Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,769
- 10,645
Nimeshangazwa sana na kauli ya mh. Mbowe wakati akihojiwa BBC kufuatia "muafaka wa kitaifa" na ikulu. Mpaka sasa sijaelewa hasa uhalali wa huo mswada walioupinga vikali umepata wapi uhalali wake kisheria kiasi cha kutaka ufanyiwe tu marekebisho na serikali. Hoja ya msingi kabisa ilikuwa ni mchakato uliopelekea mswada kussomwa mara ya pili kwamba haukuwa halali. Sasa baada ya maongezi ya faragha ikulu ghafla mswada umepatiwa uhalali wake kiasi cha kutokuwa na haja ya kupelekwa kwa wananchi. Je CHADEMA walikuwa wakipigania maslahi ya nani haswa? Kwamba sasa wanasubiri "nia njema" ya serikali kuufanyia marekebisho wakiingiza mapendekezo yao pia!!!!!!!!!!! We still have a long way to go.