BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,009
Date::10/4/2008
Wananchi wapongeza trafiki wala rushwa kuonyeshwa kwenye televisheni
Na Waandishi Wetu
Mwananchi
TAARIFA za kusimamishwa kazi kwa askari polisi wa kikosi cha usalama barabarani 11 katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro walionaswa katika mikanda ya video wakipokea rushwa imezua hofu kwa askari wa kikosi hicho nchi nzima.
Wakati Trafiki nchi nzima wakionekana kuingiwa na wasiwasi jinsi wenzao walivyonaswa na kamera hizo, wananchi mbalimbali wakiwamo wasafirishaji wa mizigo wamefurahia tukio hilo.
Watu mbalimbali waliopiga simu chumba cha habari cha Mwananchi Jumapili jana kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Arusha, Manyara,Tanga, Pwani, Morogorogo, Iringa na Mbeya walisema zoezi hilo lingefanyika nchi nzima.
''Wasingetoa kwanza hadi wakamilishe angalau mikoa 10, hata hivyo ni mwanzo mzuri na umeonyesha waandishi wanaweza wakiamua,'' alidai John Godson mkazi wa Dar es Salaam.
Wakazi sita wa Wilaya za Hai, Moshi Mjini, Mwanga, Same na Rombo waliopiga simu kwa nyakati tofauti walienda mbali na kusema wamepata ujasiri na kwamba watatumia simu zao za mikononi kuwapiga picha trafiki wala rushwa.
Tulilalamika miezi kadhaa iliyopita lakini tukashangaa RPC (Kamanda wa Polisi) badala ya kuchunguza akatoa kauli ya kisiasa kwamba, hakuna jambo kama hilo alilalamika mmiliki mmoja wa mabasi ya abiria Mkoa wa Kilimanjaro.
Mmiliki huyo wa mabasi yanayofanya safari zake kati ya Rombo-Moshi na Arusha alisema kama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ingekuwa makini haichukui dakika tano kuwanasa trafiki wa Kilimanjaro.
Leo wameonekana kama wamemwagiwa maji kile kiburi chao kimekwisha wanamuogopa kila mtu wanayemuona kwa kweli tunavishukuru vyombo vya habari hasa wapiga picha waliofanya kazi ile,alisema.
Wananchi wanaoishi Barabara Kuu za Tanga-Dar es Salaam, Dar es Salaam-Morogoro, Dar-Dodoma na Dar- Mbeya kupitia Iringa walitaka waandishi waliofanya kazi hiyo watunukiwe tuzo maalumu kwa uzalendo waliouonyesha.
Tumepita hapo Chalinze leo hatujasimamishwa wala ule utitiri wa trafiki kuanzia Kibaha hadi Mikumi haupo leo hii inaonyesha kuna jambo walilokuwa wanalifanya ndio maana wameogopa kiasi hicho,alidai dereva mmoja.
Kondakta wa mabasi ya kampuni moja maarufu inayofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Dodoma alisema kutoa Sh2,000 kwa trafiki ni jambo la kawaida iwe gari lina matatizo au halina.
Mhudumu huyo wa mabasi alitoa wito kwa Jeshi la Polisi kubadili mfumo wa namna ya kuwapata askari wa usalama barabarani kwa sababu wengi ni watoto wa wakubwa na baadhi yao walitoa rushwa kupata nafasi hizo.
''Lazima Jeshi la polisi litazame upya mfumo wa Idara zake ili polisi wa kikosi cha kuzuia Rushwa asimuonee gere yule wa Trafiki kwamba ana maslahi zaidi na dawa ni kuondoa tu rushwa na upendeleo wa ajira'' alisema.
Wananchi kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania walitoa changamoto kwa Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema na Kamanda wa trafiki, James Kombe kukifanyia mabadiliko makubwa kikosi hicho.
Wananchi wapongeza trafiki wala rushwa kuonyeshwa kwenye televisheni
Na Waandishi Wetu
Mwananchi
TAARIFA za kusimamishwa kazi kwa askari polisi wa kikosi cha usalama barabarani 11 katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro walionaswa katika mikanda ya video wakipokea rushwa imezua hofu kwa askari wa kikosi hicho nchi nzima.
Wakati Trafiki nchi nzima wakionekana kuingiwa na wasiwasi jinsi wenzao walivyonaswa na kamera hizo, wananchi mbalimbali wakiwamo wasafirishaji wa mizigo wamefurahia tukio hilo.
Watu mbalimbali waliopiga simu chumba cha habari cha Mwananchi Jumapili jana kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Arusha, Manyara,Tanga, Pwani, Morogorogo, Iringa na Mbeya walisema zoezi hilo lingefanyika nchi nzima.
''Wasingetoa kwanza hadi wakamilishe angalau mikoa 10, hata hivyo ni mwanzo mzuri na umeonyesha waandishi wanaweza wakiamua,'' alidai John Godson mkazi wa Dar es Salaam.
Wakazi sita wa Wilaya za Hai, Moshi Mjini, Mwanga, Same na Rombo waliopiga simu kwa nyakati tofauti walienda mbali na kusema wamepata ujasiri na kwamba watatumia simu zao za mikononi kuwapiga picha trafiki wala rushwa.
Tulilalamika miezi kadhaa iliyopita lakini tukashangaa RPC (Kamanda wa Polisi) badala ya kuchunguza akatoa kauli ya kisiasa kwamba, hakuna jambo kama hilo alilalamika mmiliki mmoja wa mabasi ya abiria Mkoa wa Kilimanjaro.
Mmiliki huyo wa mabasi yanayofanya safari zake kati ya Rombo-Moshi na Arusha alisema kama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ingekuwa makini haichukui dakika tano kuwanasa trafiki wa Kilimanjaro.
Leo wameonekana kama wamemwagiwa maji kile kiburi chao kimekwisha wanamuogopa kila mtu wanayemuona kwa kweli tunavishukuru vyombo vya habari hasa wapiga picha waliofanya kazi ile,alisema.
Wananchi wanaoishi Barabara Kuu za Tanga-Dar es Salaam, Dar es Salaam-Morogoro, Dar-Dodoma na Dar- Mbeya kupitia Iringa walitaka waandishi waliofanya kazi hiyo watunukiwe tuzo maalumu kwa uzalendo waliouonyesha.
Tumepita hapo Chalinze leo hatujasimamishwa wala ule utitiri wa trafiki kuanzia Kibaha hadi Mikumi haupo leo hii inaonyesha kuna jambo walilokuwa wanalifanya ndio maana wameogopa kiasi hicho,alidai dereva mmoja.
Kondakta wa mabasi ya kampuni moja maarufu inayofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Dodoma alisema kutoa Sh2,000 kwa trafiki ni jambo la kawaida iwe gari lina matatizo au halina.
Mhudumu huyo wa mabasi alitoa wito kwa Jeshi la Polisi kubadili mfumo wa namna ya kuwapata askari wa usalama barabarani kwa sababu wengi ni watoto wa wakubwa na baadhi yao walitoa rushwa kupata nafasi hizo.
''Lazima Jeshi la polisi litazame upya mfumo wa Idara zake ili polisi wa kikosi cha kuzuia Rushwa asimuonee gere yule wa Trafiki kwamba ana maslahi zaidi na dawa ni kuondoa tu rushwa na upendeleo wa ajira'' alisema.
Wananchi kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania walitoa changamoto kwa Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema na Kamanda wa trafiki, James Kombe kukifanyia mabadiliko makubwa kikosi hicho.