ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
- Thread starter
- #21
Upo sahihi mkuu, labda inategemea pia na aina ya kozi ambayo mtoa hoja anajaribu kuziungumzia..kwa ujumla ukienda vyuo vingi vya umma vinajitosheleza kwa kiasi kikubwa na ufuatiliaji wa mitaala.generalization yako sio sahihi mkubwa na ningependa uangalie vyuo binafsi kwa umakini kabla ya kutoa maoni humu JF. Mfano ukiangalia vyuo vingi vya umma ndio vinaongoza kwa wanachuo wake kufanya mafunzo ya vitendo mfano pale ardhi kila mwisho wa muhula wanachuo wote wanafanya field na ni kwa mda wa siku 80,ukienda udsm pia courses nyingi ukiondoa za CASS na UDBS(kwa mwaka wa kwanza hawana mafunzo ya vitendo) ila collages zingine wanafanya haya mafunzo.
Ukija kwenye vyuo binafsi huko ni mwendo wa projects yani wanachuo mpaka wanahitimu hawajawahi fanya haya mafunzo sasa kwa hali ya kawaida tu unatarajia ufanisi kutoka kwa muhitimu huyo? Maana wengi wao mpaka wakae sawa inabidi ofisi itumie nguvu ya ziada ili akae sawa katika hiyo taaluma ambayo kwa ofisi zinazo-recruit vizuri hawezi kupata nafasi muhitimu wa hivyo vyuo binafsi.