Malafyale
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 13,813
- 11,126
ZAIDI ya wanafunzi 1,800 wa shule za misingi katika Manispaa ya Kigoma Ujiji, wanatumia mawe, magogo na mifuko ya plastiki maarufu kama rambo kama viti vya kukalia wawapo madarasani kutokana na uhaba wa madawati unaozikabili shule hizo.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano umebaini kuwa, kati ya shule 47 za Manispaa ya Kigoma-Ujiji, takribani asilimia 55 tu ya wanafunzi wanapata fursa ya kutumia madawati wakati wa masomo hali inayochangia kushuka kwa elimu katika wilaya hiyo.
Kwamba manispaa hiyo inakabiliwa na upungufu wa madawati 5,883 ili kukidhi haja ya wanafunzi kukalia madawati, hasa wakati wa masomo ambapo imefahamika kwa sasa kuna madawati 8,117 pekee.
Kwa mujibu wa maelezo ya baadhi ya wadau wa elimu, akiwamo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwasenga, Jeremia Ntibashima, changamoto ya upungufu wa madawati mashuleni unachangia taaluma za wanafunzi kuwa duni.
Mwalimu Ntibashima alifafanua kuwa, pamoja na majengo mazuri katika shule za manispaa, lakini bado suala la uhaba wa madawati ni la msingi katika kukuza na kuendeleza taaluma ya mwanafunzi shuleni.
Akizungumza na gazeti hili, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Tatala Mpangalukela alisema kuwa, moja ya njia ya haraka ya kuondokana na changamoto hiyo ni kwa wahisani na mashirika mbalimbali kusaidia misaada ya madawati.
Mpangalukela alifafanua kuwa, misaada ya wahisani na mashirika kwa kiasi kikubwa imechangia kupunguza uhaba wa madawati kwani manispaa hiyo imeshapokea madawati zaidi ya 419 kutoka kwa Hifadhi ya Taifa (TANAPA).
Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, John Mongella alieleza kuwa, ongezeko la shule za msingi katika kila kijiji na kitongoji, ni moja ya changamoto ambazo zinaikabili serikali na wadau wa elimu na kuwataka kushirikiana kwa pamoja kupata suluhisho.
Mongella alieleza kuwa, serikali imetatua tatizo kubwa la kukosa majengo kwa kujenga shule kila mahali, na sasa juhudi ni kuhakikisha kuwa madawati yanapatikana.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano umebaini kuwa, kati ya shule 47 za Manispaa ya Kigoma-Ujiji, takribani asilimia 55 tu ya wanafunzi wanapata fursa ya kutumia madawati wakati wa masomo hali inayochangia kushuka kwa elimu katika wilaya hiyo.
Kwamba manispaa hiyo inakabiliwa na upungufu wa madawati 5,883 ili kukidhi haja ya wanafunzi kukalia madawati, hasa wakati wa masomo ambapo imefahamika kwa sasa kuna madawati 8,117 pekee.
Kwa mujibu wa maelezo ya baadhi ya wadau wa elimu, akiwamo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwasenga, Jeremia Ntibashima, changamoto ya upungufu wa madawati mashuleni unachangia taaluma za wanafunzi kuwa duni.
Mwalimu Ntibashima alifafanua kuwa, pamoja na majengo mazuri katika shule za manispaa, lakini bado suala la uhaba wa madawati ni la msingi katika kukuza na kuendeleza taaluma ya mwanafunzi shuleni.
Akizungumza na gazeti hili, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Tatala Mpangalukela alisema kuwa, moja ya njia ya haraka ya kuondokana na changamoto hiyo ni kwa wahisani na mashirika mbalimbali kusaidia misaada ya madawati.
Mpangalukela alifafanua kuwa, misaada ya wahisani na mashirika kwa kiasi kikubwa imechangia kupunguza uhaba wa madawati kwani manispaa hiyo imeshapokea madawati zaidi ya 419 kutoka kwa Hifadhi ya Taifa (TANAPA).
Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, John Mongella alieleza kuwa, ongezeko la shule za msingi katika kila kijiji na kitongoji, ni moja ya changamoto ambazo zinaikabili serikali na wadau wa elimu na kuwataka kushirikiana kwa pamoja kupata suluhisho.
Mongella alieleza kuwa, serikali imetatua tatizo kubwa la kukosa majengo kwa kujenga shule kila mahali, na sasa juhudi ni kuhakikisha kuwa madawati yanapatikana.