Wanajeshi watesa na kuua raia Monduli

FreedomTZ

JF-Expert Member
Jul 18, 2012
1,104
250
Wanajeshi kadhaa wa JWTZ kikosi cha mizingo wanaoishi katika mji wa Monduli wamewatesa vijana wawili waliowatuhumu kwa kuwaibia vifaa vya elektroniki. Mateso hayo ya kipigo kwa siku mbili mfululizo yamepelekea kijana mmoja kati ya walioteswa kwa kupigwa mbele ya maafisa wa jeshi la polisi na UWT kupoteza maisha. Ndugu wa kijana aliyeuwawa wamekataa kuuchukua mwili hospitalini kwa ajili ya maziko hadi uchunguzi unaoridhisha utakapofanyika na wauaji kufikishwa mahakamani. Inasemekana kuwa askari hao wa JWTZ walitoa taarifa ya kuibiwa mali zao kituo cha polisi Monduli. Baada ya kuona polisi hawachukui hatua kwa haraka kama walivyotarajia ndipo walipoamua kujichukulia sheria mkononi.

Hii ndiyo nchi ya amani na utulivu.
 
Wanajeshi kadhaa wa JWTZ kikosi cha mizingo wanaoishi katika mji wa Monduli wamewatesa vijana wawili waliowatuhumu kwa kuwaibia vifaa vya elektroniki. Mateso hayo ya kipigo kwa siku mbili mfululizo yamepelekea kijana mmoja kati ya walioteswa kwa kupigwa mbele ya maafisa wa jeshi la polisi na UWT kupoteza maisha. Ndugu wa kijana aliyeuwawa wamekataa kuuchukua mwili hospitalini kwa ajili ya maziko hadi uchunguzi unaoridhisha utakapofanyika na wauaji kufikishwa mahakamani. Inasemekana kuwa askari hao wa JWTZ walitoa taarifa ya kuibiwa mali zao kituo cha polisi Monduli. Baada ya kuona polisi hawachukui hatua kwa haraka kama walivyotarajia ndipo walipoamua kujichukulia sheria mkononi.

Hii ndiyo nchi ya amani na utulivu.

wasionyeshe ubabe kwa raia, waende Syria na Iraq, wakirudi tutawaita wanaume!
 
Yaani hayo ni mambo ya kizamani kweli! Wanataka walete ishu za enzi hizo kwamba ukimuona mwanajeshi basi ujue ana haki ya kukufanya lolote. Wanaua walipa kodi wanaowalipa mishahara bila ushahidi wa kutosha. Hiyo sio haki kabisa. Naamini ni wanajeshi wachache waliokosa nidhamu ndio wanataka waharibu sura ya jeshi letu.
 
Mi wala sishangai kabsaaaa,icho kitu n cha kawaida sana kwakua hata raia wanaua mwizi,wezi wangapi wameuwawa mitaani? Kwani wanajeshi ndo wanapenda wizi au ndo hawajachoshwa na uharifu? Aya mambo tumezoea hii itapunguza uharifu!
 
Back
Top Bottom