BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
Date::11/25/2008
Wanafunzi vyuo vikuu wataka mjadala na Rais Kikwete
Na Hussein Kauli na Angela Mwakilasa
Mwananchi
MARAIS wa Serikali za wanafunzi wa vyuo vinavyounda Umoja wa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini (UVEJUTA), wameomba kukutana na Rais Jakaya Kikwete ili wamweleze juu ya athari za Sera ya uchangiaji wa elimu ya juu nchini.
Wanafunzi ho walisema jana jijini Dar es Salaam kwamba wanataka kukutana na Rais Kikwete kwa sababu ndiye anayeweza kuyapatia ufumbuzi matatizo yao.
Hatua hiyo imechukuliwa na wanafunzi hao mikutano yao na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa. Jumanne Maghembe, kujadili suluhisho la madai yao kutotoa mwelekeo sahihi.
"Tumefanya majadiliano mengi tu na viongozi wa Serikali, lakini ufumbuzi wa madai yetu haukupatikana. Sasa kwa kuwa tunapenda kutumia nji ya majadiliano tumeona mtu pekee anayeweza kuyapatia ufumbuzi madai yetu ni Rais Jakaya Kikwete," alisema Rais wa DARUSO, Anthony Machibya.
Hata hivyo baadhi ya viongozi hao, wameipokea kwa mitazamo tofauti kauli ya Rais Kikwete ya kuwataka wanafunzi waliofukuzwa ambao wanakubaliana na sera ya uchangiaji, warejee vyuoni, wakisema kuwa inalenga kuwagawa wanafunzi walio na wasio na uwezo wa kuchangia elimu.
"Sisi viongozi wa wanafunzi hatuna matatizo na matamko yaliyotolewa viongozi wa serikali, ila matatizo yetu yako kwenye masharti magumu ya kurejea vyuoni ambayo yanaonesha kuwa viongozi wa Serikali hawana lengo la kumaliza migomo ya wanafunzi kutokana na sera mbovu ya uchangiaji," alisema Machibya.
Naye Rais wa Chuo Kikuu Ardhi, Masawe Anthony alisema hali ya kifedha kwa asilimia kubwa ya wazazi wa wanafunzi mbaya hivyo kuwaambia wachangie Sh400,000 hadi Sh1 milioni kunawafanya wanafunzi wengi washindwe kulipa.
Naye Rais wa Serikali ya Wanafunzi ya Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT), Cleophas Mahalangata alisema: "Tumeipokea kauli ya Rais Kikwete kwa masikitiko makubwa kwa sababu, inalenga kuwagawa wanafunzi wenye uwezo na wasio na uwezo na kibaya zaidi inawakandamiza wasio na uwezo".
Kwa upande wa Rais wa serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Tiba na Afya Muhimbili, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja huo, Godbless Charles, alisema anashangaa Rais Kikwete kutoa kauli tofauti na aliyoitoa mwaka jana katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kuwa hakuna mwanafunzi atakayeshindwa kusoma kwa kukosa ada.
Viongozi hao pia wamepinga masharti yaliyotolewa na Wizara ya Elimu ya kuwataka wanafunzi waliofukuzwa vyuoni kujaza fumu za kukubaliana na sera ya uchangiaji kabla hawajareshwa vyuoni, wakisema haina lengo la kumaliza kiini cha matatizo yao.
Walibainisha kuwa wanafunzi wanaotoka katika familia masikini hawataweza kukidhi vigezo vya sera hiyo na kwamba, wanaweza wakajaza fomu za mikataba hiyo lakini wengi watashindwa kulipa kwa sababu ya kukosa uwezo.
"Tumesikitishwa na kauli ya Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Gaudensia Kabaka akiwataka wanafunzi wanaotaka kurejea vyuoni kujaza fomu za kukubaliana na sera ya uchangiaji, kwa sababu si rahisi kupata fedha hizo katika kipindikifupi," alisema Gogbless.
Wanafunzi vyuo vikuu wataka mjadala na Rais Kikwete
Na Hussein Kauli na Angela Mwakilasa
Mwananchi
MARAIS wa Serikali za wanafunzi wa vyuo vinavyounda Umoja wa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini (UVEJUTA), wameomba kukutana na Rais Jakaya Kikwete ili wamweleze juu ya athari za Sera ya uchangiaji wa elimu ya juu nchini.
Wanafunzi ho walisema jana jijini Dar es Salaam kwamba wanataka kukutana na Rais Kikwete kwa sababu ndiye anayeweza kuyapatia ufumbuzi matatizo yao.
Hatua hiyo imechukuliwa na wanafunzi hao mikutano yao na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa. Jumanne Maghembe, kujadili suluhisho la madai yao kutotoa mwelekeo sahihi.
"Tumefanya majadiliano mengi tu na viongozi wa Serikali, lakini ufumbuzi wa madai yetu haukupatikana. Sasa kwa kuwa tunapenda kutumia nji ya majadiliano tumeona mtu pekee anayeweza kuyapatia ufumbuzi madai yetu ni Rais Jakaya Kikwete," alisema Rais wa DARUSO, Anthony Machibya.
Hata hivyo baadhi ya viongozi hao, wameipokea kwa mitazamo tofauti kauli ya Rais Kikwete ya kuwataka wanafunzi waliofukuzwa ambao wanakubaliana na sera ya uchangiaji, warejee vyuoni, wakisema kuwa inalenga kuwagawa wanafunzi walio na wasio na uwezo wa kuchangia elimu.
"Sisi viongozi wa wanafunzi hatuna matatizo na matamko yaliyotolewa viongozi wa serikali, ila matatizo yetu yako kwenye masharti magumu ya kurejea vyuoni ambayo yanaonesha kuwa viongozi wa Serikali hawana lengo la kumaliza migomo ya wanafunzi kutokana na sera mbovu ya uchangiaji," alisema Machibya.
Naye Rais wa Chuo Kikuu Ardhi, Masawe Anthony alisema hali ya kifedha kwa asilimia kubwa ya wazazi wa wanafunzi mbaya hivyo kuwaambia wachangie Sh400,000 hadi Sh1 milioni kunawafanya wanafunzi wengi washindwe kulipa.
Naye Rais wa Serikali ya Wanafunzi ya Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT), Cleophas Mahalangata alisema: "Tumeipokea kauli ya Rais Kikwete kwa masikitiko makubwa kwa sababu, inalenga kuwagawa wanafunzi wenye uwezo na wasio na uwezo na kibaya zaidi inawakandamiza wasio na uwezo".
Kwa upande wa Rais wa serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Tiba na Afya Muhimbili, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja huo, Godbless Charles, alisema anashangaa Rais Kikwete kutoa kauli tofauti na aliyoitoa mwaka jana katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kuwa hakuna mwanafunzi atakayeshindwa kusoma kwa kukosa ada.
Viongozi hao pia wamepinga masharti yaliyotolewa na Wizara ya Elimu ya kuwataka wanafunzi waliofukuzwa vyuoni kujaza fumu za kukubaliana na sera ya uchangiaji kabla hawajareshwa vyuoni, wakisema haina lengo la kumaliza kiini cha matatizo yao.
Walibainisha kuwa wanafunzi wanaotoka katika familia masikini hawataweza kukidhi vigezo vya sera hiyo na kwamba, wanaweza wakajaza fomu za mikataba hiyo lakini wengi watashindwa kulipa kwa sababu ya kukosa uwezo.
"Tumesikitishwa na kauli ya Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Gaudensia Kabaka akiwataka wanafunzi wanaotaka kurejea vyuoni kujaza fomu za kukubaliana na sera ya uchangiaji, kwa sababu si rahisi kupata fedha hizo katika kipindikifupi," alisema Gogbless.