KING COBRA
JF-Expert Member
- Nov 10, 2011
- 2,782
- 864
[h=2]Tuesday, November 22, 2011[/h] [h=3] WANANCHI WAMKATAA DC WA JK, NI KUHUSU UJENZI WA NYUMBA ZA KISASA NA NHC MBEYA
[/h]
KATIKATI NI MKUU WA WILAYA YA MBEYA EVANCE BALAMA AKIWA NA MKURUGENZI WA WILAYA HIYO JULIANA MALANGE.
WANANCHI wa kijiji cha Ikumbi wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya leo walimweleza Mkuu wa wilaya hiyo Evance Balama na ujumbe wake uliokuwa umefika Kijijini hapo kuwa wanamtaka Rais Jakaya Kikwete kuzungumza nae na wala si yeye.
Hali hiyo ambayo ilishangaza vigogo wa Serikali waliokuwa wamefika katika eneo hilo ilianza na wananchi kukataa salamu za viongozi hao akiwemo mwakilishi wa Shirika la Nyumba la Taifa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Juliana Malange.
Mkutano huo ulifunguliwa na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Ackson Mwanjoka ambaye alisema kuwa mkutano huo ulikuwa na agenda moja ya kujengwa kwa mji wa kisasa katika Kijiji hicho kilichopo karibu na kiwanja kipya cha ndege cha Songwe mahala ambapo walihamishwa awali bila kulipwa vema stahiki zao.
Mwenyekiti huyo alipojaribu kumkaribisha Mkuu wa wilaya, wananchi walikataa kwa kunyosha vidole wakiashiria kuwa hawakuwa tayari kusikiliza agenda hiyo ambapo Mkuu wa wilaya aliinuka na kuwaambia kuwa waanze wao kusema.
Baada ya Mkuu wa wilaya kuwataka waseme hoja zao ndipo wananchi wakanyosha kidole na Mwenyekiti wa Kijiji hicho akampa nafasi mwananchi Meshack Job.
Mwananchi huyo alisema kuwa wananchi walikuwa wamebaini mbinu ya Serikali ya kuwahamisha hivyo kutokana na hali iyo na kwasababu awali hawakupewa fidia stahiki katika eneo ulipojengwa uwanja wa ndege hawakuwa tayari kuusikiliza ujumbe huo bali wanameitaji Rais Kikwete ili wazungumze nae.
Niweke wazi kuwa agenda iliyopo mezani ni kama zilizowahi kujitokeza hapo nyuma mwanzoni mwa mwaka huu na wananchi hatuhitaji kuwasikiliza na kuzungumza chochote na nyinyi ambaye tunamwitaji ni Rais Jakaya Kikwete na si mtu mwingine yeyote alisema Job huku akiondoka na wananchi wenzake wakishangilia kwa kusambaratika.
Kitendo hicho kiliwaacha midomo wazi huku wakitazamana kwa zaidi ya dakika tatu viongozi wa Serikali wakiongozwa na Mkuu huyo wa wilaya huku wakianza kumtupia lawama Mwenyekiti wa Kijiji hicho kuwa alikuwa anaufahamu mpango huo wa kuwadhalilisha viongozi wa Serikali.
Mkuu wa wilaya alipoulizwa mtazamo wake juu ya hali hiyo iliyokuwa imejitokeza alisema kuwa wananchi walipaswa kusikiliza kwasababu Serikali ina mpango mzuri wa kuwajengea makazi ya kisasa katika maeneo yao kupitia Shirika la Nyumba la Taifa NHC.
Mwenyekiti Wa Kijiji hicho Ackson Mwanjoka alisema kuwa shutuma zilizotolewa dhidi yake ya kuwadhalilisha vigogo hao kupitia wananchi alisema kuwa hakutendewa haki kwasababu hata taarifa za mkutano huo alipewa Novemba 18, mwaka huu hivyo hasingeweza kujua lolote ingawa alikiri kuwa wananchi wana hasira na Serikali katika masuala ya Ardhi katika eneo hilo.
Hali hiyo imejitokeza ikiwa ni siku chache wananchi wa Kijiji cha Mbalizi wilayani humo kumtaka Rais Jakaya Kikwete kumwondoa wilayani humo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Juliana Malange kwa madai kuwa analinda genge la waporaji wa miradi ya wananchi ukiwemo mradi wa maji wa Kijiji hicho.
Viongozi wa Shirika la nyumba la Taifa waliokuwa wameongozana na Mkuu huyo wa wilaya ili kutoa elimu juu ya uwekezaji huo wa nyumba za kisasa ni pamoja na Meneja wa Shirika hilo mkoa wa Mbeya Charles Kessy, Frola Luvanda, Gidion Mgaya na Raymond Mdolwa ambaye alimwakilisha Mkurugenzi wa Shirika hilo.
[/h]
KATIKATI NI MKUU WA WILAYA YA MBEYA EVANCE BALAMA AKIWA NA MKURUGENZI WA WILAYA HIYO JULIANA MALANGE.
WANANCHI wa kijiji cha Ikumbi wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya leo walimweleza Mkuu wa wilaya hiyo Evance Balama na ujumbe wake uliokuwa umefika Kijijini hapo kuwa wanamtaka Rais Jakaya Kikwete kuzungumza nae na wala si yeye.
Hali hiyo ambayo ilishangaza vigogo wa Serikali waliokuwa wamefika katika eneo hilo ilianza na wananchi kukataa salamu za viongozi hao akiwemo mwakilishi wa Shirika la Nyumba la Taifa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Juliana Malange.
Mkutano huo ulifunguliwa na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Ackson Mwanjoka ambaye alisema kuwa mkutano huo ulikuwa na agenda moja ya kujengwa kwa mji wa kisasa katika Kijiji hicho kilichopo karibu na kiwanja kipya cha ndege cha Songwe mahala ambapo walihamishwa awali bila kulipwa vema stahiki zao.
Mwenyekiti huyo alipojaribu kumkaribisha Mkuu wa wilaya, wananchi walikataa kwa kunyosha vidole wakiashiria kuwa hawakuwa tayari kusikiliza agenda hiyo ambapo Mkuu wa wilaya aliinuka na kuwaambia kuwa waanze wao kusema.
Baada ya Mkuu wa wilaya kuwataka waseme hoja zao ndipo wananchi wakanyosha kidole na Mwenyekiti wa Kijiji hicho akampa nafasi mwananchi Meshack Job.
Mwananchi huyo alisema kuwa wananchi walikuwa wamebaini mbinu ya Serikali ya kuwahamisha hivyo kutokana na hali iyo na kwasababu awali hawakupewa fidia stahiki katika eneo ulipojengwa uwanja wa ndege hawakuwa tayari kuusikiliza ujumbe huo bali wanameitaji Rais Kikwete ili wazungumze nae.
Niweke wazi kuwa agenda iliyopo mezani ni kama zilizowahi kujitokeza hapo nyuma mwanzoni mwa mwaka huu na wananchi hatuhitaji kuwasikiliza na kuzungumza chochote na nyinyi ambaye tunamwitaji ni Rais Jakaya Kikwete na si mtu mwingine yeyote alisema Job huku akiondoka na wananchi wenzake wakishangilia kwa kusambaratika.
Kitendo hicho kiliwaacha midomo wazi huku wakitazamana kwa zaidi ya dakika tatu viongozi wa Serikali wakiongozwa na Mkuu huyo wa wilaya huku wakianza kumtupia lawama Mwenyekiti wa Kijiji hicho kuwa alikuwa anaufahamu mpango huo wa kuwadhalilisha viongozi wa Serikali.
Mkuu wa wilaya alipoulizwa mtazamo wake juu ya hali hiyo iliyokuwa imejitokeza alisema kuwa wananchi walipaswa kusikiliza kwasababu Serikali ina mpango mzuri wa kuwajengea makazi ya kisasa katika maeneo yao kupitia Shirika la Nyumba la Taifa NHC.
Mwenyekiti Wa Kijiji hicho Ackson Mwanjoka alisema kuwa shutuma zilizotolewa dhidi yake ya kuwadhalilisha vigogo hao kupitia wananchi alisema kuwa hakutendewa haki kwasababu hata taarifa za mkutano huo alipewa Novemba 18, mwaka huu hivyo hasingeweza kujua lolote ingawa alikiri kuwa wananchi wana hasira na Serikali katika masuala ya Ardhi katika eneo hilo.
Hali hiyo imejitokeza ikiwa ni siku chache wananchi wa Kijiji cha Mbalizi wilayani humo kumtaka Rais Jakaya Kikwete kumwondoa wilayani humo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Juliana Malange kwa madai kuwa analinda genge la waporaji wa miradi ya wananchi ukiwemo mradi wa maji wa Kijiji hicho.
Viongozi wa Shirika la nyumba la Taifa waliokuwa wameongozana na Mkuu huyo wa wilaya ili kutoa elimu juu ya uwekezaji huo wa nyumba za kisasa ni pamoja na Meneja wa Shirika hilo mkoa wa Mbeya Charles Kessy, Frola Luvanda, Gidion Mgaya na Raymond Mdolwa ambaye alimwakilisha Mkurugenzi wa Shirika hilo.