Wanafunzi wa kike Saluni,UHUNI MTUPU!

Msafiri Kasian

JF-Expert Member
Sep 9, 2011
2,133
659
Leo niliingia SALUNI moja mitaa ya Holili(BODA)-Moshi mida ya saa 11 jioni,kwaajili ya kupunguza nywele.Nikawakuta wanafunzi wawili wa kike(kati ya kidato cha 2 hadi 4). Kinyozi naye amekaa kwa pembeni,anatafuna Mirungi na Big G huku wakipiga stori.Matendo niliyoyaona ambayo siwezi kuyaandika,ni kwamba binti mmoja kati ya wale alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na kinyozi yule.Kinyozi akaanza kunihudumia huku akijisifu kuwa yeye anafahamika sana,punde si punde wakaingia wanafunzi wengine wawili wa kike.Hawa walikuwa ni wa form 4(mmoja alikuwa na kitabu cha chemistry form 4) ktk shule moja hapa holili.Kinyozi akanifinya kidogo,akaniambia "sinimekuambia nafahamika? Hawa wote nawanyoa mimi" akawasha muziki,wanafunzi wakaanza kucheza hapo,mara nyingine anaacha kuninyoa,anacheza nao kidogo.Ni mengi nimeyashuhudia jamani. Sasa ikabidi,wale wasichana wamkazanie jamaa aninyoe haraka "wewe vipi? mnyoe kaka wa watu haraka unamchelewesha!"
Sasa mimi nikajiuliza,hizi division 4 and 0 zitapungua kwa hali kama hi? Na maambukizi ya magonjwa ya zinaa je?
MAONI YANGU: Wazazi wenye watoto wanaosoma shule za kutwa,muwe makini na watoto wenu kwasababu,wengi wanaharibikia mitaani,disco na sehemu kama hizi alafu mwisho wa siku wanafeli masomo yao,alafu lawama zote anatupiwa mwalimu shuleni na serikali.
 
ok kiongozi,umetimiza wajibu wako wa kufikisha ujumbe hapa jamvini,lakini nadhani ingekuwa bora zaidi kama ungeenda mbali zaidi ya hapo,je wewe sio mzazi?Je ulifanya nini katika kufikisha ujumbe/elimu kwa hao mabinti na huyo kijana wa salon kwamba wanachokifanya si sahihi au ni sahihi lakini sikatika muda muafaka?..au mkuu uliburudika walipokuwa wanashake then baada ya kumaliza kilichokupeleka ndio ukagundua lililofanyika si sahihi?..Fikiri na next time chukua hatua stahili.
 
wazazi wamesahau watoto wao..hapa wa kulaumiwa ni mzazi na hakuna mwingine

hapo akirudi nyumbani utasikia,"tulikuwa kwenye discussion!" akitumwa,hata maji tu utasikia "ah! Mimi nimechoka bwana.!" tatizo hata wazazi wetu wengine hawajali kuwauliza watoto wao,na ikiwezekana,kufuatilia maendeleo yao.
 
Well spoken, i feel pity those people

fundi mkweli ni kinyoziiiiii! Ambapo kichwa chako humwachiii,ila ana sifa zake nyingiiiii! Fundi kinyozi! Hahaaaa,nimekumbuka huu wimbo wa enzi zile bongo flava inaitwa ya wahuni.
 
ok kiongozi,umetimiza wajibu wako wa kufikisha ujumbe hapa jamvini,lakini nadhani ingekuwa bora zaidi kama ungeenda mbali zaidi ya hapo,je wewe sio mzazi?Je ulifanya nini katika kufikisha ujumbe/elimu kwa hao mabinti na huyo kijana wa salon kwamba wanachokifanya si sahihi au ni sahihi lakini sikatika muda muafaka?..au mkuu uliburudika walipokuwa wanashake then baada ya kumaliza kilichokupeleka ndio ukagundua lililofanyika si sahihi?..Fikiri na next time chukua hatua stahili.

Usiwaze! Leo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika saluni pale.Kwa sasa naishi karibu kabisa na hapo,nilipanga kuhudhuria saluni pale mara nyingi kwa nia ya kupiga stori na yule jamaa ili nipate full data. Ndipo nitazungumza,ikiwa ngumu,nitaongea na waalimu wao ambao nawafahamu. Sikufurahia kitendo hicho,ukizingatia kwa sasa mimi ni mwalimu wa muda ktk shule ya jirani yao. NITAFANYA UCHUNGUZI WA UHAKIKA,NA NITACHUKUA HATUA.
 
Usiwaze! Leo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika saluni pale.Kwa sasa naishi karibu kabisa na hapo,nilipanga kuhudhuria saluni pale mara nyingi kwa nia ya kupiga stori na yule jamaa ili nipate full data. Ndipo nitazungumza,ikiwa ngumu,nitaongea na waalimu wao ambao nawafahamu. Sikufurahia kitendo hicho,ukizingatia kwa sasa mimi ni mwalimu wa muda ktk
shule ya jirani yao. NITAFANYA UCHUNGUZI WA UHAKIKA,NA NITACHUKUA HATUA.

Mkuu msafiri, nakushauri kuwa makini na mtazamo wa the don. Kwa maisha ya siku hizi mtoto wa mwenzako sio mwanao kama zamani. Na hata usishangae ukitaka kuwarekebisha wazazi wao wakisikia wakuone wewe ndo mbaya. Ukijaribu kuwaeleza chochote hao wanafunzi au huyo kinyozi utashangaa matusi ya nguoni utayoyapata na fedheha itakuwa juu yako. Labda kidogo kama ukiwataarifu walimu wa shule hiyo inaweza ikawa njia sahihi kidogo. Kizazi cha sasa hivi hakina maadili na heshima. Kama hauna direct control juu yao hawawezi katu kukusikiliza wala kukuheshimu.
 
Mkuu msafiri, nakushauri kuwa makini na mtazamo wa the don. Kwa maisha ya siku hizi mtoto wa mwenzako sio mwanao kama zamani. Na hata usishangae ukitaka kuwarekebisha wazazi wao wakisikia wakuone wewe ndo mbaya. Ukijaribu kuwaeleza chochote hao wanafunzi au huyo kinyozi utashangaa matusi ya nguoni utayoyapata na fedheha itakuwa juu yako. Labda kidogo kama ukiwataarifu walimu wa shule hiyo inaweza ikawa njia sahihi kidogo. Kizazi cha sasa hivi hakina maadili na heshima. Kama hauna direct control juu yao hawawezi katu kukusikiliza wala kukuheshimu.

Umeongea point! Kwanza kinyozi mwenyewe anakula mirungi,hawezi kosa na bangi huyu. Nitaendelea kuobserve alafu ntaongea na waalimu wao.
 
Ni kweli fanya ivyo na utakuwa umeplay your part. Tunapenda sana kuwasaidia wanyooke kwenye njia bora lakini lazima tujiangalie na upande wetu. Hakuna anayependa kufehedheka kwa ajili ya wengine
 
Mkuu mbona hiyo cha mtoto sana?
Yawezekana huko ni maajabu lakini huku dar umri kama huo analisha familia kwa ile biashara ya uchi.
Ukipita kwenye baadhi ya maklabu,bar na hata zile sehemu maarufu wanazojiuza mabinti hukusi kuwaona hawa mabinti.
Usiku wanakesha biasharani asubuhi wanaenda shule ukiwaona asubuhi waendapo shule wamechoka sana kimwili na kiakiri kwenye madaladala full kusinzia wakifika shule ndo hoi kabisaa mda wote wanasinzia kama bundi.

Ikiwa tu mkuu wa kaya pamoja na wadhifa wake wote aliokuwa nao kashindwa kumkochi mwanae mwanaasha mpaka form 4 kataga ukiangalia hakuna alichokikosa sembuse kwa watoto wasomao sant kayumba?? Tena wao ndio hugeuka na kuwa wazazi wa famili.
 
hivi bado vitoto sana na ni chini ya miaka 20 ..nadhani umri unawaruhusu kufanya haya...
nakumbuka enzi zangu niko pale Tboys nlikuaga naibuka disco vumbi night ni noma kila siku...
na ukikutana na mimi utaeza kufikiri nsapoteza mwelekeo ila mwisho wa siku nkatoka na DVSION ONE Huyoo nkasepa mlimani..
lo tukikutana huezi amini..ni umri tuu huwa unapita
 
Back
Top Bottom