Wanafunzi zaidi Muhimbili University Kufukuzwa

2mbaku

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
316
67
Kuna tetesi kuwa wanafunzi zaidi katika chuo cha afya na sayansi shirikishi watafukuzwa na wengine kusimamishwa masomo mbali na wale 66 kutokana na kuhusika kwa namna moja au nyingine na mgomo uliotokea chuoni hapo tarehe 8 na 10. Swali ni miaka 4 ijayo tutazalisha madaktari wangapi kama wanafukuzwa namana hii? Pallangyo chonde chonde spidi yako punguza Profesa. Ikiwezekana maliza huo ugomvi na kuwarudisha wot haraka iwezekanavyo>
 
Tatizo wanafunzi hawa nao hawana msimamo na elimu yao haiwasaidii kuwa na utambuzi mwisho wa siku wanajiendea tu kama nao ni watu wasio na elimu ya kutosha,maana taarifa niliyonayo ya muda mrefu hapo Mhimbili hakuna serikali ya wanafunzi ilishavunjwa na wamepigwa mkwala wakanywea,sasa leo hii kwa kuwa mmekuwa waoga wa kudai haki zenu kwa muda mrefu na mmekuwa na tabia ya kujitenga haya leo ndo yanayowakuta.cha msingi muungane na mdai haki zenu kwa nguvu zote na kwa taratibu zote na kama wakiendlea kuiminya basi mgomo ni moja ya njia mbadala.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom