Msafiri Kasian
JF-Expert Member
- Sep 9, 2011
- 2,133
- 659
Leo niliingia SALUNI moja mitaa ya Holili(BODA)-Moshi mida ya saa 11 jioni,kwaajili ya kupunguza nywele.Nikawakuta wanafunzi wawili wa kike(kati ya kidato cha 2 hadi 4). Kinyozi naye amekaa kwa pembeni,anatafuna Mirungi na Big G huku wakipiga stori.Matendo niliyoyaona ambayo siwezi kuyaandika,ni kwamba binti mmoja kati ya wale alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na kinyozi yule.Kinyozi akaanza kunihudumia huku akijisifu kuwa yeye anafahamika sana,punde si punde wakaingia wanafunzi wengine wawili wa kike.Hawa walikuwa ni wa form 4(mmoja alikuwa na kitabu cha chemistry form 4) ktk shule moja hapa holili.Kinyozi akanifinya kidogo,akaniambia "sinimekuambia nafahamika? Hawa wote nawanyoa mimi" akawasha muziki,wanafunzi wakaanza kucheza hapo,mara nyingine anaacha kuninyoa,anacheza nao kidogo.Ni mengi nimeyashuhudia jamani. Sasa ikabidi,wale wasichana wamkazanie jamaa aninyoe haraka "wewe vipi? mnyoe kaka wa watu haraka unamchelewesha!"
Sasa mimi nikajiuliza,hizi division 4 and 0 zitapungua kwa hali kama hi? Na maambukizi ya magonjwa ya zinaa je?
MAONI YANGU: Wazazi wenye watoto wanaosoma shule za kutwa,muwe makini na watoto wenu kwasababu,wengi wanaharibikia mitaani,disco na sehemu kama hizi alafu mwisho wa siku wanafeli masomo yao,alafu lawama zote anatupiwa mwalimu shuleni na serikali.
Sasa mimi nikajiuliza,hizi division 4 and 0 zitapungua kwa hali kama hi? Na maambukizi ya magonjwa ya zinaa je?
MAONI YANGU: Wazazi wenye watoto wanaosoma shule za kutwa,muwe makini na watoto wenu kwasababu,wengi wanaharibikia mitaani,disco na sehemu kama hizi alafu mwisho wa siku wanafeli masomo yao,alafu lawama zote anatupiwa mwalimu shuleni na serikali.