Wananchi wanapopiga vita wenye bidii kati yao ni janga kwa taifa

SuperNgekewa

Member
May 10, 2010
49
3
Katika sehemu nyingi za hii nchi yetu mtu akipata mafanikio anaitwa mchawi au ananyonya damu au amemtoa mhanga mtu wake ili apate mafanikio... In fact katika sehemu nyingi mchawi na mtu mwenye mafanikio ni synonymous. Katika tabia na tamaduni zinazokwamisha maendeleo na kudumisha umaskini, tabia hii iko mstari wa mbele kabisa. Ili kupata maendeleo jamii haina budi kuwashangilia na kuwapongeza wanaosonga mbele ili wawe mfano wa kuigwa na walio nyuma yao. Lakini sisi tuko tofauti: tunapiga vita wanaosonga mbele na kuwashangilia walio nyuma kama ndio mfano wa kuigwa! Jamani, kwa mtezamo huo si itabidi kubaki nyuma tu?

Ili taifa letu na wananchi wake twende mbele inabidi tubadili mtezamo wetu wa kuangalia nyuma na kushangilia nyuma na badala yake tuangalie mbele na kushangilia bidii na mafanikio. Kwa mfano hai angalia kiambatanisho hiki.

View attachment Waonywa kutowaua waleta maendeleo.docx
 
Ndiyo maana tunapendelea nchi kuongozwa na Mmasai au Mbarbaig, siyo kwa kuwa wanajua kuchunga ngombe na kupigana na simba bali kwa kuwa wako nyuma kimaendeleo kuliko Watz wengine! Yaani kwetu Tz walio nyuma ndio mfano wa kuigwa!
 
Back
Top Bottom