Kakke
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,883
- 1,482
[h=2][/h]
Wanafunzi wa Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere, (MNMA) mjini hapa wamekuwa wakitishiwa maisha na watu wasiyojulikana kutokana na kuacha nywele na mabega wazi.
Wakizungumza na NIPASHE jana wanafunzi hao walisema kwamba wamekuwa wakipokea vitisho kutoka kwa watu wasiyojulikana wanapokwenda chuoni na kurudi katika hosteli wanayoishi huko Mtaa wa Maisara kisiwani Unguja.
Wanafunzi hao waliyataja maeneo ambayo yamekuwa yakitumiwa na watu hao kutoa vitisho dhidi yao ni maeneo ya Bububu, Darajani na Mkunazini Mkoa wa mjini Magharibi Zanzibar.
Walisema kwamba wamekuwa wakizomewa na kutishiwa maisha yao kutokana na kutembea bila kufunika vichwa na mabega pamoja na kuvaa nguo zinazobana mwili.
Tangu tumeanza masomo tumekuwa tukiishi bila amani kutokana na vitendo vya unyanyasaji na ubaguzi tunaofanyiwa wakati sote ni Watanzania. Walilalamika wanafunzi hao walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar.
Wanafunzi hao walitoa mfano juzi katika makutano ya barabara ya Bububu na Chuo hicho watu wasiyojulikana waliandika maneno ya vitisho kwa rangi nyekundu na kusababisha wasiwasi mkubwa kwa wanafunzi hao.
Faida ya muungano ongezeko la ngono Zanzibar, hatutaki muungano Zanzibar. Yalisomeka maandishi hayo.
Akizungumza na NIPASHE, Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Mushi Jackson, alisema kwamba bado hajapokea malalamiko ya wanafunzi wake kutishiwa maisha.
Alisema kwamba kwa mujibu wa sheria wanafunzi wa vyuo hawatakiwi kuvaa sare isipokuwa wanatakiwa kuvaa nguo za heshima wanapokuwa katika mazingira ya Chuo.
Hata hivyo Kamishina wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, alisema kwamba watafanya uchunguzi kuhusiana na vitendo hivyo.
Hata hivyo haliwataka wanafunzi hao kuripoti matukio kama hayo polisi ili uchunguzi uweze kufanyika na wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.
Chuo hicho kimezinduliwa mwaka huu huko katika Mtaa wa Bububu, na wanafunzi 300 asilimia 95 ni wanafunzi kutoka Tanzania bara.
CHANZO: NIPASHE
Wanafunzi wa Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere, (MNMA) mjini hapa wamekuwa wakitishiwa maisha na watu wasiyojulikana kutokana na kuacha nywele na mabega wazi.
Wakizungumza na NIPASHE jana wanafunzi hao walisema kwamba wamekuwa wakipokea vitisho kutoka kwa watu wasiyojulikana wanapokwenda chuoni na kurudi katika hosteli wanayoishi huko Mtaa wa Maisara kisiwani Unguja.
Wanafunzi hao waliyataja maeneo ambayo yamekuwa yakitumiwa na watu hao kutoa vitisho dhidi yao ni maeneo ya Bububu, Darajani na Mkunazini Mkoa wa mjini Magharibi Zanzibar.
Walisema kwamba wamekuwa wakizomewa na kutishiwa maisha yao kutokana na kutembea bila kufunika vichwa na mabega pamoja na kuvaa nguo zinazobana mwili.
Tangu tumeanza masomo tumekuwa tukiishi bila amani kutokana na vitendo vya unyanyasaji na ubaguzi tunaofanyiwa wakati sote ni Watanzania. Walilalamika wanafunzi hao walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar.
Wanafunzi hao walitoa mfano juzi katika makutano ya barabara ya Bububu na Chuo hicho watu wasiyojulikana waliandika maneno ya vitisho kwa rangi nyekundu na kusababisha wasiwasi mkubwa kwa wanafunzi hao.
Faida ya muungano ongezeko la ngono Zanzibar, hatutaki muungano Zanzibar. Yalisomeka maandishi hayo.
Akizungumza na NIPASHE, Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Mushi Jackson, alisema kwamba bado hajapokea malalamiko ya wanafunzi wake kutishiwa maisha.
Alisema kwamba kwa mujibu wa sheria wanafunzi wa vyuo hawatakiwi kuvaa sare isipokuwa wanatakiwa kuvaa nguo za heshima wanapokuwa katika mazingira ya Chuo.
Hata hivyo Kamishina wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, alisema kwamba watafanya uchunguzi kuhusiana na vitendo hivyo.
Hata hivyo haliwataka wanafunzi hao kuripoti matukio kama hayo polisi ili uchunguzi uweze kufanyika na wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.
Chuo hicho kimezinduliwa mwaka huu huko katika Mtaa wa Bububu, na wanafunzi 300 asilimia 95 ni wanafunzi kutoka Tanzania bara.
CHANZO: NIPASHE