Wanafunzi wa Elimu ya Juu Anzisheni .....

SolarPower

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
223
27
Kutokana na uwezo wa kifedha walionao vijana wetu wa Elimu ya Juu, nawashauri wakusanye nguvu zao pamoja na kuanzisha Benki yao. Ushauri ni kuwa kila Mwanafunzi wa Elimu ya Juu awekeze angalau shilingi 500 kila siku kwa kununua hisa za Benki watakayoianzisha. Kwa utaratibu huu kwa mwaka mmoja tu, watakuwa na uwezo wa kukusanya mtaji usiopungua shilingi bilioni 27. Baada ya miaka 10 naamini watakuwa na tawi la hiyo benki yao katika kila mkoa kama sio katika kila wilaya hapa chini. Kupitia Benki hii vijana wetu wengi wapata fursa nzuri ya kuweza kujiajiri na kutimiza ndoto zao katika katika maisha yao.
 
Changanua zaidi wakuelewe! Hiyo 500 ni makadirio ya wanafunzi wangapi? Kama ni mia 5 kwa siku ina maana ni sh.15,000/= kwa mwezi. Kwa wanafunzi wanaotegemea loan tu hiyo ni pesa ya mlo wa siku 3 hadi nne. Vipi kuhusu miezi ambayo haipo kwenye budget yao, wataweza mudu changia hizo 15?
 
Changanua zaidi wakuelewe! Hiyo 500 ni makadirio ya wanafunzi wangapi? Kama ni mia 5 kwa siku ina maana ni sh.15,000/= kwa mwezi. Kwa wanafunzi wanaotegemea loan tu hiyo ni pesa ya mlo wa siku 3 hadi nne. Vipi kuhusu miezi ambayo haipo kwenye budget yao, wataweza mudu changia hizo 15?

kwahiyo wewe unashauri nini?
 
Changanua zaidi wakuelewe! Hiyo 500 ni makadirio ya wanafunzi wangapi? Kama ni mia 5 kwa siku ina maana ni sh.15,000/= kwa mwezi. Kwa wanafunzi wanaotegemea loan tu hiyo ni pesa ya mlo wa siku 3 hadi nne. Vipi kuhusu miezi ambayo haipo kwenye budget yao, wataweza mudu changia hizo 15?

Nashukuru kwa maswali uliyouliza. Naomba nikujibu ifuatavyo

1. Hizo shilingi 500 ni uwekezaji wa kila siku. Kama mtu akishindwa kabisa njia rahisi ni kufunga kwa siku moja kila wiki ambapo kila wiki atakuwa na akiba isyopungua shilingi 5,000. Fedha hizi zitamuwezesha kununua hisa za shilingi elfu tano kila wiki.

2. Idadi ya wanafunzi wa elimu ya juu ni zaidi ya laki moja.

3. Kwa siku ambazo hawapo chuoni, baadhi zitafidiwa na akiba watayoiweka kutokana na fedha ya mkopo wanayopata wakiwa shuleni. Naomba wanafunzi wetu waelewe kuwa mtu aliyewekeza shilingi milioni 1.5 kwa kununua pikipiki fedha anayopewa kila siku na dereva wake haizidi shilingi elfu 7 kwa siku. Pia ni muhimu kufahamu kuwa kama umewekeza katika biashara ya Bajaj hutegemei kupata zaidi ya shilingi elfu 15 kwa siku na ili uwe na hiyo Bajaj utatakiwa kuwekeza si chini ya shilingi milioni 5.6

4. Ni muhimu sana kwa vijana wetu walioko elimu ya juu wakawa ni mfano wa kuigwa katika kuweka AKIBA. Ukweli ni kwamba kama wanafunzi wetu wakiamua kukusanya nguvu zao pamoja wana uwezo kwa kila mmoja wao kuweka akiba ya angalau shilingi 1,500 kila siku wawapo chuoni.
 
Hii itasaidia nini??

NingaR,

Asante kwa swali lako. Kimsingi faida ni nyingi. Naomba nitaje baadhi.

1. Vijana wetu watakuwa na uwezo mkubwa wa kiuchumi ambao utawasaidia kufanya uwekezaji wa kiwango chochote kile watakachoamua kwa pamoja.

2. Iwapo watatekeleza ushauri huu wa kuanzisha benki yao, wataacha urithi mzuri kwa vizazi vijavyo katika kuendeleza kila walichokianzisha watangulizi wao.

3. Benki yao itawasaidia katika kuzipatia mikopo kampuni mbalimbali ambazo vijana wetu watakuwa wamezianzisha.

4. Benki yao itakuwa na mchango mzuri katika uchumi wa nchi yetu kwa kusaidia sekta mbalimbali kwa njia ya mikopo na ushauri.

5. Wataondoa hali ya utegemezi, watakuwa imara kifikra na kivitendo kwa kuamini kuwa wanaweza kutenda na kuanzisha jambo lolote kwa pamoja na kufanikiwa.

6. +UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU+

 
Back
Top Bottom