Mchungaji wa Pentekoste mbaroni kwa tuhuma za kubaka wanafunzi
Na Shija Felician,Kahama
RAIA mmoja wa Rwanda anayedaiwa kuwa ni Mchungaji wa makanisa ya Pentekoste Tanzania, anashikiliwa na Polisi wilayani Kahama,kwa tuhuma za kuwabaka kwa zamu, wanafunzi watatu wa Shule ya Msingi Nyahanga.
Mchungaji huyo (Jina linahifadhiwa) anadaiwa kufanya vitendo hivyo kati ya Septemba mwaka jana na mwaka huu alipokamtwa.
Kwa mujibu wa habari za kipolisi, mchunganji huyo alikuwa akifanya ubakaji huo nyumbani kwake Nyahanga, karibu na shule wanayosoma watoto hao wa darasa la sita.
Inadaiwa kuwa wanafunzi hao walikuwa wanakwenda nyumbani kwa mchungaji huyo ambaye inasemekana alikuwa anawafungia chumbani kwake na kuwabaka kwa zamu.
Inadaiwa kuwa mtuhumiwa alikuwa akiwashawishi watoto hao kwa kuwapa kalamu, soksi za shule na fedha zisizozidi Sh 1,000, kama kifunga mdomo, baada ya kuwabaka.
Hata hivyo uongozi wa Kanisa la hilo wilayani Kahama, linalodaiwa kuwa ni mwajiri wa Basongela, lilimkana.
Badala yake, kanisa hilo limemtambua mtuhumiwa kuwa ni muumini na msharika wa kawaida na kwamba lilimpokea kutoka makanisa ya T.A.G na E.A.G.T ya wilayani hapa.
Habari za awali zilidai kuwa mtuhumiwa alikuwa amefukuza kutoka katika makanisa hayo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga,Shaibu Ibrahimu, alithibitisha habari kuhusu kushikiliwa kwa mchungaji huyo na kwamba polisi wanakamilisha taratibu za kumpima afya yake ili kuona usalama wa afya za watoto hao.
Na Shija Felician,Kahama
RAIA mmoja wa Rwanda anayedaiwa kuwa ni Mchungaji wa makanisa ya Pentekoste Tanzania, anashikiliwa na Polisi wilayani Kahama,kwa tuhuma za kuwabaka kwa zamu, wanafunzi watatu wa Shule ya Msingi Nyahanga.
Mchungaji huyo (Jina linahifadhiwa) anadaiwa kufanya vitendo hivyo kati ya Septemba mwaka jana na mwaka huu alipokamtwa.
Kwa mujibu wa habari za kipolisi, mchunganji huyo alikuwa akifanya ubakaji huo nyumbani kwake Nyahanga, karibu na shule wanayosoma watoto hao wa darasa la sita.
Inadaiwa kuwa wanafunzi hao walikuwa wanakwenda nyumbani kwa mchungaji huyo ambaye inasemekana alikuwa anawafungia chumbani kwake na kuwabaka kwa zamu.
Inadaiwa kuwa mtuhumiwa alikuwa akiwashawishi watoto hao kwa kuwapa kalamu, soksi za shule na fedha zisizozidi Sh 1,000, kama kifunga mdomo, baada ya kuwabaka.
Hata hivyo uongozi wa Kanisa la hilo wilayani Kahama, linalodaiwa kuwa ni mwajiri wa Basongela, lilimkana.
Badala yake, kanisa hilo limemtambua mtuhumiwa kuwa ni muumini na msharika wa kawaida na kwamba lilimpokea kutoka makanisa ya T.A.G na E.A.G.T ya wilayani hapa.
Habari za awali zilidai kuwa mtuhumiwa alikuwa amefukuza kutoka katika makanisa hayo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga,Shaibu Ibrahimu, alithibitisha habari kuhusu kushikiliwa kwa mchungaji huyo na kwamba polisi wanakamilisha taratibu za kumpima afya yake ili kuona usalama wa afya za watoto hao.