Wanafunzi tunaosoma Algeria kwa Udhamini wa Serikali, tumecheleweshewa Mikopo, hali ni mbaya

Malcom the X

New Member
Nov 11, 2016
3
8
Mpaka lini wanafunzi wa chuo tunaosoma nchini Algeria kwa udhamini wa serikali ya Tanzania tutaendelea kuteseka kwa kucheleweshewa fedha za mkopo ?

Tabia hii imekubuhu na inatunyong'onyeza sana na kuififisha imani yetu juu ya serikali ya nchi yetu na kutufanya tujiulize kama kweli serikali yetu inajali watu wake kwa kadri inavyopaswa au imekuwa ikisema inafanya hivyo kisiasa tu????
Sasa ni takribani miezi 3 imepita tangu muda rasmi wa kupewa mkopo na hakuna taarifa zozote za matumaini kutoka wizarani pia bodi ya mkopo ambao wanaonekana hawana mamlaka juu ya hili kwani kila wanapowasiliana na viongozi wetu wanawaambia wanasubiri waagizwe na uongozi wa juu.

Sasa tunapenda kuwataarifu wale wote wanaohusika kuwa tumechoka kuvumilia kwani hali ya kifedha ni mbaya sana, kuna watu wanaumwa lakini hawawezi kwenda kupata matibabu kwa sababu gharama ni kubwa, kuna wanafunzi shule karibu itawashinda kwa sababu hawana pesa za kufanya research( gharama za internet ni kubwa na pesa hakuna ) , vifaa vya shule hakuna pesa ya kununulia, hatuna pesa za kununulia mavazi ya kujikinga baridi , ulaji wetu ni wa tabu sana ( afya zetu zimedhoofika ) .

Kwa kifupi ni kwamba wanafunzi tulioletwa na serikali ya Tanzania nchini Algeria hatupo katika mazingira stahiki ya kimasomo kwa sababu ya kukosa pesa ambazo serikali kipitia bodi ya mikopo inapaswa kututumia.
Hivyo tunaomba serikali itume pesa upesi ili kunusuru janga hili kwa sababu tunaamini inaweza ama sivyo itume tiketi za ndege wanafunzi wote turudishwe nyumbani ili tusiendelee kuteseka bila sababu za msingi.

Wanafunzi walioalgeria wamejitolea kuja kusoma kwa ajili ya maendeleo ya taifa la Tanzania, hivyo wakiwa kama raia wema na wazalendo tunaomba haki zetu zizingatiwe na utu wetu usidhihakiwe .

Sisi pamoja na wengine wote walipolekwa nchi mbalimbali ni mashujaa wa taifa la Tanzania hivyo serikali itutendee inavyowapasa mashujaa na sio kama waomba misaada.

N.B
Tumeyasema haya si kwa hasira bali kwa kadri tulivyoguswa na hali yetu
 
Daah poleni sana jaman MUNGU awafanyie wepesi but mtapata tu ............japo hata ss local undergraduate bado hatujapata baadh yetu japo nlisoma govt tangu vidudu mpaka six(PCB) na pale kuna death certificate ni Shida kaka
 
Hii tz govt inazngua.....
Inaleta siasa hadi kwenye masuala nyet ya elmu........
Polen sana wazalendo
 
Msije kushangaa kuambiwa ''nani aliwapeleka huko''? Nakumbuka December 2013 wakati tifu limeanza kati ya Dr. Machar na Salva Kiir pale Sudan ya Kusini, serikali ya Eritrea iligoma kutuma ndege kwenda kuwaevacuate raia wake maana Watawala wa Eriteria walisema ''hawajui hao raia wanafanya nini huko na waliendajeendaje''
 
Tunanunua ng'ombe kwanza kuku badae!

Ndege na viwanda ndo kipaumbele cha awamu 5,

AJIRA,ELIMU,STAHIKI ZA WATUMISHI NA KATIBA SIO KIPAUMBELE CHA JPM, subirini ndege zifke tulizolipia cash maana bado zipo viwandani! Serikali inafanya kitu kimoja kimoja sasa kama kinachokuhusu kitakua cha mwsho basi kitafanyika 2020 ili utoe kura yako tena!
 
Muda si mrefu Serikali itaanza kuwakiki wanafunzi wote wanaolipiwa nje ya nchi na baadhi yao watarudishwa wasomee nchini tu maana hata Je.sika tunae huku..
 
Mpaka lini wanafunzi wa chuo tunaosoma nchini Algeria kwa udhamini wa serikali ya Tanzania tutaendelea kuteseka kwa kucheleweshewa fedha za mkopo ?

Tabia hii imekubuhu na inatunyong'onyeza sana na kuififisha imani yetu juu ya serikali ya nchi yetu na kutufanya tujiulize kama kweli serikali yetu inajali watu wake kwa kadri inavyopaswa au imekuwa ikisema inafanya hivyo kisiasa tu????
Sasa ni takribani miezi 3 imepita tangu muda rasmi wa kupewa mkopo na hakuna taarifa zozote za matumaini kutoka wizarani pia bodi ya mkopo ambao wanaonekana hawana mamlaka juu ya hili kwani kila wanapowasiliana na viongozi wetu wanawaambia wanasubiri waagizwe na uongozi wa juu.

Sasa tunapenda kuwataarifu wale wote wanaohusika kuwa tumechoka kuvumilia kwani hali ya kifedha ni mbaya sana, kuna watu wanaumwa lakini hawawezi kwenda kupata matibabu kwa sababu gharama ni kubwa, kuna wanafunzi shule karibu itawashinda kwa sababu hawana pesa za kufanya research( gharama za internet ni kubwa na pesa hakuna ) , vifaa vya shule hakuna pesa ya kununulia, hatuna pesa za kununulia mavazi ya kujikinga baridi , ulaji wetu ni wa tabu sana ( afya zetu zimedhoofika ) .

Kwa kifupi ni kwamba wanafunzi tulioletwa na serikali ya Tanzania nchini Algeria hatupo katika mazingira stahiki ya kimasomo kwa sababu ya kukosa pesa ambazo serikali kipitia bodi ya mikopo inapaswa kututumia.
Hivyo tunaomba serikali itume pesa upesi ili kunusuru janga hili kwa sababu tunaamini inaweza ama sivyo itume tiketi za ndege wanafunzi wote turudishwe nyumbani ili tusiendelee kuteseka bila sababu za msingi.

Wanafunzi walioalgeria wamejitolea kuja kusoma kwa ajili ya maendeleo ya taifa la Tanzania, hivyo wakiwa kama raia wema na wazalendo tunaomba haki zetu zizingatiwe na utu wetu usidhihakiwe .

Sisi pamoja na wengine wote walipolekwa nchi mbalimbali ni mashujaa wa taifa la Tanzania hivyo serikali itutendee inavyowapasa mashujaa na sio kama waomba misaada.

N.B
Tumeyasema haya si kwa hasira bali kwa kadri tulivyoguswa na hali yetu


Kwani hamna Wazazi? Siku nyingine jifunzeni kuweka akiba ya fedha na siyo kustarehekea zote!
 
Ile kauli ya miaka ileeee... "Lazima RADAR inunuliwe hata kama tutakula nyasi".... ndio sasa inafanyiwa kazi.
 
Back
Top Bottom