Kipeperushi
Senior Member
- Aug 17, 2011
- 167
- 33
Tunafahamu kwamba mzee Kingunge ni miongoni mwa makada na wanasiasa wakongwe wa CCM. Kwa mujibu wa mzee Kingunge kikao kilichokaa kupitisha mabadiliko ya katiba hakikuwa na mamlaka ya kikatiba ya kufanya maamuzi hayo. Inasemekana kwamba kikao hicho kilitakiwa kutoa mapendekezo yaliyotakiwa kupelekwa kwenye Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM; ikiwa ndio kikao pekee chenye mamlaka ya kikatiba ya kupitisha mabadiliko ya katiba ya chama. Swali langu kwa wana-CCM ni hili:- Mnataka kutuambia kwamba katika kipindi chote ambacho mzee Kingunge amekuwa anakitumikia chama cha CCM hakuwa anajua anachokifanya mpaka leo híi aonekane kama ni mtu aliyekurupuka juu ya msimamo wake?