Wanafunzi wanaswa wakifanyiana mitihani IFM

Che Kalizozele

JF-Expert Member
Jul 20, 2008
777
49
na Sauli Giliard


WATU watatu, akiwamo mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Azania, jijini Dar es Salaam wamekamatwa wakiwafanyia mitihani wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaosoma ngazi ya stashahada ya juu pamoja na shahada.

Mwanafunzi huyo, Frank Kaduma, aliyekuwa anamfanyia mtihani mwanafunzi aliyemtaja kwa jina moja la Tina, alikuwa ameahidiwa na mtu aliyemuunganisha na mtahiniwa huyo kuwa baada ya kutoka kwenye mtihani huo angelipwa sh 150,000.

Tanzania Daima ilimshuhudia mtuhumiwa huyo akihojiwa na Michael Andekisye, ambaye ni Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo.

Msajili huyo alisema kuwa kitambulisho alichokuwa akikitumia kumfanyia Tina mtihani kilikuwa na jina la Christian Mbago, mwanafunzi wa mwaka wa tatu.

Kaduma alifafanua mbele ya ofisi hiyo kuwa aliitwa na rafiki yake ambaye hata hivyo hakutaka kumtaja jina, na baadaye alimuunganisha na mtahiniwa na kukubaliana kiasi hicho cha fedha baada ya kazi hiyo kumalizika.

“Mimi ninasoma Azania, nachukua PCM (Fizikia, Kemia na Hisabati), rafiki yangu anasoma masomo ya biashara na mtihani wa leo una hisabati, hivyo juzi nilikuja naye ili anionyeshe darasa na leo ndiyo nimekuja kumfanyia mtihani,” alisema Kaduma.

Wakati mwanafunzi huyo akihojiwa, mwanafunzi mwingine, John Kapinga, alikamatwa na kupelekwa katika ofisi ya msajili baada ya kukutwa akimfanyia mtihani mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuoni hapo, Joel Mlengule, anayesoma Stashahada ya Juu ya Hifadhi ya Jamii (Advanced Diploma in Social Protection).

Kapinga, alikiri kuwa alihitimu kidato cha sita mwaka 2003, akisoma masomo ya PCM, pamoja na kuahidi kwamba angetoa ushirikiano ili kumkamata mtahiniwa halisi.

“Sikutaka kufanya, ila nilishawishiwa mara nne sikutaka, hata ikafikia hatua ndugu yake kunishawishi, nikakubali, ila dhamiri ikinisuta. kwani hakuna malipo yoyote tuliyoahidiana na ndugu yangu huyo,” alisema Kapinga huku akijiinamia.

Tanzania Daima ilishuhudia kitambulisho chake kikiwa na jina la Joel Mlengule, kikiwa na namba ya usajili ADSP/16492/2007 na kinamalizika muda wake mwaka huu.

Kwa upande wake, Joel Mlengule, aliyefanyiwa mtihani na kukamatwa akiwa nje ya eneo la IFM akimsubiri Kapinga, alinaswa na walinzi wa chuo na kuhojiwa, ambapo alikiri kufanyiwa mtihani na Kapinga.

Mlengule ambaye ni mkazi wa Upanga, jijini Dar es Salaam, alikiri kuwapo mtu aliyemuunganisha na Kapinga, baada ya kufeli somo lake la hesabu mara mbili mfululizo, hivyo hakutaka hali hiyo imrudie, hasa ikizingatiwa kuwa huo ulikuwa mtihani wa mwisho chuoni hapo.

“Ni kweli alikuwa ananifanyia mtihani baada ya kufeli somo hili mara mbili. Niliona mwaka huu, na huu ni mtihani wangu wa mwisho, mimi sijui hesabu, ndiyo maana hata aliponiambia anifundishe nilikataa na kumwomba anisaidie kunifanyia,” alisema Mlengule.

Kwa mujibu wa Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo, tukio jingine la namna hiyo lilitokea jana, ambapo msichana mmoja alikimbia na kuacha viatu vyake, baada ya kubainika kuwa alikuwa akimfanyia mtihani mwanafunzi ambaye jina lake halikupatikana mara moja.

Aliongeza kuwa, mwaka jana matukio hayo yalitokea na imebainika kuwa kuna wakala anayewaunganisha wanafunzi wa chuo na watu wa nje kuwafanyia mitihani hiyo kinyume cha taratibu.

Akizungumzia udhibiti wa wanafunzi hao, Andekisye alisema chuo hicho kiko katika mchakato wa kubadili vitambulisho kwa wanafunzi na kuongeza nguvu katika usimamizi.

Alisema wanafunzi waliobainika kufanyiwa mitihani watafikishwa kwenye bodi ya chuo na waliowafanyia watapelekwa polisi, kwani tukio hilo ni la kughushi.

Sina hakika kama tutafika kwa mwendo huu.
 
WATU watatu, akiwamo mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Azania, jijini Dar es Salaam wamekamatwa wakiwafanyia mitihani wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaosoma ngazi ya stashahada ya juu pamoja na shahada.
Hii ni aibu kubwa kwa wanafunzi wetu wa vyuo vyikuu,hata siamini mwanafunzi wa kidato cha sitta kumfanyia mtihani mwanachuo wa stashahada ya juu na shahada,hii ni kweli wandugu?
 
WATU watatu, akiwamo mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Azania, jijini Dar es Salaam wamekamatwa wakiwafanyia mitihani wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaosoma ngazi ya stashahada ya juu pamoja na shahada.
Hii ni aibu kubwa kwa wanafunzi wetu wa vyuo vyikuu,hata siamini mwanafunzi wa kidato cha sitta kumfanyia mtihani mwanachuo wa stashahada ya juu na shahada,hii ni kweli wandugu?

unabisha nini sasa?, mtihani wa hesabu wa adv diploma wa mtu anayesoma biashara unadhani utamshinda mtu anayesoma PCM???, simple calculus, algebra etc!!. simple, very possible.
 
Hahahaha dah hesabu ni ugonjwa kweli wa taifa....

aah sana mkuu!,
tatizo msingi mzuri kwa wanafunzi hasa wa shule za msingi haujengwi, hivyo watoto wanakua na akili ya jumla kwamba hesabu ni somo gumu!, but amini usiamini mathematics is one of the easiest subjects, just playing around with logics!!.
ukiweza hesabu then hakuna somo lolote la sayansi litakuzingua.
 
Last edited:
aah sana mkuu!,
tatizo msingi mzuri kwa wanafunzi hasa ya msingi haujengwi, hivyo watoto wanakua na akili ya jumla kwamba hesabu ni somo gumu!, but amini usiamini mathematics is one of the easiest subjects, just playing around with logics!!.
ukiweza hesabu then hakuna somo lolote la sayansi litakuzingua.

Utajengwa vp wkt hao walimu wanao wafundisha mnawalipa mishahara kiduchu 150000/= kwa mwezi wkt nyie vibopa hiyo ni pesa ya vocha kwa siku wao wanapiga miayo tu. Acheni iendelee kufeli mpaka muwakumbuke walimu kwanza ndo wanao watoa matongo tongo lakini mnawasahau kana kwamba wao hawastahili kula vizuri, kulala pazuri, kunywa vinono vinono, kuendesha escudo n.k
 
mkuu
tatizo sio mshahara mdogo kwa walimu!, bali uwezo wa walimu wenyewe sio mzuri sana.
hebu nambie mwalimu wa vodafasta anifundishie mwanangu kweli hesabu ataelewa??.
ujue waliosemaga ualimu ni wito ndio kile kipindi amabcho tulikua na walimu wa uhakika mtu unapigwa shule kweli unasema hesabu zimeingia kichwani sawa sawia, siku hizi twisheni nyingi uswazi na watoto hawaelewi wala hawana misingi mizuri ya hesabu.
 
Tatizo lingine ni uongo tunaoimbiwa tukiwa bado wadogo.Ukiingia shule utasikia kila mtu anasema hesabu ngumu! hesabu ngumu! sasa unaweka hilo akilini na unaamini hesabu ngumu bila hata kuzijaribu kama ngumu kweli ,unafeli kabla hujaanza kuzifanya.Kumbe mawazo yangebadilika na kuamini inawezekana hakuna ambaye angefeli hesabu sababu ukweli ni kuwa hesabu ni rahisi sana tu.
 
Tatizo ni rushwa wakati wa kufanya admission ya wanafunzi wa IFM, so baadhi yao hawakuwa na sifa hata za kuwawezesha kujiunga, sasa ndo unakuta mitihani hata ya hesabu rahisi tu inawasumbua.
 
Tatizo lingine ni uongo tunaoimbiwa tukiwa bado wadogo.Ukiingia shule utasikia kila mtu anasema hesabu ngumu! hesabu ngumu! sasa unaweka hilo akilini na unaamini hesabu ngumu bila hata kuzijaribu kama ngumu kweli ,unafeli kabla hujaanza kuzifanya.Kumbe mawazo yangebadilika na kuamini inawezekana hakuna ambaye angefeli hesabu sababu ukweli ni kuwa hesabu ni rahisi sana tu.

uko sawa kabisa,
kula gwala!!.
icon10.gif
 
Wasichana wa ifm kazi yao kubwa ni kuchuna mabuzi
no wonder inaiitwa institute of female management.
 
Wanafunzi wengine wa IFM ni "viwango duni", sasa hii ni aibu kubwa sana. Vile vile nasikia IFM inaongoza kwa wanachuo kununua mitihani. AIBU
 
Duuh huu sasa kweli upumbavu,kuanzia Frank Kaduma pamoja na washiriki wake,vimini vitawaponza watoto,mabinti wengi wa IFM wanachanganya watoto,baba zao n.k.

Mtu mwenye akili zako huwezi kukubali kumfanyia mtu ona sasa mnavyodhalilika.Frank kimemponza kimini,IFM wanatega saaaaaaaaaana,shauri zenu.
 
na Sauli Giliard


WATU watatu, akiwamo mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Azania, jijini Dar es Salaam wamekamatwa wakiwafanyia mitihani wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaosoma ngazi ya stashahada ya juu pamoja na shahada.

Mwanafunzi huyo, Frank Kaduma, aliyekuwa anamfanyia mtihani mwanafunzi aliyemtaja kwa jina moja la Tina, alikuwa ameahidiwa na mtu aliyemuunganisha na mtahiniwa huyo kuwa baada ya kutoka kwenye mtihani huo angelipwa sh 150,000.

Tanzania Daima ilimshuhudia mtuhumiwa huyo akihojiwa na Michael Andekisye, ambaye ni Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo.

Msajili huyo alisema kuwa kitambulisho alichokuwa akikitumia kumfanyia Tina mtihani kilikuwa na jina la Christian Mbago, mwanafunzi wa mwaka wa tatu.

Kaduma alifafanua mbele ya ofisi hiyo kuwa aliitwa na rafiki yake ambaye hata hivyo hakutaka kumtaja jina, na baadaye alimuunganisha na mtahiniwa na kukubaliana kiasi hicho cha fedha baada ya kazi hiyo kumalizika.

“Mimi ninasoma Azania, nachukua PCM (Fizikia, Kemia na Hisabati), rafiki yangu anasoma masomo ya biashara na mtihani wa leo una hisabati, hivyo juzi nilikuja naye ili anionyeshe darasa na leo ndiyo nimekuja kumfanyia mtihani,” alisema Kaduma.

Wakati mwanafunzi huyo akihojiwa, mwanafunzi mwingine, John Kapinga, alikamatwa na kupelekwa katika ofisi ya msajili baada ya kukutwa akimfanyia mtihani mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuoni hapo, Joel Mlengule, anayesoma Stashahada ya Juu ya Hifadhi ya Jamii (Advanced Diploma in Social Protection).

Kapinga, alikiri kuwa alihitimu kidato cha sita mwaka 2003, akisoma masomo ya PCM, pamoja na kuahidi kwamba angetoa ushirikiano ili kumkamata mtahiniwa halisi.

“Sikutaka kufanya, ila nilishawishiwa mara nne sikutaka, hata ikafikia hatua ndugu yake kunishawishi, nikakubali, ila dhamiri ikinisuta. kwani hakuna malipo yoyote tuliyoahidiana na ndugu yangu huyo,” alisema Kapinga huku akijiinamia.

Tanzania Daima ilishuhudia kitambulisho chake kikiwa na jina la Joel Mlengule, kikiwa na namba ya usajili ADSP/16492/2007 na kinamalizika muda wake mwaka huu.

Kwa upande wake, Joel Mlengule, aliyefanyiwa mtihani na kukamatwa akiwa nje ya eneo la IFM akimsubiri Kapinga, alinaswa na walinzi wa chuo na kuhojiwa, ambapo alikiri kufanyiwa mtihani na Kapinga.

Mlengule ambaye ni mkazi wa Upanga, jijini Dar es Salaam, alikiri kuwapo mtu aliyemuunganisha na Kapinga, baada ya kufeli somo lake la hesabu mara mbili mfululizo, hivyo hakutaka hali hiyo imrudie, hasa ikizingatiwa kuwa huo ulikuwa mtihani wa mwisho chuoni hapo.

“Ni kweli alikuwa ananifanyia mtihani baada ya kufeli somo hili mara mbili. Niliona mwaka huu, na huu ni mtihani wangu wa mwisho, mimi sijui hesabu, ndiyo maana hata aliponiambia anifundishe nilikataa na kumwomba anisaidie kunifanyia,” alisema Mlengule.

Kwa mujibu wa Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo, tukio jingine la namna hiyo lilitokea jana, ambapo msichana mmoja alikimbia na kuacha viatu vyake, baada ya kubainika kuwa alikuwa akimfanyia mtihani mwanafunzi ambaye jina lake halikupatikana mara moja.

Aliongeza kuwa, mwaka jana matukio hayo yalitokea na imebainika kuwa kuna wakala anayewaunganisha wanafunzi wa chuo na watu wa nje kuwafanyia mitihani hiyo kinyume cha taratibu.

Akizungumzia udhibiti wa wanafunzi hao, Andekisye alisema chuo hicho kiko katika mchakato wa kubadili vitambulisho kwa wanafunzi na kuongeza nguvu katika usimamizi.

Alisema wanafunzi waliobainika kufanyiwa mitihani watafikishwa kwenye bodi ya chuo na waliowafanyia watapelekwa polisi, kwani tukio hilo ni la kughushi.

Sina hakika kama tutafika kwa mwendo huu.

Noma tupu , Majirani zetu kenya, uganda rwanda ,zaire malawi n.k sijui kama watatupa kazi aibu tupu....
 
Hahahaha dah hesabu ni ugonjwa kweli wa taifa....
Hesabu sio ugonjwa wa Taifa tu bali ni wa dunia, kila nchi inalalamikia wanafunzi wake kukimbia masomo yanayokuwa na hisabati, nilikuwa Zambia, Malawi, BOtsw na hata SA kilio ni hichohicho tu
 
Duuh huu sasa kweli upumbavu,kuanzia Frank Kaduma pamoja na washiriki wake,vimini vitawaponza watoto,mabinti wengi wa IFM wanachanganya watoto,baba zao n.k.

Mtu mwenye akili zako huwezi kukubali kumfanyia mtu ona sasa mnavyodhalilika.Frank kimemponza kimini,IFM wanatega saaaaaaaaaana,shauri zenu.
Hawa wanafunzi wa IFM hawakutoka kwenye sayari tofauti na wengine. Kugeneralise hao na kuwaexclude wengine si sahihi
 
Back
Top Bottom