samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Mawaziri wa mikopo katika serikali za wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu jana waliitisha kikao na kuutaka umoja wa vijana wa ccm kuacha kuingilia utendaji wa bodi ya mikopo na kutoa ushauri usio na tija wa kutaka bodi hiyo ivunjwe bila kushauri hatua mbadala. Tamko hilo lilikua na jibu kwa UVCCM ambao kupitia mjumbe wake zamaradi kawawa uliitaka serikali ya chama cha mapinduzi kuivunja bodi ya mikopo kwa kua imeshindwa kutimiza majukumu yake. Wakiongea na waandishi wa habari mawaziri hao wa mikopo waliionya uvccm iache kujitafutia umaarufu kwa kua bodi ya mikopo sio mali ya uvccm. Walisema ushauri uliotakiwa kutolewa ni wa kuboresha bodi hiyo. Aidha mawazili hao wa mikopo wameiomba serikali kuongeza pesa za kujikimu na malazi kutoka sh. 5,000 hadi sh 10,000 kutokana na kuongezeka kwa garama za maisha. Source: itv news sa mbili usiku jana. .