Wanafunzi UDSM wafa Njaa!

RedDevil

JF-Expert Member
Apr 30, 2009
2,367
1,519
WanaJF, kuna tetesi kuwa, mpaka sasa ni wiki ya tano inaingia tokea mhura wa pili ulipoanza lakini bodi ya mikopo haijaweza kuwapa wanafunzi fedha za kujikimu, na hali ni mbaya haswa kwa dada zetu na wale watoto wa masikini wasiokuwa na ndugu hapo dar. Wanafunzi sasa hawawezi kusema kwani wanaogopa kufukuzwa tena. Hebu nisaidieni ni kweli jamani, serikali pamoja na uongozi wa chuo haujui kuwa hawa ni binadamu kama wao wanahitaji kujikimu ikiwa ni maradhi pamoja na mahitaji mengine ya kibinadamu. kazi kwenu wanaJF najua mnajibu zuriii, ambalo laweza hata kuwasaidia hawa wenzetu. Ikiwezekana, kama kunamwanaJF mpiganaji huru atembelee kimya kimya aulize atupe habari kamili ili tujue hatuna serikali siku hizi. Karibuni kwenye mjadala huu.
 
Kuna uvumi kuwa wanafunzi UDSM, hawapata fedha ya kujikimu hadi sasa na ni wiki ya tano tokea chuo kifunguliwe. Jamaa, wamefanikiwa kuwanyamazisha, wanafunzi wanogopa hata kuuliza wala hawana mategemeo yakupata, hali ni mbaya kwa watoto wengi wa kike na masikini. Masomo hayaendi tena, wanaJF mwenye taarifa kamili atupe, maana nina dogo hapo kila siku ananilipua kamshahara.
 
jamani hampo au mpo? changieni maada hiyo, inaguza wengi na nisekta nyeti kweli kweli. kama kuna mwanjf YUPO KARIBU na UDSM atupe habari hizo. Kuna maafa ya kimya kimya hapo udsm na watu wako kimya. sa sijui pesa inazalishwa kwanza au ndo ufisadi unamiliki hadi vyuo vyetu vya umma.
 
Sio UDSM peke yao ni vyuo vyote hawajapewa hela ya Meals & Accomodation hadi kuna rumours kuwa hao jamaa wa Bodi walipanda DECI hizo fedha
 
jamani ni kweli UDSM hawajapata fedha hadi leo, nipeni taarifa jamani. Chanzo cha habari kinaeleza kuwa ni wiki ya tano lakini bado wanafunzi hawajui ni lini watapata. Watoto wa kike ndo balaa zaidi kwani njaa kali. Nipo mbali kidogo na TZ nipeni taarifa jamani.
 
Nani wa kuwajibika kwa hawa wanafunzi?

JK yuko Denmark/SA, Pinda yuko Sumbawanga! Waziri wa Elimu yuko Same ktk kuwatafuta wavuvi haramu!

Kwa nini hadi ichukuwe wiki 5 bila hatua? Je serikali inajali?
 
Kweli, si unajua tena serikali iko busy kuhakikisha suala la Rostamu na wenzake linaisha bila kuilazimisha kuwapeleka mahakamani kama ilivyolazimishwa kupeleka angalau watuhumiwa wachache wa fedha za EPA. Si mnakumbuka Sofia Simba na waziri mwenzake walivyokurupuka kumkemea Mengi.. kwa hilo wako 'very alart' lakini kwa masuala yanayohusu maisha ya wananchi 'wamelala fo fo fo'.

Pengine, wanafunzi ni wakati wao kujifunza kuhusu aina ya viongozi tulionao, na kuhakikisha wanatumia kula zao na ushawishi kwa wenzao na jamii inayowazunguka kuondoa viongozi wasiokuwa na tija kwa taifa hili.

Fedha za mkopo si za bure wa la si hisani wala siyo za kiongozi yeyote wa serikali, ni fedha za walipakodi, watendaji wa serikali wanapaswa kuhakikisha anayestahili analipwa na tena kwa wakati. kwa kuwa zipo tena kwa ajili hiyo na kikubwa zaidi ni za mkopo, zitarejeshwa, sasa kwa nini wanafunzi wanyanyaswe?

Mwenye masikio na asikie, mwenye akili na atafakari!
 
Uchaguzi unakaribia so viongozi sasa wameweka kipaumbele kwenye majimbo yao ili wapate uhakika wa kuchaguliwa tena mwakani
 
WanaJF, kuna tetesi kuwa, mpaka sasa ni wiki ya tano inaingia tokea mhura wa pili ulipoanza lakini bodi ya mikopo haijaweza kuwapa wanafunzi fedha za kujikimu, na hali ni mbaya haswa kwa dada zetu na wale watoto wa masikini wasiokuwa na ndugu hapo dar. Wanafunzi sasa hawawezi kusema kwani wanaogopa kufukuzwa tena. Hebu nisaidieni ni kweli jamani, serikali pamoja na uongozi wa chuo haujui kuwa hawa ni binadamu kama wao wanahitaji kujikimu ikiwa ni maradhi pamoja na mahitaji mengine ya kibinadamu. kazi kwenu wanaJF najua mnajibu zuriii, ambalo laweza hata kuwasaidia hawa wenzetu. Ikiwezekana, kama kunamwanaJF mpiganaji huru atembelee kimya kimya aulize atupe habari kamili ili tujue hatuna serikali siku hizi. Karibuni kwenye mjadala huu.

Hivi sisi watanzania TUMELOGWA???? Mbona hutuwezi kuwa serious hata siku moja? Kila siku utasikia tunalalamika elimu inashuka, wakati sisi wenyewe ndio tunaishusha kila kukicha. Viongozi wa Bodi ya Mikopo mbona mmelala, mnategemia nini kama mpaka sasa hamjawapatia wanafunzi wa elimu ya juu pesa ya meals and accomodation???

Mimi sidhani kama mtu anaweza kupiga shule huku akiwa hajui atakulanini machana na jioni.
 
Nipo SUA hali pia ni mbaya sana kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wa pili watoto wa wakulima wapo taabani wanakula chai na mkate kama mlo wa siku nzima,unategemea nini kwa msomi huyu? ndugu zangu inatia uchungu watu wanajuta kuzaliwa katika nchi ambayo vipaumbele vya watawala ni kinyume na mahitaji ya wananchi maskini
tumwombe MUNGU awakumbushe watawala wajibu wao katika jamii yetu
 
Wanafunzi nao wanatakiwa kueleza ukweli ni kitu gani kinaendelea kati yao na board. Suala lenyewe lilivyo ni kama ifuatavyo. Mwanzoni mwa muhula wa masomo, board ya mikopo ilitoa fedha pungufu kwa wanachuo (badala ya kuwapa pesa ya muhula mzima, ili wapatia ya nusu muhula (Miezi miwili, Sep/oct, Oct/Nov)). Wanafunzi wengi walilalamika sana maana wengi wao huwa wanatumia sehemu ya hiyo pesa kulipia hata hizo % ambazo hawalipiwi na board kwenye ada. Wakati board wanajiandaa kuwapatia pesa iliyokuwa imesalia, tayari wanachuo walikuwa katika hekaheka za mgomo. Kabla ya tangazo la kuvifunga vyuo halijatoka board ya mikopo ilipost hela tayari kwa baadhi wa wanachuo wa UDSM. Kwa DUCE karibia wanachuo wote walipewa pesa. Sina taarifa ya vyuo vingine. Hao walipewa kiasi gani? Walipewa pesa ya kumalizia miezi miwili ya mwisho ya muhula wa kwanza (Sh. 300,000 ambayo ilitakiwa iwe for Nov/Dec, Dec/Jan) na pesa ya kuanzia muhula wa pili (ya miezi miwili Sh 300,000 ambayo wangeitumia kwa mwezi Feb/March, march/April). Hivyo basi wakati chuo kinafungwa wale waliokwisha kupata hela walipokuwa wanaondoka walikuwa na jumla ya sh. 720,000 kwenye account zao. Walizitumiaje wakiwa nyumbani baada ya chuo kufungwa na baada ya chuo kufunguliwa ili kumalizia muhula wa kwanza tuwaulize wao.

Tukija kwa wale ambao hawakuwekewa hela kwenye account zao wakati vyuo vinafungwa. Wengi wao waliwekewa wakati vyuo vilipofunguliwa mwezi january na february. Na wao walipewa pesa kama wenzao jumla sh. 600,000 ikiwa na maana kuwa sehemu ya hiyo pesa ni kwa ajili ya miezi miwili ya mwisho ya muhula wa pili (sh. 300,000 ambazo zilikuwa ni kwa ajili ya Feb/March, March/April) na nyingine ni nyingine ni kwa ajili ya miezi miwili ya mwanzo ya muhula wa pili (sh. 300,000, April/May, May/June). Nina mdogo wangu na mtoto wa uncle wanasoma UDSM ambao niliwashauri wanipatie pesa niwahifadhie ambazo nilikuwa kwa za muhula wa pili (300,000). Hili nililifanya kutokana na experience yangu nilipokuwa mwananchuo. Nilishuhudia wananchuo wengi wakipata shida kutokana na matumizi mabovu. Akina dogo walikuwa waelewa walinipatia zile pesa (jumla 600,000). Chuo kilipofunguliwa mid April niliwapatia pesa zao zote.


Wanachuo wengi walikuwa wameshalipwa pesa kwa ajili ya miezi miwili ya mwanzo ya muhula wa pili (April/May, and May/June). Kama wanaidai board, basi ni ile pesa sh. 300,000 ambazo ni kwa aliji ya mwezi June/July, July/Aug. Na kwa kawaida ya board hiyo pesa ingetolewa kwenye tar. 10 mwezi wa sita. Kwa mwanachuo ambaye anadai sh. 600,000 mpaka sasa, huyo hata akigoma mi namuunga mkono maana atakuwa anaonewa kwa kiasi kikubwa. Wengine waliobaki watafute tu njia nzuri ya kunegotiate na board kwa sababu hawana sababu ya msingi ya kugoma maana muda wa kupewa pesa yao iliyobaki haujafika.

Mambo niliyo observe ni kuwa, Board hawana utaratibu mzuri wa kutoa pesa, na wanachuo wengi nao hawana mpango mzuri wa kutumia pesa.





 
Sio UDSM peke yao ni vyuo vyote hawajapewa hela ya Meals & Accomodation hadi kuna rumours kuwa hao jamaa wa Bodi walipanda DECI hizo fedha

Wajinga tu hawa watu wa bodi ya mikopo, this shit does not add up at all, ila pesa za kuwaongezea misharahara wabunge mambumbu serikali inazo???!!!!!

Education hapa bongo is going down the toilet sio siri.

.....Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu za zamani, haya twende uswahili uswahili tu.
 
Ukweli ni kwamba wanafunzi wengi wa vyuo nao waliwekeza pesa zao DECI. Hivyo hawana hata akiba kwenye akaunti zao.
 

Mambo niliyo observe ni kuwa, Board hawana utaratibu mzuri wa kutoa pesa, na wanachuo wengi nao hawana mpango mzuri wa kutumia pesa.

Hiyo mtaani wanakwambia "KWA MWIZI KAINGIA JAMBAZI... VURUGU TUPU"
 
leta data za uhakika sio maneno ya saluni.......
wala sio maneno ya salon, nina rafiki aliweka pesa DECI nae sasa anahaha na pesa ya kula. Maana alitegemea kuvuna lkn kama ujuavyo tena Serikali imewakatili DECI hivyo watu hawawezi kuvuna tena kama walivyotegemea.
 
Ukweli ni kwamba wanafunzi wengi wa vyuo nao waliwekeza pesa zao DECI. Hivyo hawana hata akiba kwenye akaunti zao.


wala sio maneno ya salon, nina rafiki aliweka pesa DECI nae sasa anahaha na pesa ya kula. Maana alitegemea kuvuna lkn kama ujuavyo tena Serikali imewakatili DECI hivyo watu hawawezi kuvuna tena kama walivyotegemea.
nikisema maneno ya saluni unabisha.......kwa kuwa ni rafiki yako mmoja basi wewe ume generalize kuwa ni wanafunzi woote.....njoo na data zingine...
 
nikisema maneno ya saluni unabisha.......kwa kuwa ni rafiki yako mmoja basi wewe ume generalize kuwa ni wanafunzi woote.....njoo na data zingine...
wengi tu, rafiki yangu ni mfano mmojawapo. Ukitaka data zaidi utapata subiri zinakuja.
 
Back
Top Bottom