Che Kalizozele
JF-Expert Member
- Jul 20, 2008
- 777
- 49
na Sauli Giliard
WATU watatu, akiwamo mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Azania, jijini Dar es Salaam wamekamatwa wakiwafanyia mitihani wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaosoma ngazi ya stashahada ya juu pamoja na shahada.
Mwanafunzi huyo, Frank Kaduma, aliyekuwa anamfanyia mtihani mwanafunzi aliyemtaja kwa jina moja la Tina, alikuwa ameahidiwa na mtu aliyemuunganisha na mtahiniwa huyo kuwa baada ya kutoka kwenye mtihani huo angelipwa sh 150,000.
Tanzania Daima ilimshuhudia mtuhumiwa huyo akihojiwa na Michael Andekisye, ambaye ni Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo.
Msajili huyo alisema kuwa kitambulisho alichokuwa akikitumia kumfanyia Tina mtihani kilikuwa na jina la Christian Mbago, mwanafunzi wa mwaka wa tatu.
Kaduma alifafanua mbele ya ofisi hiyo kuwa aliitwa na rafiki yake ambaye hata hivyo hakutaka kumtaja jina, na baadaye alimuunganisha na mtahiniwa na kukubaliana kiasi hicho cha fedha baada ya kazi hiyo kumalizika.
Mimi ninasoma Azania, nachukua PCM (Fizikia, Kemia na Hisabati), rafiki yangu anasoma masomo ya biashara na mtihani wa leo una hisabati, hivyo juzi nilikuja naye ili anionyeshe darasa na leo ndiyo nimekuja kumfanyia mtihani, alisema Kaduma.
Wakati mwanafunzi huyo akihojiwa, mwanafunzi mwingine, John Kapinga, alikamatwa na kupelekwa katika ofisi ya msajili baada ya kukutwa akimfanyia mtihani mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuoni hapo, Joel Mlengule, anayesoma Stashahada ya Juu ya Hifadhi ya Jamii (Advanced Diploma in Social Protection).
Kapinga, alikiri kuwa alihitimu kidato cha sita mwaka 2003, akisoma masomo ya PCM, pamoja na kuahidi kwamba angetoa ushirikiano ili kumkamata mtahiniwa halisi.
Sikutaka kufanya, ila nilishawishiwa mara nne sikutaka, hata ikafikia hatua ndugu yake kunishawishi, nikakubali, ila dhamiri ikinisuta. kwani hakuna malipo yoyote tuliyoahidiana na ndugu yangu huyo, alisema Kapinga huku akijiinamia.
Tanzania Daima ilishuhudia kitambulisho chake kikiwa na jina la Joel Mlengule, kikiwa na namba ya usajili ADSP/16492/2007 na kinamalizika muda wake mwaka huu.
Kwa upande wake, Joel Mlengule, aliyefanyiwa mtihani na kukamatwa akiwa nje ya eneo la IFM akimsubiri Kapinga, alinaswa na walinzi wa chuo na kuhojiwa, ambapo alikiri kufanyiwa mtihani na Kapinga.
Mlengule ambaye ni mkazi wa Upanga, jijini Dar es Salaam, alikiri kuwapo mtu aliyemuunganisha na Kapinga, baada ya kufeli somo lake la hesabu mara mbili mfululizo, hivyo hakutaka hali hiyo imrudie, hasa ikizingatiwa kuwa huo ulikuwa mtihani wa mwisho chuoni hapo.
Ni kweli alikuwa ananifanyia mtihani baada ya kufeli somo hili mara mbili. Niliona mwaka huu, na huu ni mtihani wangu wa mwisho, mimi sijui hesabu, ndiyo maana hata aliponiambia anifundishe nilikataa na kumwomba anisaidie kunifanyia, alisema Mlengule.
Kwa mujibu wa Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo, tukio jingine la namna hiyo lilitokea jana, ambapo msichana mmoja alikimbia na kuacha viatu vyake, baada ya kubainika kuwa alikuwa akimfanyia mtihani mwanafunzi ambaye jina lake halikupatikana mara moja.
Aliongeza kuwa, mwaka jana matukio hayo yalitokea na imebainika kuwa kuna wakala anayewaunganisha wanafunzi wa chuo na watu wa nje kuwafanyia mitihani hiyo kinyume cha taratibu.
Akizungumzia udhibiti wa wanafunzi hao, Andekisye alisema chuo hicho kiko katika mchakato wa kubadili vitambulisho kwa wanafunzi na kuongeza nguvu katika usimamizi.
Alisema wanafunzi waliobainika kufanyiwa mitihani watafikishwa kwenye bodi ya chuo na waliowafanyia watapelekwa polisi, kwani tukio hilo ni la kughushi.
Sina hakika kama tutafika kwa mwendo huu.
WATU watatu, akiwamo mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Azania, jijini Dar es Salaam wamekamatwa wakiwafanyia mitihani wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaosoma ngazi ya stashahada ya juu pamoja na shahada.
Mwanafunzi huyo, Frank Kaduma, aliyekuwa anamfanyia mtihani mwanafunzi aliyemtaja kwa jina moja la Tina, alikuwa ameahidiwa na mtu aliyemuunganisha na mtahiniwa huyo kuwa baada ya kutoka kwenye mtihani huo angelipwa sh 150,000.
Tanzania Daima ilimshuhudia mtuhumiwa huyo akihojiwa na Michael Andekisye, ambaye ni Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo.
Msajili huyo alisema kuwa kitambulisho alichokuwa akikitumia kumfanyia Tina mtihani kilikuwa na jina la Christian Mbago, mwanafunzi wa mwaka wa tatu.
Kaduma alifafanua mbele ya ofisi hiyo kuwa aliitwa na rafiki yake ambaye hata hivyo hakutaka kumtaja jina, na baadaye alimuunganisha na mtahiniwa na kukubaliana kiasi hicho cha fedha baada ya kazi hiyo kumalizika.
Mimi ninasoma Azania, nachukua PCM (Fizikia, Kemia na Hisabati), rafiki yangu anasoma masomo ya biashara na mtihani wa leo una hisabati, hivyo juzi nilikuja naye ili anionyeshe darasa na leo ndiyo nimekuja kumfanyia mtihani, alisema Kaduma.
Wakati mwanafunzi huyo akihojiwa, mwanafunzi mwingine, John Kapinga, alikamatwa na kupelekwa katika ofisi ya msajili baada ya kukutwa akimfanyia mtihani mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuoni hapo, Joel Mlengule, anayesoma Stashahada ya Juu ya Hifadhi ya Jamii (Advanced Diploma in Social Protection).
Kapinga, alikiri kuwa alihitimu kidato cha sita mwaka 2003, akisoma masomo ya PCM, pamoja na kuahidi kwamba angetoa ushirikiano ili kumkamata mtahiniwa halisi.
Sikutaka kufanya, ila nilishawishiwa mara nne sikutaka, hata ikafikia hatua ndugu yake kunishawishi, nikakubali, ila dhamiri ikinisuta. kwani hakuna malipo yoyote tuliyoahidiana na ndugu yangu huyo, alisema Kapinga huku akijiinamia.
Tanzania Daima ilishuhudia kitambulisho chake kikiwa na jina la Joel Mlengule, kikiwa na namba ya usajili ADSP/16492/2007 na kinamalizika muda wake mwaka huu.
Kwa upande wake, Joel Mlengule, aliyefanyiwa mtihani na kukamatwa akiwa nje ya eneo la IFM akimsubiri Kapinga, alinaswa na walinzi wa chuo na kuhojiwa, ambapo alikiri kufanyiwa mtihani na Kapinga.
Mlengule ambaye ni mkazi wa Upanga, jijini Dar es Salaam, alikiri kuwapo mtu aliyemuunganisha na Kapinga, baada ya kufeli somo lake la hesabu mara mbili mfululizo, hivyo hakutaka hali hiyo imrudie, hasa ikizingatiwa kuwa huo ulikuwa mtihani wa mwisho chuoni hapo.
Ni kweli alikuwa ananifanyia mtihani baada ya kufeli somo hili mara mbili. Niliona mwaka huu, na huu ni mtihani wangu wa mwisho, mimi sijui hesabu, ndiyo maana hata aliponiambia anifundishe nilikataa na kumwomba anisaidie kunifanyia, alisema Mlengule.
Kwa mujibu wa Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo, tukio jingine la namna hiyo lilitokea jana, ambapo msichana mmoja alikimbia na kuacha viatu vyake, baada ya kubainika kuwa alikuwa akimfanyia mtihani mwanafunzi ambaye jina lake halikupatikana mara moja.
Aliongeza kuwa, mwaka jana matukio hayo yalitokea na imebainika kuwa kuna wakala anayewaunganisha wanafunzi wa chuo na watu wa nje kuwafanyia mitihani hiyo kinyume cha taratibu.
Akizungumzia udhibiti wa wanafunzi hao, Andekisye alisema chuo hicho kiko katika mchakato wa kubadili vitambulisho kwa wanafunzi na kuongeza nguvu katika usimamizi.
Alisema wanafunzi waliobainika kufanyiwa mitihani watafikishwa kwenye bodi ya chuo na waliowafanyia watapelekwa polisi, kwani tukio hilo ni la kughushi.
Sina hakika kama tutafika kwa mwendo huu.