Game Theory
Platinum Member
- Sep 5, 2006
- 8,545
- 835
Hakuna usawa hapa wa sheria katika mizania ya vyombo vitatu vya utawala katika taifa letu Tanzania
Kama wanaharakati wangekuwa ni chama cha siasa ningewaunga mkono wao kuliko huu utititiri wa NGO zilizojificha kama ni vyama vya siasa.
Kubadili chama/serikali iliyokomaa madarakani kwa miaka kibao hakuwezi kuletwa na helikopta au vijizawadi vya mashabiki waliojificha UK.
Mabadiliko yatawezekana tu kama viongozi wa vyama upinzani wataachana na tabia ya kupaa tu na ndege na kushuka ardhini ili kuwaunganisha wananchi kwa maandamano, migomo n.k. ili kupinga maonevu, ufisadi n.k. vinavyowakabili.
Hivi sasa inaelekea hakuna kiongozi mwenye ubavu na nia ya kuyafanya hayo na ndio maana tunabaki kupiga kelele tu kwenye hizi keyboards zetu.