sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,681
- 1,109
Sherehe za maazimisho ya kumbukumbu ya Mwalimu J K Nyerere na mapokezi ya uzimaji mwenge ni matukio makubwa yaliyojiri mwishoni mwa wiki hii mkoani Shinyanga kwenye manispaa ya Shinyanga mjini.Maazimisho haya yalipambwa na halaiki ya watoto wadogo ambao walipata mafundisho ya kutosha kiasi cha kuweza kukonga nyoyo za wakazi wa manispaa hii na viunga vyake.
Nikiwa mmoja wa mashuhuda waliohudhuria sherehe hizi nilitafakari mengi ambayo mwalimu Nyerere aliyowatendea Watanzania katika kipindi cha uongozi wake akiwa madarakani.Nilitafakari tulikotoka,tulipo na tuendako ikiwa ni pamoja na mmomonyoko wa maadili ya jamii hususani kati awamu hii ya nne.
Mmomonyoko huu wa maadili ninao uzungumzia ni mmomonoyko wa maadili ya viongozi wa umma katika kusimamia rasilimali za nchi yetu.Nilifananisha awamu zote baada ya mwalimu na awamu ya mwalimu,niligundua kuna hitaji spirit ya kweli katika kuutokomeza mfumo mbovu wa uongozi unao sababisha mmonyoko wa maadili wa viongozi wa umma.
Watanzania wamekosa uzalendo ,wanacho jali ni mkate wao wa siku.Wananchi wamekosa mvuto kwa viongozi wao hususani wa serikali kiasi cha kuwa na mvuto na matukio ambayo yanatumika kama burudani na kuifanya sehemu ya kupotezea muda.
Tukio la jana ambalo limenigusa kiasi cha kupelekea kuandika uzi huu ni ile ari ya wananchi kupungua kutokana na viongozi wao kutokuwa karibu nao na kuwakumbuka kipindi cha kampeni za uchaguzi tu.Kupungua kwa ari hiyo ndiko kulikopelekea umati uliofurika uwanjani hapo kuondoka ghafla mara baada ya halaiki ya watoto wetu kumaliza onyesho lao kabla hata ya hotuba ya rais, kiongozi wao waliye mchagua kwakura nyingi.
Niltafakari mengi na kujiuliza kama kweli kiongozi wao mpendwa waliye mchagua kwa kura nyingi ni kitu gani hasa kilichowakumba ghafla na kutotaka kumsikiliza ilihali alikuja na maneno ya kuwaeleza Watanzania.SI mila na desturi zetu Watanzania kuwakimbia wageni wetu wanapokuja kututembelea.Kitendo cha wananchi wengi kumkimbia mgeni wao wa kitaifa ambaye walimchagua na kumkubali kuwa kiongozi wao kinaashiria wnanchi kutokuwa na imani na viongozi wao.
Sherehe kama hizi enzi za mwalimu watu walizi sherehekea kwa bashasha na hamasa kubwa na kila mwananchi alikuwa na shauku ya kutaka kujua mwalimu leo ataongea nini.Wengine walitaka tu hata kumuona na kumpa mkono ilikuwa ni faraja kwao.Lakini siku ya kumkumbuka mwalimu viongozi wetu wana kimbiwa tena mbele ya mama wetu wa taifa mama Maria Nyerere.
Ni muda muafaka kwa viongozi tuliowapa dhamana kujiangalia na kubadilika tabia,wananchi wamechoshwa na madudu yenu kiasi mmeamua kujikita zaidi katika mambo yenu binafsi na kuacha kuitumia fursa mliyopewa na wananchi katika kudumisha na kuboresha ustawi wa maisha ya kila Mtanzania.Tukio la jana liwe fundisho kwa viongozi wengine ambao ndiyo wanao muangusha rais wetu.
Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki Afrika.
Nikiwa mmoja wa mashuhuda waliohudhuria sherehe hizi nilitafakari mengi ambayo mwalimu Nyerere aliyowatendea Watanzania katika kipindi cha uongozi wake akiwa madarakani.Nilitafakari tulikotoka,tulipo na tuendako ikiwa ni pamoja na mmomonyoko wa maadili ya jamii hususani kati awamu hii ya nne.
Mmomonyoko huu wa maadili ninao uzungumzia ni mmomonoyko wa maadili ya viongozi wa umma katika kusimamia rasilimali za nchi yetu.Nilifananisha awamu zote baada ya mwalimu na awamu ya mwalimu,niligundua kuna hitaji spirit ya kweli katika kuutokomeza mfumo mbovu wa uongozi unao sababisha mmonyoko wa maadili wa viongozi wa umma.
Watanzania wamekosa uzalendo ,wanacho jali ni mkate wao wa siku.Wananchi wamekosa mvuto kwa viongozi wao hususani wa serikali kiasi cha kuwa na mvuto na matukio ambayo yanatumika kama burudani na kuifanya sehemu ya kupotezea muda.
Tukio la jana ambalo limenigusa kiasi cha kupelekea kuandika uzi huu ni ile ari ya wananchi kupungua kutokana na viongozi wao kutokuwa karibu nao na kuwakumbuka kipindi cha kampeni za uchaguzi tu.Kupungua kwa ari hiyo ndiko kulikopelekea umati uliofurika uwanjani hapo kuondoka ghafla mara baada ya halaiki ya watoto wetu kumaliza onyesho lao kabla hata ya hotuba ya rais, kiongozi wao waliye mchagua kwakura nyingi.
Niltafakari mengi na kujiuliza kama kweli kiongozi wao mpendwa waliye mchagua kwa kura nyingi ni kitu gani hasa kilichowakumba ghafla na kutotaka kumsikiliza ilihali alikuja na maneno ya kuwaeleza Watanzania.SI mila na desturi zetu Watanzania kuwakimbia wageni wetu wanapokuja kututembelea.Kitendo cha wananchi wengi kumkimbia mgeni wao wa kitaifa ambaye walimchagua na kumkubali kuwa kiongozi wao kinaashiria wnanchi kutokuwa na imani na viongozi wao.
Sherehe kama hizi enzi za mwalimu watu walizi sherehekea kwa bashasha na hamasa kubwa na kila mwananchi alikuwa na shauku ya kutaka kujua mwalimu leo ataongea nini.Wengine walitaka tu hata kumuona na kumpa mkono ilikuwa ni faraja kwao.Lakini siku ya kumkumbuka mwalimu viongozi wetu wana kimbiwa tena mbele ya mama wetu wa taifa mama Maria Nyerere.
Ni muda muafaka kwa viongozi tuliowapa dhamana kujiangalia na kubadilika tabia,wananchi wamechoshwa na madudu yenu kiasi mmeamua kujikita zaidi katika mambo yenu binafsi na kuacha kuitumia fursa mliyopewa na wananchi katika kudumisha na kuboresha ustawi wa maisha ya kila Mtanzania.Tukio la jana liwe fundisho kwa viongozi wengine ambao ndiyo wanao muangusha rais wetu.
Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki Afrika.