Wamisri wamuaga papa Shenouda

Boflo

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
4,384
4,409
Wamisri wamuaga papa Shenouda


20 Machi, 2012 - Saa 12:19 GMT


120318124030_shenouda_304x171_reuters_nocredit.jpg
Papa Shenouda


Idadi kubwa ya watu wamejumuika mjini Cairo katika mazishi ya Papa Shenouda wa Tatu wa Kanisa la Coptic.
Papa Shenouda alifariki Jumamosi akiwa na umri wa miaka themanini na minane.
Viongozi wa kijeshi nchini Misri wametangaza siku ya maombolezi ya kitaifa kwa heshima ya papa huyo aliyeongoza waumini wa Copti kwa zaidi ya miongo minne.
Baada ya misa mwili wa papa utasafirishwa na kuzikwa katika makao ya watawa eneo la Nile Delta.
Papa huyo alikuwa kiongozi wa kidini wa waumini hao ambao ni asilimia kumi ya idadi yote ya watu wa Misri.

Baada ya misa ya wafu , papa Shenouda atazikwa katika nyumba ya watawa ya St Bishoy monastery katika eneo la Nile Delta.
Wa Copti ndio jamii kubwa ya wakristo mashariki ya kati. Hii leo walipewa likizo kuweza kufanya maziko huku siku moja ya maomblozi ya kitaifa ikitangazwa.

Source: BBC
 
Mbona hamchangiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii

Wana Jf vipi....

Au mko Mabwepande??????????????????
 
mkuu we si umetoa habari subiri waje wajuzi wa maswala ya kimataifa.
 
Dini ya coptic Orthodox ililetwa na Mt Marko yule mmoja wa watu wanne walioandika injili kwenye miaka ya 64 AD. Papa Shenouda alipigwa marufuku na akawa kwenye exile kwa miaka 5 wakati Anwar Sadat. Lakini Hosni Mubaraka alipoingia madarakani alimruhusu Papa Shenouda aendelee kueneza injili takatifu na wafuasi wake. Jamii ya wakristu wa coptic inabaguliwa sana katika mfumo wa ajira na siasa hususam kwenye jeshi na polisi. Mwaka jana kanisa la Coptic Orthodox lilipata mapigo mawili baada ya vurugu za kuchomewa makanisa yao katika jini la Cairo
 
Dini ya coptic Orthodox ililetwa na Mt Marko yule mmoja wa watu wanne walioandika injili kwenye miaka ya 64 AD. Papa Shenouda alipigwa marufuku na akawa kwenye exile kwa miaka 5 wakati Anwar Sadat. Lakini Hosni Mubaraka alipoingia madarakani alimruhusu Papa Shenouda aendelee kueneza injili takatifu na wafuasi wake. Jamii ya wakristu wa coptic inabaguliwa sana katika mfumo wa ajira na siasa hususam kwenye jeshi na polisi. Mwaka jana kanisa la Coptic Orthodox lilipata mapigo mawili baada ya vurugu za kuchomewa makanisa yao katika jini la Cairo
Ila bado wanakeep rising in number-they are about 10-15 million in Egypt.
kwenye siasa boutros ghali nazan ni mtu wa dini hiyo aliyewahi kuwa na cheo cha juu pamoja na political influence nchini Egypt
 
Ila bado wanakeep rising in number-they are about 10-15 million in Egypt.
kwenye siasa boutros ghali nazan ni mtu wa dini hiyo aliyewahi kuwa na cheo cha juu pamoja na political influence nchini Egypt


Hata matajiri wawili au watatu wa kwanza huko egypt ni wa dini hii wanatoka Sanawirs Family wale wamiliki wa Orascom
 
Na wao pia ni wakristo? nataka nifahamu tu?

Kama ndio tofauti na wakatoliki, walutheri na walokole wetu huku TZ ni nini?
 
Na wao pia ni wakristo? nataka nifahamu tu?

Kama ndio tofauti na wakatoliki, walutheri na walokole wetu huku TZ ni nini?

soma hapa utapata mwanga japo kidogo

"Coptic" means Egyptian and Christians living in Egypt identify themselves as Coptic Christians. As a denomination they originated in the city of Alexandria, one of the most faithful, respected, and fruitful during the Apostolic period. Proudly, the Coptic Christians acknowledge and herald John Mark, (author of the Gospel of Mark), as their founder and first bishop sometime between A.D. 42 - A.D. 62. The Coptic church was actually the very first major split in the Church and it was well before there was such a thing as "Roman" Catholicism and it was also well before the East/West split. Prior to the major east/west schism of AD 1054, they were separated from the rest by the Council of Chalcedon in AD 451.

fwata link hii kwa maelezo zaid
What is the difference between Coptic, Russian, and Greek Orthodox religions?
 
Ni wakristu na huko ulaya una kutana na Orthodox wengine kama Eastern Orthodox, Russian Orthodox, Armenian Orthodox etc
 
Mbona hamchangiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii

Wana Jf vipi....

Au mko Mabwepande??????????????????
Haya tunachangia: Wameikalisha maiti kwenye kiti cha enzi huku wameivalisha mapambo na makofi makubwa ! Wako bize kupiga picha na kuiaga ! Hivi maiti huagwa !?? Kweli akili zinapishana ! Kiongozi wao wamemfanya kituko !
 
Na wao pia ni wakristo? nataka nifahamu tu?

Kama ndio tofauti na wakatoliki, walutheri na walokole wetu huku TZ ni nini?
Tofauti yao wakristo wa Coptic wanaweka maiti kwa kiti kisha wanaiaga ! Na wa TZ wanaiweka kwa sanduku kisha wanaiaga ! La msingi wote wanaaga ''maiti'' !
 
Back
Top Bottom