Wananchi wavamia shamba la Nabii Josephati Mwingira Break Throw Mapinga

Mwamakula

JF-Expert Member
Nov 7, 2010
1,890
382
Wananch wa Bagamoyo eneo la Mapinga Wamevamia Shamba la Nabii na Mtume Josephati Mwingira. Juzi Mwingira alikwenda huko akiwa na walinzi wa Kimasai walioambatana Na Mabounce na kuendesha operation ya kuwaondoa kwa nguvu wananchi hao na kuzua mapigano makali ambapo leo kuna kikao cha ulinzi na usalama kujadili suala hilo kinachofanyika shule ya Sekondari ya Lord baden MEMORIAL SCHOOL inayomilikiwa na Col Kipingu.

Mgogoro huo unasululishwa na Polisi Bagamayo na polis DSM na watendaji wa Serikali. Hii ni mara ya pili kwa Mwingira kuvamiwa ambapo kule Sumbuwanga anamiliki shamba zaidi ya ekar 500 alilouziwa Tshs 600m na wananchi wanapinga.
 
"Akupigae kofi shavu la kulia mgeuzie na kushoto" akunyanganyae koti mpe na shati! Mtu akikukosea msamehe 7 mara 70! Sasa mchungaji,Nabii,Mtume Mwingira kaamua kutumia jino kwa jino! Haya bana!

Mkuu nukuu yako ni nzuri, lakini usiitumie ku-justfy kinachoendelea mapinga. Naamini mazungumzo yatatoa ufumbuzi wa mgogoro kati ya mtumishi Josephat Mwingira na wakazi wa eneo la mgogoro. Siamini kama kuna jino kwa jino.
 
Huyo ni tapeli tu anakula hela za wajinga wanao mwamin na na kuabudu katika kanisa lake nina ndugu yangu mmoja kesha wahi fanya kazi mashamba yake ya sumbawanga unaambiwa ni katili huyo shetan huko hafai hata bure yaan huyo ni nabii wa kuzim kabisa wooote wanao amini katika kanisa lake wametekwa na ni mateka wa shetan ingawa wao hawajitambui na ukiwaambia wankuwa wakali, nabii mwenyewe mtume mwenyewe khee hii noumaaaaa
 
Wananch wa Bagamoyo eneo la Mapinga Wamevamia Shamba la Nabii na Mtume Josephati Mwingira. Juzi Mwingira alikwenda huko akiwa na walinzi wa Kimasai walioambatana Na Mabounce na kuendesha operation ya kuwaondoa kwa nguvu wananch hao na kuzua mapigano makali ambapo leo kuna kikao cha ulinzi na usalama kujadili suala hilo kinachofanyika shule ya Sekondari ya Lord baden MEMORIAL SCHOOL inayomilikiwa na Col Kipingu.

Mgogoro huo unasululishwa na Polis Bagamnyo na polis Dsm na watendaji wa Serikali.

Hii ni mara ya pili kwa Mwingira kuvamiwa ambapo kule Sumbuwanga anamiliki shamba zaidi ya ekar 500 alilouziwa Tshs 600m na wananch wanapinga.

Ni wakati muafaka sasa Serikali ikaingilia kati hawa wachungaji uchwara ambao kazi yao kubwa ni kupora sadaka kutoka kwa wananchi maskini na hasa wanawake.Kwa kuanzia wafuatao wanatakiwa serikali iwachukulie hataua hawa wezi haswa Mwingira, Lusekelo na Kakobe
 
huyu jamaa tatizo lake anajazba sana hasa pale anapokuwa anapata challenge kidogo tu...
 
Kwakusema ukweli nabii wa mungu hula alindwi na wamasai, nabii wa mungu anaulinzi mkubwa sana kutoka kwa mungu mwenyewe, napata wasiwasi kusikia Kuwait nabii wa mungo analindwa na wamasai na mabaunsa. Shame on you.
 
mitanzania mijinga kweli,.yani yeye anablingbling wao wamechokaaaaaaaaa..sadaka wanayompa si bora wangefanyia mambo mengine..ndio maana naparty kuliko kwenda kwenye makanisa ya wahuni kama hawa..
 
Wananch wa Bagamoyo eneo la Mapinga Wamevamia Shamba la Nabii na Mtume Josephati Mwingira. Juzi Mwingira alikwenda huko akiwa na walinzi wa Kimasai walioambatana Na Mabounce na kuendesha operation ya kuwaondoa kwa nguvu wananch hao na kuzua mapigano makali ambapo leo kuna kikao cha ulinzi na usalama kujadili suala hilo kinachofanyika shule ya Sekondari ya Lord baden MEMORIAL SCHOOL inayomilikiwa na col Kipingu.

Mgogoro huo unasululishwa na Polis Bagamnyo na polis Dsm na watendaji wa Serikali.Hii ni mara ya pili kwa Mwingira kuvamiwa ambapo kule Sumbuwanga anamiliki shamba zaidi ya ekar 500 alilouziwa Tshs 600m na wananch wanapinga.

Hivi mapinga kuna nini hawataki maendeleo? Kuna wakati wakazi wengi wa Dar es salaam walinunua mashamba kwa wenyeji huko mapinga.Walikuwa wamepania hasa kupaendeleza wengine walinunua hadi matrekta kwa ajili ya kuanzisha ufugaji na kilimo.

Walikuwa ni watu wengi kutoka Dar tena wengi middle class.Kilichotokea wananchi wa Dar na mapinga hawakuwa na tatizo ila serikali kupitia mkuu wa mkoa wakati huo christina Ishengoma wakaanza kuwakimbiza mashambani walionunua kuyaendeleza kwa kutumia FFU kulinda hilo pori eti wamevamia pori (siyo shamba lingekuwa shamba lingekuwa na mazao) la mfanyabiashara fulani.

Kilichouma watu ni kuona mapolisi wanashinda porini kulinda vichaka vya porini visivamiwe!!! wangekuwa wanalinda shamba la mtu lenye mazao sawa.Lakini kulinda mavichaka that is too much for police proffession.Kazi ya police ni kulinda properties za watu vichaka vya porini sio properties za watu ni mali ya mwenyeji Mungu mndio maana hata kwenye fidia ya mashamba huwa havitathiminiwi.

kama mtu anajenga shule analeta maendeleo watu wanamkimbiza ili kusudi eneo liendelee kuwa pori hii ni kitu gani? Lakini kama analiendeleza hamna shida.

Mtu akipewa pori na asipoliendeleza kwa kipindi takiwa awe nabii au mkazi wa mapinga au mwekezaji aondolewe tu hatuwezi kuwa kama wakenya ambao sheria yao ya ardhi ni ya kijinga unakuta mtu anamiliki heka hata maelfu za pori kazungushia seng`eng`e hazina kitu, haiendelezi na haifanyii chochote miaka nenda rudi na analindwa na serikali wakati wananchi wengi wa kenya hawana ardhi.

Nashauri Serikali ijitoe kulinda mapori.Mtu mwenye pori wacha wampore bila kujali ardhi hiyo aliinunua au ameirithi na amekuwa akiishi hapo kwenye pori kwa karne ngapi wacha wachukue waendelezaji.

kingadvisor@yahoo.com
 
Hivi huyo mwingira anamtafuta mungu au mali? Manake simwelewi mara anamiliki mashamba, bank, viwanja vikubwa anatembelea magari ya gharama sasa huyu ni mtumishi wa mungu au mtafutaji. Huyu jamaa anatia shaka.
Biblia inasema huwezi kutumikia mabwana wawili yaani pesa na mungu. Sasa mtume anamuhubiri mungu gani.
 
Hivi huyo mwingira anamtafuta mungu au mali? Manake simwelewi mara anamiliki mashamba, bank, viwanja vikubwa anatembelea magari ya gharama sasa huyu ni mtumishi wa mungu au mtafutaji. Huyu jamaa anatia shaka.
Biblia inasema huwezi kutumikia mabwana wawili yaani pesa na mungu. Sasa mtume anamuhubiri mungu gani.

Makanisa mengi ikiwemo Roman Catholic.hayategemei sadaka wanaamini asiyefanya kazi na asile hata kama ni kanisa au ni padre lazima ajishughulishe.Ndio maana Roman catholic wana miradi ya mashule,vyuo vya VETA na vikuu kama st augustine ,miradi ya mashamba,hostel,miradi ya kupangisha maduka kama ilivyo msimbazi Centre,Vituo vya Radio,Television,Magazeti,Bank ya Mkombozi kwa ajili ya kuweka sadaka zao na ada za mashule yao na pesa za waumini wao na kuzikopesha,kuziwekeza n.k Makanisa mengi yamegundua kuwa ukitolea macho sadaka pekee kanisa haliwezi kujitegemea na kuendelea kwa kasi litakuwa tegemezi kwa watoa sadaka waumini ambao kila siku wanapungua kwa kupenda dunia,kwa kuhama hovyo makanisani na wabahili wa kutupwa kutoa sadaka na hata wakitoa midomo juu padre hapumui mara kala hela zetu hela zenyewe hazijai kibaba.

Hivyo Usishangae Mwingira anachofanya kanisa ni sehemu ya jamii linapatikani kanisani na sokoni pia llinapatikana likiuza bidhaa zake ili lipate pesa za kujiendesha.Na ni kitu kizuri.Sababu wanaweza hudumia yatima,wenye shida n.k wakiwa na mapato mazuri kuliko waanzishe mfano kituo cha yatima kinachotegemea huruma ya maruhuni mtoa sadaka ambaye mpaka apende siku ya sikukuu ndio alete mlo mmoja akiwa kazungukwa na vyombo vya habari kibao kwa katukio ka kutoa mlo mmoja.

Kutafuta mali kwa ajili ya kuhudumia jamii kwa shule,bank,n.k sidhani ni kosa.Sidhani mbinguni watu wanaenda tu kwa kujisalia na kusalia wengine tu inataka watu wahudumie wengine pia kwa mahitaji na huwezi hudumia mwingine wakati ni lofa huna kitu.Yesu aliwahi kulalamika kuwa nilikuwa sina nguo hukunivika,nilikuwa sina kile hukunipa nenda motoni.Ina maana anaendelea kulalamika nilikuwa sina shule hukunijengea,nilikuwa sina hospitali hukujenga,sina benki hukunianzishia,sina sehemu ya kupangisha maduka hukunijengea nenda motoni.Makanisa yasiyofanya hayo yajiulize tena.Vigezo vya kwenda motoni viko vingi si tu kwa sababu wewe huibi huzini basi wewe wa mbinguni.Vimo vigezo pia hivyo vya huduma kwa jamii.

Lakini una haki ya kuamini chochote hata katiba ya nchi inakuruhusu.Imani ni kitu cha mtu binafsi sikupingi unachoamini natoa maoni yangu.
 
Back
Top Bottom