Kwa waaminio biblia(ingawa sina uhakika kama hadithi hii iko pia ktk Q'uran Tukufu)tunakumbuka jinsi wana wa Israeli walivyoteseka utumwani Misri mpaka baadhi yao wakauzoea na kuamini ni sehemu ya maisha yao.Hata Musa alipoanza harakati za kuwakomboa,wapo waliombeza na kumwambia ni bora warudi kufia utumwani kuliko kufia jangwani!Lkn Musa hakusikiliza mtu,alisonga mbele pamoja na wale walioamini kuwa saa ya ukombozi ilikuwa imewadia!Habari za maandamano ya wanaharakati wa LRHC ni kama Musa kwetu Tanzania,wanaashiria saa ya ukombozi.Lkn wapo wanaobeza harakati hizi!Wanahisi serikali haina makosa,tuiache iendelee,ingawa tuna hali ngumu kila kona,baadhi hawaoni taabu!Lkn wanaharakati msife mioyo,mtatuona tukiungana nanyi punde,zibeni masikio msisikia maneno ya wanafiki ya kukatisha tamaa,tuikomboe nchi kwa ajili ya wote!Maji yao ya kuwasha,risasi zao,n.k vitaisha lkn cc tutabaki,na mwisho hata police na jeshi tutakuwa nao ktk ukombozi,tukishinda tutagongesheana glass pamoja!