3. Matumizi- Usisubiri mpaka hali iwe mbaya sana kiuchumi ndiyo mchukue maamuzi magumu ya kuachana na matumizi yasiyo ya lazima. Inatakiwa matumizi yasiyo ya lazima yasitishwe mara moja. Manunuzi ya vipodozi ghali kwa wanawake, simu za gharama au kamera kwa wanaume zisubiri kwanza hali ya uchumi itengemae. Kumbukeni kujiuliza kabla ya manunuzi kama ni muhimu kununua bidhaa hiyo kwa wakati huo au inaweza kusubiri. Ni vyema wote mkajadili kwa kuangalia faida na hasara za kununua bidhaa hiyo.
4. Kuomba msaada-Msione aibu kuomba msaada pale inapobidi, kwa mfano wazazi au marafiki wa karibu ni vyema ukawashirikisha katika masaibu uliyo nayo, wanaweza kuwa msaada mkubwa kwenu na sio lazima uwe msaada wa fedha bali pia hata wa mawazo.
5. Madeni-kama mnadaiwa ni vyema kuwajulisha wadeni wenu hali yenu kifedha ilivyo kabla ya tarehe mliyoahidi kulipa haijafika. Hiyo itakusaidia kuwajengea uaminifu kwao na huenda wengine wakawasaidia kuondokana na jinamizi hilo la ukata.
Kama mkikubaliana kama familia kufuata hizo hatua tano, basi mnaweza kuondokana na jakamoyo na maisha mkayaona ya kawaida.
Je ninyi kama wanandoa mnafanya nini ili kuondokana na jinamizi hilo la mgogoro wa kiuchumi?
Hapa chini nitajaribu kuainisha hatua tano za kuchukua:
1. Kuwa na matumaini- hata kama hali ni ngumu kiasi gani, kuwa na matumaini ni hatua muhimu sana itakayowawezesha wanandoa kuondokana na msongo wa mawazo. Kuwa na hali ngumu hakumaanishi kwamba ndio mwisho wa maisha na kuwa na matuamaini ni moja ya nguzo muhimu zitakawafanya mfikiri vizuri ili kuondokana na hali hiyo
2. Umoja ni nguvu- Kuna usemi usemao umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, msemo huu una maana pana sana, maisha yetu kwa kiasi kikubwa yanategemea ushirikiano ili kufikia malengo yetu, iwe ni huko makazini kwetu, katika biashara zetu na hata katika ndoa zetu, tunahitaji sana kushirikiana ili kumudu kufikia malengo yetu. Kama wanandoa wanakumbwa na hali ngumu kiuchumi halafu kila mmoja akawa anajali maisha yake itawachukua karne kuondokana na hali hiyo au ndoa hiyo inaweza kukumbwa na mgogoro mkubwa na hata kuvunjika.
3. Matumizi- Usisubiri mpaka hali iwe mbaya sana kiuchumi ndiyo mchukue maamuzi magumu ya kuachana na matumizi yasiyo ya lazima. Inatakiwa matumizi yasiyo ya lazima yasitishwe mara moja. Manunuzi ya vipodozi ghali kwa wanawake, simu za gharama au kamera kwa wanaume zisubiri kwanza hali ya uchumi itengemae. Kumbukeni kujiuliza kabla ya manunuzi kama ni muhimu kununua bidhaa hiyo kwa wakati huo au inaweza kusubiri. Ni vyema wote mkajadili kwa kuangalia faida na hasara za kununua bidhaa hiyo.
4. Kuomba msaada-Msione aibu kuomba msaada pale inapobidi, kwa mfano wazazi au marafiki wa karibu ni vyema ukawashirikisha katika masaibu uliyo nayo, wanaweza kuwa msaada mkubwa kwenu na sio lazima uwe msaada wa fedha bali pia hata wa mawazo.
5. Madeni-kama mnadaiwa ni vyema kuwajulisha wadeni wenu hali yenu kifedha ilivyo kabla ya tarehe mliyoahidi kulipa haijafika. Hiyo itakusaidia kuwajengea uaminifu kwao na huenda wengine wakawasaidia kuondokana na jinamizi hilo la ukata.
Kama mkikubaliana kama familia kufuata hizo hatua tano, basi mnaweza kuondokana na jakamoyo na maisha mkayaona ya kawaida.