Wanajamii Prof. Muhongo si suluhisho wizara ya madini na madini pamoja na elimu yake!

sexologist

JF-Expert Member
Dec 5, 2010
2,283
976
Wakuu,
Nimefatilia kwa ukaribu mijadala na maoni ya wadau mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii kuhusu uteuzi wa wabunge wapya watatu akiwemo prof. Muhongo. Ambapo wengi wameshauri apewe wizara ya nishati na madini kutokana na utaalamu wake ktk madini kwenye masuala ya geology.

Mtazamo wangu, profesa muhongo kama tunamfikiria awe waziri wa nishati kutokana na weledi wake kiutaalam ktk sekta hyo si sahihi hata kidogo. Tukumbuke kuwa matatizo ya nchi yetu mengi hayapo kwenye ukosefu wa utaalamu, bali ni upungufu au kutokutekelezwa kwa sera husika. Hvyo ni sera ndizo zinatuletea matatizo yote haya, ikiwemo umaskini wetu. Kwa maneno mengine mtaalamu wa madini anatakiwa kuajiriwa kwenye sekta ya madini direct kama ni ukurugenzi au utendaji wa kawaida ili alete tija stahili.. Uwaziri anahitajika mtu mwenye uwezo wa kutekeleza au kutengeneza sera [as long as ni mbunge] kwa CV niliyoiona ya Muhongo nadhani anastahili ukatibu mkuu. Pia wadau tumekuwa tukiongozwa na prof. Mwakyusa, prof. Msolwa, na wengine wengi ktk wizara husika za taaluma zao lakini bdo hakukuwa na tija. Ni kwa sababu nilizozitaja.

Naomba kuwasilisha.
 
Naunga mkono,bado tunahitaji wazalendo wa kweli labda tujiulize ni kitu gani ametufanyia alipokua Stamico asije kuwa kama kina Nundu.
 
Naunga mkono,bado tunahitaji wazalendo wa kweli labda tujiulize ni kitu gani ametufanyia alipokua Stamico asije kuwa kama kina Nundu.
"As you learn more as you know small " hilo nalo neno u prof wa kitabu ni tofauti kubwa na ule wa utekelezaji na hakuna prof katika uadilifu. Tuwaombee tu kwa bwana God waondokane na mapepo ya kifisadi. Eee bwana God muumba wa viumbe vyote ingawa wengine wanamkiuka kwa kuwa na vitambi vya kero za wananchi tunakuomba utusamee na nchi yetu tuishi kwa amani. Amen
 
ningelikuwa na uwezo wa kumshauri huyu mtani wangu basi ningemshauri aachane na hizi 'siasa uchwala' kama alivyowahi kuziita mzee King Maker. Huyu ni mtu mwenye profile inayojitosheleza kuweza kuliachia taifa na vizazi kitu cha ku-share lakini kwa uteuzi huu anaweza akajikuta anapoteza.

Kwa jinsi mazingira ya siasa za tz zilivyo, Mh. Mbowe alisema hata akishuka malaika hawezi kufanya lolote. Na watu wa mpira waliwahi kusema kuwa 'hata akija Alex Furgerson' bila kubadilisha mfumo hatuwezi kupiga hatua yoyote ya maana.

Namshauri Prof. Muhongo aangalie Prof. mwenzake Anna Tibaijuka anasemaje akiwa waziri wa ardhi. Cha msingi kama ana nia ya kubadilisha mfumo basi afanye hivyo kwa kutokea nje lakini kwa kutokea ndani pamejaa wanafiki wengi, sio kazi rahisi
 
Nadahni Prof Muhongo atakuwa Waziri na Naibu wake atakuwa KAfumu, kama wizara itabaki kuwa Nishati na Madini, zikitengenishwa yaani kuwe na wizara ya Nishati na kisha ya Madini basi kuna uwezekano wa wote kuwa mAwaziri
 
nadhani serikali inashindwa kujua ni nani hasa nafaa kuwa kiongozi, lakini hili la kuchukua wataalamu wasio wanasiasa na kuja kuongoza ni makosa makubwa sana, tuna mifano mingi ya failure za hao wasomi waliobobea

Prof Sarungi
Prof Kapuya
Prof Mwandosya
Dr Mathayo
Dr Makongoro Mahanga

na wengineo
 
nakubaliana sera tunazo nzuri lakini utekelezaji hamna.Kama wataweza kutekeleza haya hakutakua na tatizo
 
Kweli kabisa, kwa mfumo huu hatutoki. Hebu cheki, waziri mkuu hana kauli kwa waziri,nae Waziri hana mamlaka kwa Naibu wake, nao wote watatu hawana mamlaka kwa Katibu mkuu. Hapo kwa nini wizara isiwe na madudu!
 
Kwa wale tunavyomfahamu Prof.Muhongo...huyu jamaa ni mtu wa serikali...Kubaki kwake Ud kuwa lecturer ilikuwa ni kituko kwani CACO alilazimisha head of department wa geology " Mama wa Kihindi" alimkataa na ud kufuta soo wakamruhusu alete mtu mwingine wa ziada ambaye alikuwa na first class kwenye darasa lao.Muhongo ana lower second. Alipokuwa head of department ilikuwa vituko kwa kwenda mbele, hakuna aliyempenda aendelee awe mwanafunzi au lecturer wenzie. Jamaa ana personality na confidence ya kufa mtu na mjivuni ile mabaya...Huyu anafaa kuwa Commissioner au Katibu wa wizara basi..
 
Wakuu,
Nimefatilia kwa ukaribu mijadala na maoni ya wadau mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii kuhusu uteuzi wa wabunge wapya watatu akiwemo prof. Muhongo. Ambapo wengi wameshauri apewe wizara ya nishati na madini kutokana na utaalamu wake ktk madini kwenye masuala ya geology.

Mtazamo wangu, profesa muhongo kama tunamfikiria awe waziri wa nishati kutokana na weledi wake kiutaalam ktk sekta hyo si sahihi hata kidogo. Tukumbuke kuwa matatizo ya nchi yetu mengi hayapo kwenye ukosefu wa utaalamu, bali ni upungufu au kutokutekelezwa kwa sera husika. Hvyo ni sera ndizo zinatuletea matatizo yote haya, ikiwemo umaskini wetu. Kwa maneno mengine mtaalamu wa madini anatakiwa kuajiriwa kwenye sekta ya madini direct kama ni ukurugenzi au utendaji wa kawaida ili alete tija stahili.. Uwaziri anahitajika mtu mwenye uwezo wa kutekeleza au kutengeneza sera [as long as ni mbunge] kwa CV niliyoiona ya Muhongo nadhani anastahili ukatibu mkuu. Pia wadau tumekuwa tukiongozwa na prof. Mwakyusa, prof. Msolwa, na wengine wengi ktk wizara husika za taaluma zao lakini bdo hakukuwa na tija. Ni kwa sababu nilizozitaja.

Naomba kuwasilisha.

Ninamtazamo tofauti na wewe juu ya wizara zinzoongozwa na maprof kutofanya vizuri. Ukiangalia vizuri na ukifikiria kwa makini utapata kusikia kuwa prof Mwakyusa for instance aliomba kutokuwepo kwenye baraza: reasons aliziweka wazi mbele ya kiranja wake, kumbuka kuwa katika serikali yetu ufanisi na ama kutokuiwa na ufanisi kuna sababu nyingi, pemgine uhodari na utaalam wa mtu hupuuzwa na kuzuiwa kutekeleza yanayostahili(angalia Magufuri na Hosea).
 
"As you learn more as you know small " hilo nalo neno u prof wa kitabu ni tofauti kubwa na ule wa utekelezaji na hakuna prof katika uadilifu. Tuwaombee tu kwa bwana God waondokane na mapepo ya kifisadi. Eee bwana God muumba wa viumbe vyote ingawa wengine wanamkiuka kwa kuwa na vitambi vya kero za wananchi tunakuomba utusamee na nchi yetu tuishi kwa amani. Amen

Ni kweli tupu mkuu.

Maprofesa waachwe vyuo vikuu waendelea kufundisha na kufanya tafiti mbalimbali zenye kuleta manufaa kwa umma. Waachwe vyuoni ili wazalishe watalaam zaidi.
 
Broken Ages nakubaliana na wewe. Hata hajaanza kazi na wala hajawahi kuwa Waziri lakini tayari wameanza kuponda na kusema hafai.

Hamuwachi jamani!
 
Kwa wale tunavyomfahamu Prof.Muhongo...huyu jamaa ni mtu wa serikali...Kubaki kwake Ud kuwa lecturer ilikuwa ni kituko kwani CACO alilazimisha head of department wa geology " Mama wa Kihindi" alimkataa na ud kufuta soo wakamruhusu alete mtu mwingine wa ziada ambaye alikuwa na first class kwenye darasa lao.Muhongo ana lower second. Alipokuwa head of department ilikuwa vituko kwa kwenda mbele, hakuna aliyempenda aendelee awe mwanafunzi au lecturer wenzie. Jamaa ana personality na confidence ya kufa mtu na mjivuni ile mabaya...Huyu anafaa kuwa Commissioner au Katibu wa wizara basi..

Watu wote waliyewahi kufundishwa, kufanya kazi, au hata kuwa karibu na huyu prof wanamkataa ktk suala zima la utendaji wa kazi licha ya kuwa na CV yenye 'madoido' kibao! Binafsi nawafaham angalau JF members 2 walio wahi kufanya nae kazi kwa ukaribu kabisa, watakuwa hawatutendei haki wasipo tupa wasifu wa kiukweli wa huyu prof
 
Nadhan ni mfumo tulio nao unachangia sana katika suala zima la udendaji katika wizara mbalimbali, kwa mfano Wazir hawez kumwajibisha mkurungezi wake ktk wizara husika ambaye ndio mtendaj mkuu ktk wizara. Hivyo bas hata Prof Muhongo Mfumo unaweza ukawa kikwazo kwake hata kama atakuwa committed and dedictated katika Wizara husika!!!!!!
 
Back
Top Bottom