Wanahabari tuisaidie nchi

KGARE

Senior Member
Jul 31, 2012
108
39
Ifikie wakati sasa tuombe vyombo vyetu vya habari kama ITV, STAR TV, TBC, CHANNEL 10, CLOUDS TV, SIBUKA, na Vyombo vingine kama radio na Magazeti..,KUANZISHA HOT INTERVIEWS kwa Viongozi Wetu wa Nchi. Ambapo mada Motomoto za maslahi ya Taifa mfano ardhi, ajira,utalii, viwanda, biashara, madini, mashirika/kampuni za kitanzania, maliasili, Utawala bora, n.k ziwe zinawekwa na wanamhoji Kiongozi huyo tena wakiwepo walau Wawakilishi wa Umma wenye ufahamu walau 2 hivi (mfano Wahadhiri, Wanaharakati, n.k).

Viongozi wawe wanajiandaa kuwaeleza Watanzania na baada ya Kipindi Kiongozi huyo aseme wazi maoni ambayo atayachukua kuyafanyia kazi na alete feedback baada ya Kipindi Fulani.
Mimi sifurahii na vipindi vya baadhi ya Televisheni vinamleta Kiongozi wa Nchi vinamuuliza maswali binafsi tu na ya kujifagilia au ya kichama tu badala ya kuzungumza mambo Mazito yanayorudisha nchi nyuma ili serikali ifanyie kazi.


HII NI NJIA MOJAWAPO KWA WANANCHI NA VIONGOZI KUWAJIBIKA KWA NCHI YAO!!
 
Wazo zuri.Lakini je, hao wanahabari wenyewe wapo? Au unamaanisha hawa hawa wanaoambiwa leteni maswali wanakusanya fasta hata kabla hawajasikia anachokiongea msemaji wanayetaka kumhoji? Hawa hawa walioitwa hotelini na "mmiliki wa dowans" akawaamrisha wasimpige picha wakatii amri hiyo haramu kutoka kwa mgeni? Nchi inamegwa na Malawi kule Ziwa Nyasa, wao wanafurahia juisi tu. Gazeti Mwanahalisi limefungiwa kwa muda usiojulikana bila kuelezwa ni habari ipi iliyokiuka maadili kwa mujibu wa sheria, lakini wamenyamaza kimya kama vile hakuna kilichotokea. Wanauza uhuru wao wa habari kwa bahasha ndogo za kaki. Kwa kifupi ndugu, wazo hili uliloleta haliwezi fanikiwa kwakuwa Tanzania hatuna wana habari. Tuna mfano wa wanahabari ambao si mbaya kama tukiwatafutia jina jingine.
 
Mi hakuna waziri hata mmoja nataka kumsikia sasa hivi. Kwanini tukae chini nakuskiza wezi wakiongea kwenye tv
 
sio sasa hivi kwa waandishi wanaojipendekeza, a.k.a buti likazi teh he he...
 
wanahabari wenyewe wooga kuna yule wa TBC sijui anaitwa nani hata hajijui!
 
wanahabari wenyewe wakina KIBONDE, HANDO, DIDA WA MCHOPS,SAKINA LIYOKA, CASTRO DICKSON, sijui FEIZA, KWISA! hahaha watazidi kutupoteza tu, mana watakuwa wanataka kuuza sura na kujipendekeza kwa hao wahusika! ninamashaka na waandishi wa habari za hapa nchini!
 
wanahabari wenyewe wakina KIBONDE, HANDO, DIDA WA MCHOPS,SAKINA LIYOKA, CASTRO DICKSON, sijui FEIZA, KWISA! hahaha watazidi kutupoteza tu, mana watakuwa wanataka kuuza sura na kujipendekeza kwa hao wahusika! ninamashaka na waandishi wa habari za hapa nchini!

mkuu tatizo kubwa ni ukuu wa wilaya!
 
mkuu tatizo kubwa ni ukuu wa wilaya!

sasa kajamaa kama kale ka kibonde kakipewa ukuu wa wilaya si wilaya itavunda kama akili zake zilivyovunda! Hando je? Ndo kabisaa box! Elimu muhimu mkuu!
 
Ifikie wakati sasa tuombe vyombo vyetu vya habari kama ITV, STAR TV, TBC, CHANNEL 10, CLOUDS TV, SIBUKA, na Vyombo vingine kama radio na Magazeti..,KUANZISHA HOT INTERVIEWS kwa Viongozi Wetu wa Nchi. Ambapo mada Motomoto za maslahi ya Taifa mfano ardhi, ajira,utalii, viwanda, biashara, madini, mashirika/kampuni za kitanzania, maliasili, Utawala bora, n.k ziwe zinawekwa na wanamhoji Kiongozi huyo tena wakiwepo walau Wawakilishi wa Umma wenye ufahamu walau 2 hivi (mfano Wahadhiri, Wanaharakati, n.k).

Viongozi wawe wanajiandaa kuwaeleza Watanzania na baada ya Kipindi Kiongozi huyo aseme wazi maoni ambayo atayachukua kuyafanyia kazi na alete feedback baada ya Kipindi Fulani.
Mimi sifurahii na vipindi vya baadhi ya Televisheni vinamleta Kiongozi wa Nchi vinamuuliza maswali binafsi tu na ya kujifagilia au ya kichama tu badala ya kuzungumza mambo Mazito yanayorudisha nchi nyuma ili serikali ifanyie kazi.


HII NI NJIA MOJAWAPO KWA WANANCHI NA VIONGOZI KUWAJIBIKA KWA NCHI YAO!!

Ni sahihi nami naunga mkono hoja tayari ITV,STAR TV ,CHANEL 10 wameanza tuwasapoti , lkn TBC na CLOUDS hizo ni ofisi za chama flani sio vyombo vya habari
 
Wazo zuri.Lakini je, hao wanahabari wenyewe wapo? Au unamaanisha hawa hawa wanaoambiwa leteni maswali wanakusanya fasta hata kabla hawajasikia anachokiongea msemaji wanayetaka kumhoji? Hawa hawa walioitwa hotelini na "mmiliki wa dowans" akawaamrisha wasimpige picha wakatii amri hiyo haramu kutoka kwa mgeni? Nchi inamegwa na Malawi kule Ziwa Nyasa, wao wanafurahia juisi tu. Gazeti Mwanahalisi limefungiwa kwa muda usiojulikana bila kuelezwa ni habari ipi iliyokiuka maadili kwa mujibu wa sheria, lakini wamenyamaza kimya kama vile hakuna kilichotokea. Wanauza uhuru wao wa habari kwa bahasha ndogo za kaki. Kwa kifupi ndugu, wazo hili uliloleta haliwezi fanikiwa kwakuwa Tanzania hatuna wana habari. Tuna mfano wa wanahabari ambao si mbaya kama tukiwatafutia jina jingine.

Umemjibu huyu bwana vizuri kabisa...hao wanahabari ni wepi...?
Wa kuambiwa kutuma maswali.., ni wale wa kudubiria labda neeema za u DC...
Hamna kitu hapo..
 
Wazo zuri.Lakini je, hao wanahabari wenyewe wapo? Au unamaanisha hawa hawa wanaoambiwa leteni maswali wanakusanya fasta hata kabla hawajasikia anachokiongea msemaji wanayetaka kumhoji? Hawa hawa walioitwa hotelini na "mmiliki wa dowans" akawaamrisha wasimpige picha wakatii amri hiyo haramu kutoka kwa mgeni? Nchi inamegwa na Malawi kule Ziwa Nyasa, wao wanafurahia juisi tu. Gazeti Mwanahalisi limefungiwa kwa muda usiojulikana bila kuelezwa ni habari ipi iliyokiuka maadili kwa mujibu wa sheria, lakini wamenyamaza kimya kama vile hakuna kilichotokea. Wanauza uhuru wao wa habari kwa bahasha ndogo za kaki. Kwa kifupi ndugu, wazo hili uliloleta haliwezi fanikiwa kwakuwa Tanzania hatuna wana habari. Tuna mfano wa wanahabari ambao si mbaya kama tukiwatafutia jina jingine.

Duh...Sasa kama kila njia ya kuliondoa Taifa letu kwenye janga la umasikini inakwama.Sasa si tutajuta kuzaliwa hapa!! I pray that the day comes when Tanzanians will feel proud of their Country and Leaders.
 
anaitwa zacharia...marine hassan ana ujasiri wa kuwatetea mafisadi

mkuu huyu jamaa ni hatari kuhoji tuu anakuwa kama anataka kulia hivi yaani hayupo happy na kazi yake, ni mwoga sijapata kuona, hata wanayoongea wengine yeye anaogopa!
 
Back
Top Bottom