Capitalist
Senior Member
- Feb 3, 2011
- 164
- 27
Wadau nilikuwa na dada 1 ambaye nilimpenda sana nayeye alionesha kunipenda ila tulikuwa tunakaa sehemu tofauti mi nilikuwa nafanya kazi wilaya nyingi na yeye mkoani, nilipata likizo sept 2008 nikaspendi naye mwezi mzima, aliniambia kuwa anamimba nikamwambia poa usijali mi nitakuoa, niliondoka kurudi kazn mawasiliano yakawepo alijifungua mei 2009. Alinipa taarifa nikaenda nilimpatia mahitaji yote, nilikuta ameondoka kwao kudai kuondoa aibu kapanga nikalipa kodi ya nyumba, kitanda, chakula alidai mamake kampa. Kumbe yupo mwanaume mwingine ambaye ameambiwa hvyohvyo na anatunza, siku moja kanicall mtoto anaumwa nilifunga safari kwenda kumjulia mwanangu hali ndipo tulipogongana na jamaa tukaeleza na alikuwa ameshaanza kuishi naye, tukaelezana ukweli jamaa alichanganyikiwa mi nikachangayikiwa, mpaka sasa anaishi naye kang'ang'ania mtoto yule wake. je kama ww ungefanyaje?