Wana Kagera Njooni Hapa Tutete, Tujadili, Tuzungumze, Tufanye Maamuzi, na Tuchuke Hatua!

Nawaombeni ndg. zangu ni vema tukafahamu kama tuko njia sahihi. Awali nilishauri tusilaumu bali tupange na tuweke mikakati. Nashauri tena twaweza kuanza na kutambuana ni nani na wa wapi (kijiji/kata/wilaya) na unaishi wapi. Baada ya hapo tuweke mikakati ya kikanda/vijiji, kata/wilaya. Hatua hii itatutoa. Ukweli tunatakiwa kuunganisha nguvu. Hakuna ubishi hapo. Mimi ninaanza hivi: Ninatokea kijiji cha IGURUGATI, kata ya BUGANDIKA, wilaya ya MISSSENYI. Katika eneo ninalotoka kuanzia kijijini hadi wilayani changamoto ni zile zile; ugonjwa wa mnyauko wa migomba, kuporomoka kwa kiwango cha elimu, kuongezeka kwa idadi ya yatima, kushuka kwa uzalishaji wa kahawa, uwekezaji mdogo unaotokana na sisi wenyewe kutokurejea mara kwa mara nyumbani n.k. Hata hivyo, wilaya hii (vijiji na kata zake) zina miundo mbinu mizuri mfano barabara, umeme, mahospitali/vituo/zahanati na baadhi ya shule. Ninaamini sisi tunaweza kupambana na umasikini pamoja na kushuka kwa elimu katika wilaya ya Missenyi kama tutakuwa tayari kujitoa na kujitolea. Lazima tuchangie maendeleo ya watu wetu kama tunavyochangia ya wengine, mahali pengine kwenye ujenzi wa mashule, barabara, makanisa, shughuli za harusi n.k. Tunao uwezo wa kuchangia kuinua elimu angalau ya msingi na sekondari, tunao uwezo wa kusomesha yatima siyo lazima wawe ndugu wa kuzaliwa nao. Ebu tuanze. Nimeona mchangiaji mmoja anaelezea kuanzisha SACCOS. Naamini hii siyo njia mbadala ya kutatua matatizo yanayotukabili. Kwetu sisi hii siyo bali tunatakiwa kuwahimiza watu wetu kule Kagera waanzishe SACCOS na VICCOBA, tuwasaidie waanzishe hizo SACCOS. Pia, wengi wetu tumeanzisha na kujiunga kwenye vyama vya kufa na kuzikana. Sawa. Ebu tuwe na agenda endelevu. Tunatakiwa tushirikiane na watu wetu kuanzisha NGOs/CBOs zenye kulenga kuchochea maendeleo ya watu wetu na zifanyie kazi huku huko Kagera. Nawaombeni wana Kagera, wana Missenyi na wana Bugandika tuungane, tujitolee na tuchangie maendeleo ya Kagera. Asanteni
 
Hii mada ni nzuri kwa upande wangu mimi nadhani elimu ya uraia inahitajika sana kwa wanakagera hasa kwa vijana ambao ndiyo nguzo ya mabadiliko.Tunahitaji vijana wajipange ili kuchukua nafasi za uongozi kuanzia vitongoji,vijiji ,kata na hatimaye majimbo na tuje na mtazamo mpya juu ya swala la kilimo chetu cha kahawa na migomba ikiwezekana tupate kilimo mbadala cha biashara hapa tutakuwa tunafanya mapinduzi ya kiuchumi ndani ya mkoa wetu.Ili haya yote yafanikiwe ni lazima CCM ing'oke KAGERA hapa tutafanikiwa.

Tunahitaji vijana ambao ni wengi tuwe na mtazamo wetu mpya juu ya KAGERA YETU.

 
Ndugu zangu wenye mapenzi mema na mkoa wa Kagera,
Sitaweza kufika kwa sababu niko mbali kidogo na dar, lakini ningeomba niweke mchango wangu juu ya agenda za kuangalia. Pamoja na mambo mengine....
1. Kilimo cha migomba na mibuni - mazao haya yanazidi kuzorota - tuafute ufumbuzi wa matatizo yaliyopo. Sio siri, tunahitaji mbinu za kitaalamu, mfano migomba iliyoko mingi ilipandwa na babu za mababu zetu, hivyo si jambo la kushangaza itakapodhoofika maana ardhi nayoinachoka tunahitaji crop rotation, mixed farming, ect wataalamu wa kilimo watatweleza.
2. Elimu: Hili halina mjadala kuwa linarudi nyuma kila kukicha - ukosefu wa shule zenye ubora, umaskini - wazazi wanashindwa kuwalipia ada watoto, "references mbaya" - fulani alimaliza F.IV tuko naye anachapa konyagi, etc ..... tuyatafutie ufumbuzi
3. Kukomboa Mwenendo wa maisha ya mwanakijiji wa leo: wengi wamejikita kwenye pombe, fikra endelevu zitatoka wapi, tunalitatuaje hili?
4. Masoko: Mazao yanayozalishwa mkoani yakitafutiwa soko la kueleweka yatakuwa mkombozi. Tunafanya nini katika hili?
5. Uwekezaji: Watanzania wanawekeza kwenye mikoa mbali mbali lakini flow ya investment iko limited kwa baadhi ya mikoa - Kagera ni mojawapo. Hapa suala sio kulaumu - tufanye nini kuvutia uwekezaji?
6. Raslimali zilizolala miaka nenda rudi: Mkoa wa kagera umebarikiwa kuwa na mvua za kutosha, mito isiyokauka kwa mwaka mzima, lakini matunizi yake ni madogo sana. Kwa ujumla tukifanya kilimo kwenye ukanda tu wa mito hiyo, tunaweza kutatua tatizo la chakula na kufikia kuuza kwenye soko la nje bila shida. Tunafanya nini kukomboa watu wa Mungu na umaskini kwa kutumia rasrimali zinazowazunguka. Bandari za Kemondo na Bukoba zikitumiwa vizuri zitakuwa kichocheo cha maendeleo ya Tanzania kwa ujumla na si maendeleo ya kagera tu.
7. Strategic location: Kagera inapakana na nchi nyingine kama alivitaja mwandishi mmojawapo. Hii ni fursa nzuri ya kujipanga kufanya biashara za kimataifa na nchi hizo. In short kuna uwezekano kabisa wa ku-reverse soko la mazao badala ya kutoka bukoba kwenda mwanza, basi mazao yakatoka mwanza kuelekea kagera "on transit" kwenda nchi nyingine.

Mwisho OMBI LANGU KUBWA, naomba maongezi yetu yazingatie yafuatayo:
1. Tunapoongelea mkoa wa Kagera hatumaanishi wahaya, ni sehemu ya Tanzania, fursa zitolewe kwa watanzania wote. Hivyo mkutano wa kesho nategemea utakuwa na watu wa makabila yote, si lazima wahaya/wanyambo/wasubi/etc tu.
2. Neutrality muhimu sana - si sehemu ya kuanza kuchambua itikadi za kisiasa - jimbo gani limechagua chama gani, etc hii sio hoja ya kujadiliwa. Vyama vyote vina haki sawa na sote tulenge kuendeleza mkoa huu na si vinginevyo.
Ni hayo wapendwa, Mungu na awatangulie katika shughuli hii, pia tupeane feedback.
 
Ericus-kimasha

Mkuu shukrani kwa hii thread, jana sikupata muda kupitia kwenye hicho kikao pale Bamaga ila ulituhaidi kutupa-updates za nini kilijiri nadhani ungekuwa vyema kutujulisha ni lini kikao kitakaa tena. Ni ukweli uliowazi ubinafsi ulipitiliza ndo umetufanya tuwe hapo tulipo hatusogei..Nilipita maeneo ya Katoma kwenda Gera nikashangaa kuna ardhi nzuri sana inapendeza kwa maana hata kama kwa kilimo haifai lakini kutengeneza recreational centre ni mahala muafaka sijui sasa pakoje manake hii ilikuwa 2008..ni moja ya miradi

Lakini tukirudi kwenye kilimo chetu cha asili cha migomba,sidhani kama shida ni wataalam naamini tunao wakazi wa mkoa wa Kagera wenye weledi wa hili..tusaidiane..wakati huu kuna watu wanalia njaa..

Nikushukuru sana kwa hili wazo...ni kweli ukiwa na upendo wa dhati wa kwenu moyo utauma kwa jinsi Kagera inavyodidimia sio ki-elimu wala kiuchumi..

Tukwate a'mashaija..
 
Last edited by a moderator:
Mimi nashauri ktk hii movement iliyooanza tuwe strategic.
kwa mfano, baadhi ya wachangiaji wameainisha baadhi ya matatizo yanayokumba mkoa huu ambayo yanaitaji wataalam, kwahiyo basi kwakuwa mkoa huu umejalia wasomi ktk nyanja mbalimbali, jitihada zitumike kltk kuwasaka wataalam hao na kuhakikisha wanahudhuria vikao vya mipango maalum. Hii itasaidia kupata ushauriorecht di wa kitaalam na kutuongoza in a right direction.

otherwise nashauri kuendeleza majadiliana kwenye mitandao, ili kutoa nafasi kwa watu walio nje ya nchi kushiriki kikamilifu.
 
Hii mada ni nzuri kwa upande wangu mimi nadhani elimu ya uraia inahitajika sana kwa wanakagera hasa kwa vijana ambao ndiyo nguzo ya mabadiliko.Tunahitaji vijana wajipange ili kuchukua nafasi za uongozi kuanzia vitongoji,vijiji ,kata na hatimaye majimbo na tuje na mtazamo mpya juu ya swala la kilimo chetu cha kahawa na migomba ikiwezekana tupate kilimo mbadala cha biashara hapa tutakuwa tunafanya mapinduzi ya kiuchumi ndani ya mkoa wetu.Ili haya yote yafanikiwe ni lazima CCM ing'oke KAGERA hapa tutafanikiwa.

Tunahitaji vijana ambao ni wengi tuwe na mtazamo wetu mpya juu ya KAGERA YETU.
hapo kwenye red ndipo matatizo mengi yapoanzia, yaani kwa 'kihaya' wanaita MINDSET.
Unakuta baadhi ya vijana waliosoma au wanaishi nje ya mkoa wanapadharau sana na wakija huku wanapenda kutuonyesha sisi tulioko kuwa wanajua na kuelewa mambo zaidi wakati sisi tunataka kuona matunda ya 'ujuaji' wao! Tofauti na wale wa Kishumundu

Na kwa jinsi maisha yalivyo huku kwa sasa naona ni bora zaidi ya sehemu nyingi na muda sio mrefu kutakuwa bora zaidiukiondoa hili tatizo migomba na kahawa kuharibika.

 
wewe waliompigia salute alitoka nao dar hawajulikani kule hata mmoja nusura wapewe kipondo
na hayo matatizo msipoangalia yataendelea kuwasumbua maana kwa sasa Kagera inaelekea kuwa kama Pemba. Pemba kuna wafanyabiashara matajiri wengi sana na hata wasomi lakini wengi wao hawaishi huko na nasikia huwa hata kupaendeleza sio sana kama wanavyojenga pale Kariakoo.
...je, ni wanaKagera wangapi wana nyumba nzuri na biashara shehemu nyingine lakini hawapajui hata kwao!?

 
Namshukuru Mungu kwa huu uzi,ninatoa ushauri ndugu zangu mkoa wetu ni mkubwa na bado una heshima yake msiwaze sana kuhusu mnayosemwa na wengine juu ya mkoa wetu!naamini na bado naamini kupitia kwetu vijana tunao uwezo wa kukaa pamoja na kuwashawishi wenzetu walio nje ya mkoa ili watuunge mkono kwa matendo na mikakati ili tukaufanye mkoa wetu mahari pa kuvutia na kuwa mfano tena

Kwa kuanza mwezi ujao ntakuwa pale mjini kwa yeyote aliyeko tayari tuwasiliane ili tuendeleze mikakati hii ..0757244853,Rutta.
 
Lakini pia naomba na wengine tuweke namba zetu za simu hapa ili mchakamchaka uanze mara moja ...Tweshubeo banyansi ntugambwa kubi mara mbasheka ngu byayanga

Nimesema niko free mwezi ujao na ntakuwa Bkb naomba tuwe serious tutafutane tuondoe aibu,weka hapa namba ya simu ama npm ili tuweke network mapema tupeane majukumu na muda wa kutekeleza


Nawashukuru sana,wenu Rutta. 0757244853/0717522175.
 
Rweye: uko sahihi kabisa, wana-Kagera inabidi tujipange; kuna haja ya kuweka Mkakati wa kutafuta meeting point kwa ajiri ya kuangalia cha kufanya kwani tuna dalili zote za kudhalilika wakati Uwezo tunao.
 
Mleta hoja mungu akubariki, kwa kuboresha zaidi, nimeona orodha ni kubwa, kuna wanaoandika (academician poticians) na wanaofanya harakati za kisiasa bila ya kuandika, (political activists) orodha nimeona ni kubwa, wanaitaka KAGERA ya miaka ya 1970 kimaendeleo? na kama ndiyo, kwa yeyote mwenye nia njema hakika tutashirikiana naye kwa hali yoyote ile. Binafsi nahisi Nkenge ni rahisi kukombolewa, japo maeneo kama KIZIBA bado kuna changamoto ukilinganisha na KYAKA na kwenda mpaka MTUKULA. Huko Muleba sijafanya utafiti ikiwa ni pamoja na Bukoba vijijini, Ngara, Karagwe pamoja na Bukoba mjini ambapo panatakiwa 'abolition of property qualification' binafsi mimi natoke KIZIBA, binafsi nikiwa Kiziba na Kagera natoa changamoto kadri ya uwezo wangu. Tufanye nini, kwa wapenda maendeleo ya mkoa wa KAGERA, kwa vile tunaboresha hoja, itakuwa vizuri tukiunda kikosi kazi cha kutathmini MAJIMBO na nguvu inayotakiwa kutumika ktk jimbo husika. Nitaandika zaidi mara baada ya kupata maoni ya wadau. N.B, TULIOPO VYUONI TUJITAHIDI.
 
Nlikua muleba juzi hali ya chakula ni mbaya sana" mnyauko" ekabaita,engemu zona zikafa,na bahati mbaya hawataki kubadilisha mazao wameng'ang'ania migomba tu.
 
Nlikua muleba juzi hali ya chakula ni mbaya sana" mnyauko" ekabaita,engemu zona zikafa,na bahati mbaya hawataki kubadilisha mazao wameng'ang'ania migomba tu.

kwa maoni yako zao gani linafaa kuwa mbadala wa migomba?
 
Tatizo sio zao mbadala tatizo ni je kwa wakati huu migombe ikiwa imeharibika watu wafanyeje?kwasababu ugonjwa unapungua hvo nliwashauri wapande kwanza mihogo na viazi..migombo iliyobaki wang'oe wapande upya..
 
Pale juu nimetoa namba makusudi ili tutafutane hewani tujadili hukohuko siyo tuanze kupondeana hapa jukwaani na wengine hata hayawahusu wao kazi kucheka tu,naelewa wengi wetu hatupo popote na hatuwezi kukutana pamoja kwa wakati mmoja ila mie napendekeza walioko vyuoni mtambuane na tuwape majukumu,walioko dar hivyo pia,Bkb pia na sehemu zingine
Si lazima hadi tuwe maelfu,ila tukianza wengine watarealize na watatusapoti for good,wekeni namba zenu za simu hapa mie niko tayari kuwakordinate nyote mlipo.
 
Back
Top Bottom