Wanandoa kufanana

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,319
Hivi inakuwaje unakuta mara nyingi mume na mke waliokaa kwa miaka kadhaa wanafanana sura?
 
Ni masuala ya kisaikolojia zaidi. Kwa kawaida tunavutiwa na watu wanaofanana nasi au wanaofanana na wale wanaotuzunguka katika familia yetu: dada, mama, kaka, baba, nk. Na mara nyingi hawa wanafamilia zetu ni watu tunaofanana nao hata kwa sura. Kumbe hata katika mahusiano na watu wa nje (wenzi) tunakuwa na mwelekeo wa kuvutiwa na wanaotufanana au wale wanaofanana na wanafamilia zetu; ambao nao kwa kawaida wanatufanana kwa sababu ya uhusiano wa kinasaba. Ndo mana unakuta mume na mke mara nyingine wanafanana kwa sura.
 
Back
Top Bottom