Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,806
- 15,379
Je unadhani kwenye vurugu za kindoa, fedha haina mchango wake? Kama unadhani hivyo, utakuwa umekosea sana. Hebu soma kuhusiana na utafiti huu uliofanyika kule Marekani.
Utafiti uliowahi kufanywa na taasisi ya Harris Interactive (Harris Interactive Poll for Men, Love & Sex) ya nchini Marekani ilibaini kwamba, asilimia 38 ya wanaume na wanawake walioshiriki kura ya Taifa ya maoni kuhusiana na mapenzi nchini humo walisema fedha ndilo tatizo nambari moja linalopelekea kudumaa, kusinyaa ama hata kufikia tamati kwa ndoa.
Mara nyingi matatizo ya fedha hutokana na ukweli kwamba wenza huwa na malengo tofauti ya kifedha na wakati mwingine ni katika mambo ya kawaida tu. Kwa mfano mwanmke anataka Pete ya Dhahabu wakati mume anataka Televisheni ya kioo cha tambarare (Flat Screen TV).
Hii hutokana na kukosekana kwa mawasiliano ya kutosha kuhusiana na malengo hayo na hasa pale ambapo mtu mmoja ndiye anayewajibika za Ankara (bill) nyingi za manunuzi na ikiwa watu hao hawapati muda wa kutosha wa kuzungumzia mambo mengine zaidi ya kupeana madai ya kile kinachotakiwa kupewa kipaumbele.
Tatizo la fedha pia mara nyingi limeonekana kuchangia kwenye kutokea kwa matatizo mengine. Kukiwa na tatizo la fedha tegemea kupewa nafasi chache sana za kufanya tendo la ndoa na mwenzi wako, usitarajie kutayarishiwa chakula kizuri na chochote kile unachotarajia kupata kwa mwenza wako.
Najua mtauliza chanzo, bofya hapa: How Money Ruins Relationshipshttp://www.articledashboard.com/Article/How-Money-Ruins-Relationships/982316
Utafiti uliowahi kufanywa na taasisi ya Harris Interactive (Harris Interactive Poll for Men, Love & Sex) ya nchini Marekani ilibaini kwamba, asilimia 38 ya wanaume na wanawake walioshiriki kura ya Taifa ya maoni kuhusiana na mapenzi nchini humo walisema fedha ndilo tatizo nambari moja linalopelekea kudumaa, kusinyaa ama hata kufikia tamati kwa ndoa.
Mara nyingi matatizo ya fedha hutokana na ukweli kwamba wenza huwa na malengo tofauti ya kifedha na wakati mwingine ni katika mambo ya kawaida tu. Kwa mfano mwanmke anataka Pete ya Dhahabu wakati mume anataka Televisheni ya kioo cha tambarare (Flat Screen TV).
Hii hutokana na kukosekana kwa mawasiliano ya kutosha kuhusiana na malengo hayo na hasa pale ambapo mtu mmoja ndiye anayewajibika za Ankara (bill) nyingi za manunuzi na ikiwa watu hao hawapati muda wa kutosha wa kuzungumzia mambo mengine zaidi ya kupeana madai ya kile kinachotakiwa kupewa kipaumbele.
Tatizo la fedha pia mara nyingi limeonekana kuchangia kwenye kutokea kwa matatizo mengine. Kukiwa na tatizo la fedha tegemea kupewa nafasi chache sana za kufanya tendo la ndoa na mwenzi wako, usitarajie kutayarishiwa chakula kizuri na chochote kile unachotarajia kupata kwa mwenza wako.
Najua mtauliza chanzo, bofya hapa: How Money Ruins Relationshipshttp://www.articledashboard.com/Article/How-Money-Ruins-Relationships/982316