KGARE
Senior Member
- Jul 31, 2012
- 108
- 39
Ifikie wakati sasa tuombe vyombo vyetu vya habari kama ITV, STAR TV, TBC, CHANNEL 10, CLOUDS TV, SIBUKA, na Vyombo vingine kama radio na Magazeti..,KUANZISHA HOT INTERVIEWS kwa Viongozi Wetu wa Nchi. Ambapo mada Motomoto za maslahi ya Taifa mfano ardhi, ajira,utalii, viwanda, biashara, madini, mashirika/kampuni za kitanzania, maliasili, Utawala bora, n.k ziwe zinawekwa na wanamhoji Kiongozi huyo tena wakiwepo walau Wawakilishi wa Umma wenye ufahamu walau 2 hivi (mfano Wahadhiri, Wanaharakati, n.k).
Viongozi wawe wanajiandaa kuwaeleza Watanzania na baada ya Kipindi Kiongozi huyo aseme wazi maoni ambayo atayachukua kuyafanyia kazi na alete feedback baada ya Kipindi Fulani.
Mimi sifurahii na vipindi vya baadhi ya Televisheni vinamleta Kiongozi wa Nchi vinamuuliza maswali binafsi tu na ya kujifagilia au ya kichama tu badala ya kuzungumza mambo Mazito yanayorudisha nchi nyuma ili serikali ifanyie kazi.
HII NI NJIA MOJAWAPO KWA WANANCHI NA VIONGOZI KUWAJIBIKA KWA NCHI YAO!!
Viongozi wawe wanajiandaa kuwaeleza Watanzania na baada ya Kipindi Kiongozi huyo aseme wazi maoni ambayo atayachukua kuyafanyia kazi na alete feedback baada ya Kipindi Fulani.
Mimi sifurahii na vipindi vya baadhi ya Televisheni vinamleta Kiongozi wa Nchi vinamuuliza maswali binafsi tu na ya kujifagilia au ya kichama tu badala ya kuzungumza mambo Mazito yanayorudisha nchi nyuma ili serikali ifanyie kazi.
HII NI NJIA MOJAWAPO KWA WANANCHI NA VIONGOZI KUWAJIBIKA KWA NCHI YAO!!