Wanafunzi wa kike na mimba mashuleni.

Da Womanizer

JF-Expert Member
May 24, 2010
1,577
148
Habari wanaJF. Hivi bandugu hamuoni kuwa kumbebesha mzigo wote wa makosa mwanaume ikitokea mwanafunzi amepewa mimba ni sawa na kusema kwamba wanawake ni wapumbavu sana kiasi kwamba hawawezi kufikiria na kujua lipi ni bora na lipi baya kwao. Naomba nieleweke vizuri hapa, kwa sababu kwa utaratibu ambao upo sasa msichana akipata mimba anachukuliwa kuwa ni "innocent" ( kwa maneno mengine alidanganywa tu) na hatakiwi kuwajibika kwa lolote na ndio maana anatakiwa kurudishwa shule na kuendelea kusoma bila adhabu yeyote. Ni kweli mwanaume ana makosa makubwa sana kufanya mapenzi na mwanafunzi lakini mimi nadhani msichana kama binadamu mwenye akili naye pia anatakiwa kuwajibika kwa upande wake. Lakini kwa mtindo tunaotaka kuutumia utafanya wanaume waendelee kuamini wako juu kuliko wanawake na utawafanya wanawake siku zote wajishushe yaani tunapiga hatua 1 mbele kuboresha hali ya wanawake halafu tunapiga hatua 2 kurudi nyuma. Kitu kingine kuhusu hawa wasichana wanaofanya mapenzi na "baba" zao ni kwamba sio kweli huwa wanadanganywa mara zote, saa nyingine unakuta kabisa kitoto cha shule kinafanya kila mbinu kukutega wewe mtu mzima (kwa kifupi ni vicheche), na kama ujuavyo kila mtu ana ukomo wa uvumilivu especially kwa wanaume kwenye kipengele kizima cha ngono ni rahisi mno kutegeka.
Kuna mengi ningependa kuongelea hapa ila kwanza naomba michango yenu wakuu.
 
mmh what i see iz -2-1=?
yote ni malipo ya dhambi tu nan aadhibiwe saaana nan aonewe uruma.........kitendawili upon em wenye busara na hekima

chamuhimu chek mazingira ya uyo mtoto kupata mimba.....then u wl b in gud position to say,judge.

nawasilisha ......:fish2:
 
Wakuu mbona kimya!!!!!!! Ningependa sana kusikia Noname, WoS, Charity an MJ1 mnasemaje kuhusu hili..Of coz na wengine pia ambao ckuwataja.
 
Back
Top Bottom