Huku mitaani wananchi wameduwazwa na udikiteta unaoendelezwa na uongozi wa juu ndani ya chama hicho.Wamekuwa wakijiuliza iweje kila jambo viongozi watake kulitolea uamuzi?.Wananchi hapa mtaani wamekasirishwa na kitendo cha katibu wa CHADEMA kuonyesha usaliti wa demokrasia kwani amekuwa akihubiri kuwa serikali inahujumu demokrasia hapa nchini kumbe na yeye ndani ya chama chake hakuna demokrasia kabisa.
Wananchi wamekuwa wakitolea mifano mambo kadhaa ambayo yamewahi kutokea ndani ya chama hicho na bado kikaendelea kuyafumbia macho huku suluhisho kikitoa vitisho vya kuwafukuza wanachama ambao wanaonekana kuhoji juu ya mwenendo ndani ya chama hicho.
1.Wamekuwa wakikumbusha juu ya Zitto Kabwe alivyozuiwa na kikundi cha ati wazee wa chama asigombee uenyekiti na baadaye kuzushiwa mambo mbalimbali ikiwemo ati Zitto amenunuliwa na CCM nadhani tunayakumbuka haya kwani Zitto amepita katika kipindi kigumu mno.
2.Pia, wananchi wamekuwa wakikumbushana juu ya lile tukio la Marehemu Chacha Wangwe alipohoji juu ya matumizi ya fedha za ruzuku ya chama kufaidisha watu wachache wa makao makuu huku ofisi za mawilayani na mikoa zikuwa katika hali mbaya kama sio taabani.Chacha Wangwe alizuliwa kashfa nyingi na kusema kwamba alikuwa amenunuliwa na CCM.Na alipotaka kutumia haki yake ya kidemokrasia kwa kutangaza kuwania uenyekiti ndani ya chama hicho mengi yalimkuta nadhani tunayakumbuka.
3.Wananchi pamoja na wapenzi wa CDM wamekuwa wakizungumzia uchaguzi wa ndani ya chama hicho.Wanahoji iweje baadhi ya wagombea ambao hutoka katika mikoa isio ya Kilimanjaro na Arusha huenguliwa katika uchaguzi huo?.Wanatoa mfano wa kuenguliwa kwa baadhi ya wagombea katika uchaguzi wa BAVICHA, wanasema udikiteta na upendeleo ndio ulitumika kuwaengua baadhi ya wagombea uenyekiti na kupitisha wale wasioweza kuhoji mwenendo wa mambo ndani ya chama hicho na si vinginevyo.Vijana wengi walidhani CDM ndio kimbilio lao kumbe wamebaini walipotea na sasa wameanza kusambaratika wengine juzijuzi tu wamejiunga na chama cha SAU na tumeona wamepewa ujumbe wa sekratirieti na wengine hivi karibuni tutawasikia NCCR-Mageuzi na CCM.
4.Jambo lingine ambalo nimekuwa nikilisikia kwa wananchi mara kwa mara suala la Mh Shibuda.Hii kweli inaonesha kuwa no intra-party demokrasi CHADEMA.Yaani mbunge hapaswi kuwa na mawazo yake tofauti ndani ya Bunge.Hapaswi kupingana na wenzake hata kama wanazungumza pumba.Wananchi wamekuwa wakihoji iweje CDM imekuwa ikiponda CCM kuwa wabunge wake ni ndio mzee wakati wa kwao hawawapi fursa ya kutoa mawazo yao au kueleza bila kubughudhiwa na chama kile wananchoamini ni sahihi?.Hapa wananchi wengi wanaona CDM si mbadala wa CCM hata kidogo na mbadala hajazaliwa labda CCM yenyewe ipasuke vipande na hapo mbadala ndio utakuwepo na upinzani wa kweli sio wa Ze- Comedy utaonekana.Wanahoji hivi mbunge kutofautiana kidogo na msimamo wa chama chake ni dhambi?.Je mbunge alienda bungeni kusimamia maslahi ya chama au ya kwao wananchi?.Mimi mfanyabiashara hapa Arusha sina jibu labda wanachadema hasa viongozi wa juu wajitokeze na kujibu haya.
5.Sasa jambo ambalo limetawala karibu magenge yote ya story hapa Arusha ni hili sakata la madiwani wa Arusha kukataa kupelekeshwa.Jambo hili limevuta hisia za watu wengi hapa na katika vyombo vya habari.Wananchi wamekasirishwa na kitendo cha viongozi wa CDM kuwatishatisha viongozi wao kwa kutaka kuwavua madaraka yao.Wananchi wengi sana hapa Arusha wanauliza hivi tulichagua viongozi hawa ikiwemo mbunge kutumikia chama au sisi wana Arusha?.Iweje chama kiwalazimishe madiwani wake kutanguliza maslahi ya chama badala ya maslahi yetu?.Sisi hatutaki vurugu kila kukicha ambazo zinapelekea kuuwawa kwa ndugu zetu.Wananchi wa Arusha wanataka amani ya kudumu sasa ili wajikite katika shughuli za maendeleo.Wananchi wengi wanaamini madiwani ambao wameshika vyeo hapa Arusha wakiongozwa na Naibu Meya Mh Estomih Mallah litakuwa suluhisho la mikwaruzo mingi ambayo imetokea hapa Arusha.Hivyo chama kuwalazimisha madiwani wavue vyeo walivyovipata kwa njia halali wakiongozwa na nia thabiti kabisa ya kujenga Arusha yetu ni kusaliti demokrasia na kuwasaliti wananchi waliowachagua kuungana na wale wa kutoka CCM ili kuleta maendeleo jijini.
Hivyo, wananchi wanasema imefika wakati sasa kwa viongozi wa chadema kujivua gamba angalau ziwepo nyuso mpya zitakazoleta matumaini mapya.Na nyuso hizo ziwe za vijana atakaopambana na Nape wa CCM ambaye anaonekana kuwatishio sasa na viongozi waliopo sasa CDM wamezeeka na nguvu za kutawala jukwaa zinaisha.Pia, wanashauri utaratibu wa viongozi kupenda kuingilia mambo ya chini kama maamuzi yanayofikiwa na madiwani wao ukome kwani utakifanya chama kiondoke kwa wananchi na kubaki chini kuwa kampuni ya watu kama kilivyokuwa huko nyuma.Wanashauri structure ya chama ibadilishwa na maamuzi yawe yanafuata approach ya bottom-up badala ya sasa ya juu-chini.Wanasema utaratibu huu unalenga kuwatafutia umaarufu viongozi wa juu ili kila kitu waonekaneonekane na hawakotayari kuona mtu mwingine ndani ya chama akiibuka na kuwa maarufu zaidi yao.Wanasema udikiteta unakiua CHADEMA taratiiibu sawa na ugonjwa wa kansa kwa binadamu.
Mie nimewasilisha kilio cha wananchi waliowengi wasioweza kufika hapa jamvini wadau!!!
5.Wananchama wa CDM na watanzania kwa
Wananchi wamekuwa wakitolea mifano mambo kadhaa ambayo yamewahi kutokea ndani ya chama hicho na bado kikaendelea kuyafumbia macho huku suluhisho kikitoa vitisho vya kuwafukuza wanachama ambao wanaonekana kuhoji juu ya mwenendo ndani ya chama hicho.
1.Wamekuwa wakikumbusha juu ya Zitto Kabwe alivyozuiwa na kikundi cha ati wazee wa chama asigombee uenyekiti na baadaye kuzushiwa mambo mbalimbali ikiwemo ati Zitto amenunuliwa na CCM nadhani tunayakumbuka haya kwani Zitto amepita katika kipindi kigumu mno.
2.Pia, wananchi wamekuwa wakikumbushana juu ya lile tukio la Marehemu Chacha Wangwe alipohoji juu ya matumizi ya fedha za ruzuku ya chama kufaidisha watu wachache wa makao makuu huku ofisi za mawilayani na mikoa zikuwa katika hali mbaya kama sio taabani.Chacha Wangwe alizuliwa kashfa nyingi na kusema kwamba alikuwa amenunuliwa na CCM.Na alipotaka kutumia haki yake ya kidemokrasia kwa kutangaza kuwania uenyekiti ndani ya chama hicho mengi yalimkuta nadhani tunayakumbuka.
3.Wananchi pamoja na wapenzi wa CDM wamekuwa wakizungumzia uchaguzi wa ndani ya chama hicho.Wanahoji iweje baadhi ya wagombea ambao hutoka katika mikoa isio ya Kilimanjaro na Arusha huenguliwa katika uchaguzi huo?.Wanatoa mfano wa kuenguliwa kwa baadhi ya wagombea katika uchaguzi wa BAVICHA, wanasema udikiteta na upendeleo ndio ulitumika kuwaengua baadhi ya wagombea uenyekiti na kupitisha wale wasioweza kuhoji mwenendo wa mambo ndani ya chama hicho na si vinginevyo.Vijana wengi walidhani CDM ndio kimbilio lao kumbe wamebaini walipotea na sasa wameanza kusambaratika wengine juzijuzi tu wamejiunga na chama cha SAU na tumeona wamepewa ujumbe wa sekratirieti na wengine hivi karibuni tutawasikia NCCR-Mageuzi na CCM.
4.Jambo lingine ambalo nimekuwa nikilisikia kwa wananchi mara kwa mara suala la Mh Shibuda.Hii kweli inaonesha kuwa no intra-party demokrasi CHADEMA.Yaani mbunge hapaswi kuwa na mawazo yake tofauti ndani ya Bunge.Hapaswi kupingana na wenzake hata kama wanazungumza pumba.Wananchi wamekuwa wakihoji iweje CDM imekuwa ikiponda CCM kuwa wabunge wake ni ndio mzee wakati wa kwao hawawapi fursa ya kutoa mawazo yao au kueleza bila kubughudhiwa na chama kile wananchoamini ni sahihi?.Hapa wananchi wengi wanaona CDM si mbadala wa CCM hata kidogo na mbadala hajazaliwa labda CCM yenyewe ipasuke vipande na hapo mbadala ndio utakuwepo na upinzani wa kweli sio wa Ze- Comedy utaonekana.Wanahoji hivi mbunge kutofautiana kidogo na msimamo wa chama chake ni dhambi?.Je mbunge alienda bungeni kusimamia maslahi ya chama au ya kwao wananchi?.Mimi mfanyabiashara hapa Arusha sina jibu labda wanachadema hasa viongozi wa juu wajitokeze na kujibu haya.
5.Sasa jambo ambalo limetawala karibu magenge yote ya story hapa Arusha ni hili sakata la madiwani wa Arusha kukataa kupelekeshwa.Jambo hili limevuta hisia za watu wengi hapa na katika vyombo vya habari.Wananchi wamekasirishwa na kitendo cha viongozi wa CDM kuwatishatisha viongozi wao kwa kutaka kuwavua madaraka yao.Wananchi wengi sana hapa Arusha wanauliza hivi tulichagua viongozi hawa ikiwemo mbunge kutumikia chama au sisi wana Arusha?.Iweje chama kiwalazimishe madiwani wake kutanguliza maslahi ya chama badala ya maslahi yetu?.Sisi hatutaki vurugu kila kukicha ambazo zinapelekea kuuwawa kwa ndugu zetu.Wananchi wa Arusha wanataka amani ya kudumu sasa ili wajikite katika shughuli za maendeleo.Wananchi wengi wanaamini madiwani ambao wameshika vyeo hapa Arusha wakiongozwa na Naibu Meya Mh Estomih Mallah litakuwa suluhisho la mikwaruzo mingi ambayo imetokea hapa Arusha.Hivyo chama kuwalazimisha madiwani wavue vyeo walivyovipata kwa njia halali wakiongozwa na nia thabiti kabisa ya kujenga Arusha yetu ni kusaliti demokrasia na kuwasaliti wananchi waliowachagua kuungana na wale wa kutoka CCM ili kuleta maendeleo jijini.
Hivyo, wananchi wanasema imefika wakati sasa kwa viongozi wa chadema kujivua gamba angalau ziwepo nyuso mpya zitakazoleta matumaini mapya.Na nyuso hizo ziwe za vijana atakaopambana na Nape wa CCM ambaye anaonekana kuwatishio sasa na viongozi waliopo sasa CDM wamezeeka na nguvu za kutawala jukwaa zinaisha.Pia, wanashauri utaratibu wa viongozi kupenda kuingilia mambo ya chini kama maamuzi yanayofikiwa na madiwani wao ukome kwani utakifanya chama kiondoke kwa wananchi na kubaki chini kuwa kampuni ya watu kama kilivyokuwa huko nyuma.Wanashauri structure ya chama ibadilishwa na maamuzi yawe yanafuata approach ya bottom-up badala ya sasa ya juu-chini.Wanasema utaratibu huu unalenga kuwatafutia umaarufu viongozi wa juu ili kila kitu waonekaneonekane na hawakotayari kuona mtu mwingine ndani ya chama akiibuka na kuwa maarufu zaidi yao.Wanasema udikiteta unakiua CHADEMA taratiiibu sawa na ugonjwa wa kansa kwa binadamu.
Mie nimewasilisha kilio cha wananchi waliowengi wasioweza kufika hapa jamvini wadau!!!
5.Wananchama wa CDM na watanzania kwa