Wamiliki wa Bodaboda za biashara tukutane hapa

Angalizo pia kwa wamiliki,hili nimekuwa nikilisema sana pia:-
Pindi unapoomba dua au maombi wakati unaenda kazini au unapoamka,basi ombea pia drivers wako au waajiriwa wako ili mungu awalinde na awape wepesi kwenye biashara yao,ikiwemo kupata wateja wengi na wenye kheir na huduma hizo.Maana Driver akipata na wewe ndio umepata.

Na kwa sie Waislam ni kwamba Mtu ukimuombea dua njema mwenzio basi mungu anakuongezea wewe zaidi,na pia hutenga malaika wa kukuombea na wewe zaidi.Ila wengi wetu kidogo hili ni tatizo.Maana hata hawa Drivers tunaowaajiri na wao pia hutuombea sie mabosi wao ila tunakuwa hatujui,maana anaomba kwamba usifilisike,na ufanikiwe zaidi,ili leo na kesho na yeye umkumbuke pindi neema zinapozidi.

Mie Drivers wangu karibia wote ni wakristo,ila katika kila sikukuu zao kwa wale nilionza nao muda wa mwaka,basi huwa natoa pesa ya sikukuu zoote kwa imani yake.Na hesabu ya siku moja au mbili za sikukuu naiacha ili na yeye aweze kuhudhuria ibada kanisani,na pia apate muda wa ku enjoy na watoto nyumbani na kuwapeleka sehem za michezo ya watoto nk.
Unapokuwa na furaha nyumbani wewe na watoto basi jua na mwenzio umkumbuke kwa imani yake.

Ila wengi wetu aisee,akiisha nunua huwa hana lugha njema,yaani ni ku force kwenda mbele,kuna jamaa mmoja yeye ni mtu wa Ulabu,basi anaweza kumstukiza Driver hata kati ya wiki ampelekee pesa bar.Asipopeleka kazi kweli.
Sasa hata hawa Drivers wanachangamoto zao nyingi sana kutoka kwa Matajiri,na ndio maana Drivers wengi hupenda kudeal na chombo anachomiliki Mwanamke.

mungu akubarik sana kk endelea na moyo uo uo gud
 
Hili nilitaka kulijaribu:-(BODABODA ALL ARROUND SERVICES)
Nilikuwa na ndoto ya kuvuta hadi kufikia bodaboda kama kumi na tano hivi ili niunde kikampuni changu cha kutoa huduma kwa mfumo wa Call center(mtanielewa tu na kizungu changu cha bodaboda)
Yaani nakuwa na home office,halafu pikipiki zangu zoote nazifunga GPS Tracking System.
Ambapo itanifanya nijue pikipiki fulani ipo maeneo gani.

Sasa nilitaka kutengeneza website ya huduma zangua Vipeperushi,na aina zoote za kuitangaza huduma zangu.
-Yaani kwanza na guarantee huduma nzuri kwa wateja wangu,all drivers in uniform.

-Yaani kama mteja yupo Sinza,basi mie na track pikipiki gani ipo sinza au inaelekea Sinza,then na mdirect driver amfuate mteja alipo
Na hii inaendana na pia kila siku kuhakikisha kila Driver and bundle ya airtime kwenye sim yake on daily duty.

-Yaani nikakuwa na Stations zangu ambazo nakuwa naweka bodaboda kama tatu kila Center ndani ya jiji.
Na kama Driver base yake ipo Sinza,na akapata route ya Buguruni,basi hatorudi,atakaa Ilala ili ikitokea kazi ya huko aifanye ili kusave mafuta na ku make more profit.

Mfumo huu unaendana pia na personal businesss contacts za Drivers,maana wao wanakuwa na wateja wao,ila nilitaka kuweka mfumo ambao Drivers wote wanatoa huduma zinazofanana,ili kama personal Customer wa mhusika hayupo,basi anae take over afanye zaidi ya yule ili kuwa uniform.


Research:-
Ila nililifanyia uchunguzi wa kutosha saana,ikiwemo kwenda makampuni kadhaa mjini kuonana na staffs wa pale,na wengi sana waliniambia nianze haraka saana,wengine wanasema huwa wanahofu sana kuchukua bodaboda hovyo,lakini kwa vile wewe ni kampuni na una guarantee basi kwetu pia ni salama.Na unaweza hata kupata vitenda vya kutumwa mizigo midogo ya watu kama drivers wako wakionyesha uaminifu.Na mmoja akaniambia kwamba endapo iki work out basi kuna mengine mengi yatajitokeza yenye faida kwa kazi zangu.

Na hasa hili la kulipa kwa mwenzi pia wengi sana liliwavutia pia,maana wengine wanawatoto mashuleni walitaka niingie nao mkataba kwa maeneo yao.

Na kwa wafanyakazi wa Sekta binasfi na Serikali:-
Kwakuwa ni Kampuni na ina drivers wenye weledi na Smart,basi nilitaka kuingia mkataba na wafanyakazi binafsi wa kutoa huduma kwao,na malipo wafanye kwa mwezi.Hapa hata kama Driver hana mafuta,basi anakuja kuchukua Movement order ya full tank ili aweze kuhudumia wateja wetu.

Vyuo Vikuu,vyuo vya kawaida na baadhi ya Shule kwa wanafunzi :
Nilienda mlimani na Chuo cha Fedha,na vingine vidogo pamoja na shule kadhaa
Nashkuru sana nilipata support nzuri saana hasa kwa wanafunzi wa kike.Walionesha sana kuvutiwa na huduma hii.Na pia walinipa pia changamoto kadhaa.
Na hii ni ni kwamba sio muda wote wanakuwa na pesa,nikawaambia mie kwanza huduma then kama kuna uhakika wapesa mie nafaham mazingira ya wanafunzi,mtalinipa mkipata.Ilimradi uungwana uwepo.Basi hili liliwavutia saana.Maana unahudumiwa then utalipa katika muda wa mwezi au muda ukipata pesa hata kabla ya mwezi,au inaweza kuwa zaidi ya mwezi pia kwa dharura za kipesa au kuchelewa kwa pesa.

Je Driver anafaidika vipi:-
Driver analipwa malipo yake in Percentage ya huduma atakazotoa.Kwanza kunakuwana basic Salay ambazo woote hupata.Then ndio kuna ratio ya huduma atakayotoa.
Na nilifanya uchunguzi kwamba hii huduma ndio ingeingizia Drivers pesa nyingi saana.Maana ingekuwa ajira rasmi

Je kwanini nilisita:-
Nilipeleka wazo kwa baadhi ya family members,na mwanasheria wangu.
Akaniambia wazo ni zuri sana tena ubunifu mzuri.Ila kipindi hiki ambazo bodaboda zipo kwenye Target ya wizi,ni hatari kwako pia.Wanawez kutokea majambazo,wakavaa uniform kama za Driver wako ili wafanye tukio,then ukaja kuzolewa wewe.Aisee hii ilinitisha kweli.Maana jambazi siku zote hutafuta wapi pa kusukumizia ushahidi ili awe Salama.
Ikabidi niache kabisaa wazo hili,na baada ya kuacha basi kila wiki kesi za bodaboda na ujambazi,duhhh ndio nikalifuta wazo kabisaaa.

Ila habari iliishia hapo,maana mie mtoto wa maskini,kuja kuingiza mtego wa ujambazi kirahisi duuh.Jela sitoki.

Kwa mwenye kuwa na Bajaji anaweza kuifanya hii naikafanyakazi vizuri:

Je nini nitafanya au mtu anaweza kufanya:-
Unajua kama mtu akiitumia JF vizuri aisee kama anamtaji atapiga hela kweli,ila mie ni kwa mawazo yangu tu wakuu juu ya hili.Maana mie hupenda sana kuheshim mawazo yangu hata kama mtu atanicheka huwa sijali.
Maana nimeanza kuchekwa zamani saaana juu ya maisha.Maana anaekucheka leo basi siku ukifanya na ukifanikia basi huwa hacheki tena ila anatabasam.Kwa hiyo kucheka Rukhsa na Kejeli kama kawaida yetu wana JF rukhsa,maana mie mwenyewe kuna siku nawazingua wenzangu humuhumu,hahaha
Na unajua wapo wanaokuecha na kukujelei na the same time wanakupa njia ya kufanya,humu wamo wengi sana na ninawakubali sana pia.

Wazo ni hili
Mfano,ukawa na Bajaji maalum au hata Taxis licha ya kwamba watu wanasema hazilipi,ila inategemea na ubunifu wako.
Mfano unaongea na mabosi wa JF kina MAX,kwamba unataka kutumia Jina lao kwa makubaliana,naamini ni waelewa,kisha ukafanya Car Branding,nimeweka picha hapo chini mfano.Yaani Logo na jina la kampuni yoote JF,yaani full JF urembo
Yaani inakuwa Branded kama JF na nakshi kibaooo
Mie naamini Members wengi will be proud kutumia gari lako kwa kukodi,hii ni imani yangu na mtizamo wangu wakuu.Huu mfumo unaweza kuanza na Taxi kama tano hivi au Bajaji kama Tano hivi.

Naamini na kwa imani yangu,Members karibia woote tutajivunia saana kutumia huduma zako,maana tunajua tunarejesha mrejesho kwenye JF family member.Ni wazo langu tu wakuu.
cars1.jpg mitchell-dejong-in-his-red-bull-rallycross-car.jpg
 
jaman eti spocket ina dum kwa muda gani? maana dreva wangu kila baada ya miez 3 nanunua nyingine
 
mm nilibadilisha mwez wa sita mpaka saa hz ipo poa ww ukiona hivyo jarbu upeleke kwa fund mwenyewe akuambie fund
 
jaman eti spocket ina dum kwa muda gani? maana dreva wangu kila baada ya miez 3 nanunua nyingine

Kwanza kama inaisha haraka namna hii ni kwamba Driver anafanya kazi vizuri,sasa asikuletee longolongo kwenye hesabu.
Unaweza kumlaumu Drivers lakini kuna sababu ambazo zonafanya kwisha haraka.Ni sawa na gari,unaweza kukuta fundi anaangalia tatizo tu,na sio kuangalia chanzo cha tatizo.Ila muda huo wa miezi mitatu naona kama ni mfupi sana,unless awe na kazi nyingi saana.

Cha msingi,weka mtego huu kama unamashaka,niliwahi kuuweka kwenye Gari yangu moja,basi siku hiyo hiyo nikamtimua kazi na ikawa fundisho kwa wenzie.
Nunua akiba iweke ndani,then itie alama maalum,na ikiisha toa ya mwanzo angalia alama iliyopo kama ipo.
Ukiona ipo basi jua ni kweli inaisha kwa kazi.Ila kama hakuna inakuwa ni mchezo kama wa kwenye Magari,anasema kifaa kimekufa ukinunua anaenda anakitoa kipya ulichofunga anapiga bei kwa driver mwenzie kisha anarejesha cha Mwanzo.

Ila usimkuhum,baadhi ya vifaa kwenye vyombo vya moto vinaweza kuisha haraka kwa chanzo cha upande mwingine kabisa tofauti na unapofikiria.Then jaribu kuwa na fundi wako maalum anaehakiki tatizo,sio kila muda kutegemea fundi wa Driver.
 
Hili nilitaka kulijaribu:-(BODABODA ALL ARROUND SERVICES)
Nilikuwa na ndoto ya kuvuta hadi kufikia bodaboda kama kumi na tano hivi ili niunde kikampuni changu cha kutoa huduma kwa mfumo wa Call center(mtanielewa tu na kizungu changu cha bodaboda)
Yaani nakuwa na home office,halafu pikipiki zangu zoote nazifunga GPS Tracking System.
Ambapo itanifanya nijue pikipiki fulani ipo maeneo gani.

Sasa nilitaka kutengeneza website ya huduma zangua Vipeperushi,na aina zoote za kuitangaza huduma zangu.
-Yaani kwanza na guarantee huduma nzuri kwa wateja wangu,all drivers in uniform.

-Yaani kama mteja yupo Sinza,basi mie na track pikipiki gani ipo sinza au inaelekea Sinza,then na mdirect driver amfuate mteja alipo
Na hii inaendana na pia kila siku kuhakikisha kila Driver and bundle ya airtime kwenye sim yake on daily duty.

-Yaani nikakuwa na Stations zangu ambazo nakuwa naweka bodaboda kama tatu kila Center ndani ya jiji.
Na kama Driver base yake ipo Sinza,na akapata route ya Buguruni,basi hatorudi,atakaa Ilala ili ikitokea kazi ya huko aifanye ili kusave mafuta na ku make more profit.

Mfumo huu unaendana pia na personal businesss contacts za Drivers,maana wao wanakuwa na wateja wao,ila nilitaka kuweka mfumo ambao Drivers wote wanatoa huduma zinazofanana,ili kama personal Customer wa mhusika hayupo,basi anae take over afanye zaidi ya yule ili kuwa uniform.


Research:-
Ila nililifanyia uchunguzi wa kutosha saana,ikiwemo kwenda makampuni kadhaa mjini kuonana na staffs wa pale,na wengi sana waliniambia nianze haraka saana,wengine wanasema huwa wanahofu sana kuchukua bodaboda hovyo,lakini kwa vile wewe ni kampuni na una guarantee basi kwetu pia ni salama.Na unaweza hata kupata vitenda vya kutumwa mizigo midogo ya watu kama drivers wako wakionyesha uaminifu.Na mmoja akaniambia kwamba endapo iki work out basi kuna mengine mengi yatajitokeza yenye faida kwa kazi zangu.

Na hasa hili la kulipa kwa mwenzi pia wengi sana liliwavutia pia,maana wengine wanawatoto mashuleni walitaka niingie nao mkataba kwa maeneo yao.

Na kwa wafanyakazi wa Sekta binasfi na Serikali:-
Kwakuwa ni Kampuni na ina drivers wenye weledi na Smart,basi nilitaka kuingia mkataba na wafanyakazi binafsi wa kutoa huduma kwao,na malipo wafanye kwa mwezi.Hapa hata kama Driver hana mafuta,basi anakuja kuchukua Movement order ya full tank ili aweze kuhudumia wateja wetu.

Vyuo Vikuu,vyuo vya kawaida na baadhi ya Shule kwa wanafunzi :
Nilienda mlimani na Chuo cha Fedha,na vingine vidogo pamoja na shule kadhaa
Nashkuru sana nilipata support nzuri saana hasa kwa wanafunzi wa kike.Walionesha sana kuvutiwa na huduma hii.Na pia walinipa pia changamoto kadhaa.
Na hii ni ni kwamba sio muda wote wanakuwa na pesa,nikawaambia mie kwanza huduma then kama kuna uhakika wapesa mie nafaham mazingira ya wanafunzi,mtalinipa mkipata.Ilimradi uungwana uwepo.Basi hili liliwavutia saana.Maana unahudumiwa then utalipa katika muda wa mwezi au muda ukipata pesa hata kabla ya mwezi,au inaweza kuwa zaidi ya mwezi pia kwa dharura za kipesa au kuchelewa kwa pesa.

Je Driver anafaidika vipi:-
Driver analipwa malipo yake in Percentage ya huduma atakazotoa.Kwanza kunakuwana basic Salay ambazo woote hupata.Then ndio kuna ratio ya huduma atakayotoa.
Na nilifanya uchunguzi kwamba hii huduma ndio ingeingizia Drivers pesa nyingi saana.Maana ingekuwa ajira rasmi

Je kwanini nilisita:-
Nilipeleka wazo kwa baadhi ya family members,na mwanasheria wangu.
Akaniambia wazo ni zuri sana tena ubunifu mzuri.Ila kipindi hiki ambazo bodaboda zipo kwenye Target ya wizi,ni hatari kwako pia.Wanawez kutokea majambazo,wakavaa uniform kama za Driver wako ili wafanye tukio,then ukaja kuzolewa wewe.Aisee hii ilinitisha kweli.Maana jambazi siku zote hutafuta wapi pa kusukumizia ushahidi ili awe Salama.
Ikabidi niache kabisaa wazo hili,na baada ya kuacha basi kila wiki kesi za bodaboda na ujambazi,duhhh ndio nikalifuta wazo kabisaaa.

Ila habari iliishia hapo,maana mie mtoto wa maskini,kuja kuingiza mtego wa ujambazi kirahisi duuh.Jela sitoki.

Kwa mwenye kuwa na Bajaji anaweza kuifanya hii naikafanyakazi vizuri:

Je nini nitafanya au mtu anaweza kufanya:-
Unajua kama mtu akiitumia JF vizuri aisee kama anamtaji atapiga hela kweli,ila mie ni kwa mawazo yangu tu wakuu juu ya hili.Maana mie hupenda sana kuheshim mawazo yangu hata kama mtu atanicheka huwa sijali.
Maana nimeanza kuchekwa zamani saaana juu ya maisha.Maana anaekucheka leo basi siku ukifanya na ukifanikia basi huwa hacheki tena ila anatabasam.Kwa hiyo kucheka Rukhsa na Kejeli kama kawaida yetu wana JF rukhsa,maana mie mwenyewe kuna siku nawazingua wenzangu humuhumu,hahaha
Na unajua wapo wanaokuecha na kukujelei na the same time wanakupa njia ya kufanya,humu wamo wengi sana na ninawakubali sana pia.

Wazo ni hili
Mfano,ukawa na Bajaji maalum au hata Taxis licha ya kwamba watu wanasema hazilipi,ila inategemea na ubunifu wako.
Mfano unaongea na mabosi wa JF kina MAX,kwamba unataka kutumia Jina lao kwa makubaliana,naamini ni waelewa,kisha ukafanya Car Branding,nimeweka picha hapo chini mfano.Yaani Logo na jina la kampuni yoote JF,yaani full JF urembo
Yaani inakuwa Branded kama JF na nakshi kibaooo
Mie naamini Members wengi will be proud kutumia gari lako kwa kukodi,hii ni imani yangu na mtizamo wangu wakuu.Huu mfumo unaweza kuanza na Taxi kama tano hivi au Bajaji kama Tano hivi.

Naamini na kwa imani yangu,Members karibia woote tutajivunia saana kutumia huduma zako,maana tunajua tunarejesha mrejesho kwenye JF family member.Ni wazo langu tu wakuu.
View attachment 296102View attachment 296103


fanyia kazi wazo lako la kwanza hakuna biashara ambayo haina changamoto, dawa ya changamoto ni kupambana nazo utafanikiwa inshaallah
 
Komaa kaka,we hata ukiibiwa Bodaboda moja kaza ongeza nyingine huku kesi ikiendelea.
Yaani hii biashara aisee inalipa asikudanganye mtu,ila kama mtoto wa mama unakimbia changamoto basi kaa mbali kabisa na biashara hii,utakuwa unanunia watu kila siku kwa kesi za Drivers,hahahaha

Maana wapo wamiliki hawataki kusikia Driver anaumwa wala anapata msiba wala anauguza,ebbbbo.
Na ndio maana wengi huwa hawabarikiwi kwenye game hii,maana wao wanajiangalia wao tu na pesa.

Mfanye Driver wako kama familia yako.Mie wapo Drivers wangu waliofiwa na wazee wao,basi huwa ndugu zangu waliopo Dar wanaenda msibani,na pia mie pia husafiri na kuja msibani au kama ninakazi basi Wife anapanda boat anakuja Dar kama siku nne then anageuza.Lakini lazima kati ya mie au wife aje Dar.Na the same akipata ajali lazima ndugu zangu wa Dar wahusike na the same time mie au wife anakuja Dar kumpa pole na kutoa mkono wa Pole.

Na kama ni ajali basi matibabu yoote tunasimamia sie,hata kama uzembe ni wa Driver basi mie huwa siangalii uzembe wake,kwanza ni kumshughulikia tiba yake then akiwa mzima ndio mengine yanafuata.Na sijawahi kumlaumu Driver kwa Uzembe wala kumlipish,maana hakuna anaependa ajali,muhim ni ushauri tu.Kisha natengeneza chombo changu siku zinaenda,na mungu mkubwa kwamba ajali nyingi sio kubwa saana.

Nikitengeneza naenda kugombana na watu wa bima,maana hawa jamaa wabishi kulipa kama wao hakuna.Wanaona Bodaboda kama vile ndio chanzo cha ajali zoote kumbe wazembe njiani ni wengi tu.
Mkuu asante nimepata kitu
 
Mie hutumia hivi:-
-Hesabu yangu mie ni kwa Wiki Tsh:50,000
-Na kila baada ya miezi sita tu nauza Chombo nanunua kingine,na huwa nanunua kwanza kisha nampa Driver halafu ndio nakiuza ili asikose kazi hata siku moja.Unless kuwe na jambo katikati.

Mkuu naomba ulueleweshe hapo faida yako inakuaje labda ajaelewa vzur, coz 50,000 kwa wiki,kwa mwezi itakua 200,000 na kwa miez sita ni 1200,000 then unaiuza kwa shling ngap?
 
Wakuu habar, nimewaita hapa, tupeane mbinu za biashara na changamoto zake, mbinu zangu mimi ni zifuatazo, huwa natumia mbinu ya kumwambia dereva kuwa ukileta hesabu wiki nzima, wiki inayofuata nampunguzia hesabu, badala ya 7000, namwambia alete 6000, hapo akirin nimepiga hesabu kuwa nimemuachia hesabu ya siku moja kama offer, na hapo biashara inaenda vizuri sana. njia nyingine, nawaambi kila tarehe 15 hutakiwi kuleta hesabu, na kila tarehe 30 utakiwi kuleta hesabu, na achukue yeye hizo pesa, lakini sharti langu siku zote lazima ulete hesabu kamili, ili uweze kupata offer hiyo.nawaombeni na nyinyi wenzangu mtoe mbinu zenu, ili tufanikiwe na hizi biashara.
Naomba kujua bei zake kwa sasa zikoje mkuu.
 
Mie hutumia hivi:-
-Hesabu yangu mie ni kwa Wiki Tsh:50,000
-Na kila baada ya miezi sita tu nauza Chombo nanunua kingine,na huwa nanunua kwanza kisha nampa Driver halafu ndio nakiuza ili asikose kazi hata siku moja.Unless kuwe na jambo katikati.

Mkuu naomba ulueleweshe hapo faida yako inakuaje labda ajaelewa vzur, coz 50,000 kwa wiki,kwa mwezi itakua 200,000 na kwa miez sita ni 1200,000 then unaiuza kwa shling ngap?
Zanzibar Spices
 
Mie hutumia hivi:-
-Hesabu yangu mie ni kwa Wiki Tsh:50,000
-Na kila baada ya miezi sita tu nauza Chombo nanunua kingine,na huwa nanunua kwanza kisha nampa Driver halafu ndio nakiuza ili asikose kazi hata siku moja.Unless kuwe na jambo katikati.

Mkuu naomba ulueleweshe hapo faida yako inakuaje labda ajaelewa vzur, coz 50,000 kwa wiki,kwa mwezi itakua 200,000 na kwa miez sita ni 1200,000 then unaiuza kwa shling ngap?
Asante mkuu kwa swali lako.
Maana huu mfano ni sawa na huku Zanzibar.
Ukitaka Dungu lililotumika miezi sita basi 16m - 20m
Mwaka 12m - 14m
Miaka miwili 8m - 10m
Maana huku gari hazichoki zinakuwa na zam,leo inapiga kesho off na mji mdogo.

Sasa nikija kwenye Jibu lako,unapouza chombo ambacho umekitumia muda mfupi na Driver akiwa mzuri basi unaweza kuuza karibia bei ya chombo kimpya.
Mfano:50,000 per week x 4 weeks x 6 months= 1,200,000
Sijawahi kuuza kwa bei ya chini ya 1.8m

Halafu pia ifahamike kwamba wakati pesa naikusanya ya week basi inaenda kuingiza pesa kwenye biashara yangu nyingine,nina viduka uchwara vya chakula,sasa pesa hiyo 50,000 inaingiza tena nyingine kwenye mlango mwingine.Sasa utakuta kwamba pesa unayopita na income yake kwa ujumla wakati wa mauzo ya pikipiki ni kubwa saana ila lazima uwe makini na ujue na kucheza na hesabu kibiashara.Kwa kipindi cha miezi sita

Wateja wangu wote nikiwauiza huwa wao ndio wananiletea wateja wengine,maana kila nikuza nampa Driver laki moja kwa kutunza chomo vizuri,so wanashindana.Na kwenye Carry niliuza moja ili kuibadilisha baada ya kufikia mwaka nimempa Driver laki tatu.Maana ilikuwakama mpya,jamaa alikuwa anipenda gari yake hadi namuohnea huruma aisee.

Sasa mkuu hapo juu unaweza kuona faida inakuwa vipi,ni zaidi ya milioni moja naingiza.
Ila lazima ujue kuallocate pesa yako,maana wafanyabiashara wengi wa bodaboda ukiwauliza pesa ipo wapi unakuta mtu hana,na yooote amekula,amelewea,amehonga,sasa kwa mfumo huo usitegemee kabisa kupiga hatua mkuu.

We mfano angalia hii hapa ilikuwa na miezi sita tu,ni kama mpya,hapo mbele iligonga kwa chini ya gari kwa break za ghafla ila haikuw aissue,ilinunuliwa faster.Picha hapo chini
 

Attachments

  • IMG_20140729_175337.jpg
    IMG_20140729_175337.jpg
    33.2 KB · Views: 107
wazo ni zuri sana usiangalie xn changamoto ila mi nakushaur anza ww kwanza na pikipiki yako then utakapo kuwa kijiweni utapata kujua nani mwaminifu na utamwajiri kwa sababu uaminifu ndio mapungufu makubwa ya bodabda drivers,pia kuwa na bodaboda chache na bajaj...badae ukienda poa unaweza anzisha kampuni ya kupeleka watoto mashulen na wafanyakaz maofisini na kampuni ya kusafirisha parcels......
 
wazo ni zuri sana usiangalie xn changamoto ila mi nakushaur anza ww kwanza na pikipiki yako then utakapo kuwa kijiweni utapata kujua nani mwaminifu na utamwajiri kwa sababu uaminifu ndio mapungufu makubwa ya bodabda drivers,pia kuwa na bodaboda chache na bajaj...badae ukienda poa unaweza anzisha kampuni ya kupeleka watoto mashulen na wafanyakaz maofisini na kampuni ya kusafirisha parcels......
Ni kweli huu mchango mzuri sana.
Ila kwa kuanza mwenyewe ni tatizo,maana wengi wanakuwa na ajira binafsi au nyingine.
Waaminifu wapo,muhim ni kujipanga,asipokuwa muaminifu unachukua chombo chako unatafuta mwingine,wale nao ni binaadam sio malaika.
Suala la kuanzisha Kampuni nalo ni zuri sana,sema tu wabongo tunasubiria aje mttoto wa waziri fulani aanzishe kisha tuseme anatubia hela zetu kwa kuanzisha kampuni,wakati hata mtu wa kawaida tu unaweza kuanzisha.

Na kwa uchunguzi wa haraka,ni kwamba Wanawake wengi ndio wanaongoza kumiliki Bodaboda.Licha ya kwamba mwanzo walianza wanaume wakakimbia changamoto na hatimae kinamama kupambana na kuweza kukomaaa.
 
Nataka kufanya hii biashara ya bodaboda ila sijui nianzie wapi.. Asante kwa dondoo mbili tatu mlizozitoa ila naomba mnisaodie process ya kumiliki chombo, kuanzia manunuzi, usajir, kuweka GPS, mpaka bima ili kuepuka usumbufu
 
Ni kweli huu mchango mzuri sana.
Ila kwa kuanza mwenyewe ni tatizo,maana wengi wanakuwa na ajira binafsi au nyingine.
Waaminifu wapo,muhim ni kujipanga,asipokuwa muaminifu unachukua chombo chako unatafuta mwingine,wale nao ni binaadam sio malaika.
Suala la kuanzisha Kampuni nalo ni zuri sana,sema tu wabongo tunasubiria aje mttoto wa waziri fulani aanzishe kisha tuseme anatubia hela zetu kwa kuanzisha kampuni,wakati hata mtu wa kawaida tu unaweza kuanzisha.

Na kwa uchunguzi wa haraka,ni kwamba Wanawake wengi ndio wanaongoza kumiliki Bodaboda.Licha ya kwamba mwanzo walianza wanaume wakakimbia changamoto na hatimae kinamama kupambana na kuweza kukomaaa.
Mkuu naitaji mawasiliano nawe
 
Nataka kufanya hii biashara ya bodaboda ila sijui nianzie wapi.. Asante kwa dondoo mbili tatu mlizozitoa ila naomba mnisaodie process ya kumiliki chombo, kuanzia manunuzi, usajir, kuweka GPS, mpaka bima ili kuepuka usumbufu
Asante mkuu nitakupa maelezo kwa ninavyoelewa,ila wengine watajazia,maana mie binaadam na sio mkamilifu wa kujua kila kitu,nitakapokosea watu watarekebisha.

Kwanza lazima uwe unaipenda hii biashara,sio kuona kwamba fulani anaifanya,au wengine hupenda kuitwa maboss.
Maana siku hizi ukiwa na bodabodam moja tu,basi kama Driver wako anapaki kituo fulani basi yeye anakuita boss,sasa na wenzie woote ukipita pale unasikia boss wake fulani yuleee,sasa kuna wengine wagonjwa kweli kuitwa boss wanaona rahaaa,hovyo kabisa
Sasa lazima iwe kwenye dam,na ukubali changamoto zake,ni biashara ngum sana ila nyepesi kama unajitambua.
Maduka mengi unapoenda kununua wanakusajilia pale pale kila kitu kama ukienda Mapema.Mie huwa naenda pale makao makuu ya Boxer duka lao kubwa.Na ukifika mapema wanakusajilia kila kitu an pia wanaku advise bima.So unatoka pale umekamilika,kinachofuata ni siku ya pili mwenyewe kwenda TRA ambapo ni procces fupi saana.
Unaweza haya yote ukayamaliza ndani ya siku mbili tu ukaanza kazi.
GPS system hii inategema na system ipi unatakiwa uwekewe ina specifications nyingi mno.Na kila moja ina gharama zake.zipo hadi zinaangalia mafuta yamo lita ngapi,zipo ambazo unazowez kuzima mwenyewe hata kama upo ulaya
Sasa kwa bodaboda,unaweka ila ya kawaida tu ya kuwezesha kujua chombo kipo wapi,na access ya Start and off.Halafu unapewa short training pale na consultation ya kuweza kutambua kama chombo chako kimeibiwa kutokana na speed na pia muelekeo wa chombo chako.Maana unaweza kuona kitu kinaeleke dodoma,hapo lazima utastuka,so unaweza kuwasiliana na kituo cha polisi na wakaikamata na unaweza pia kuizima ukiwa popote pale.
Ila wengi wakiibiwa na kama mwizi hajui,basi mtu huizimi,ila unawasiliana na kampuni iliyokufungia,then wao wana link a poloce wa kwenye doria kisha wanaikamata hata kama ipo Kyela huko.

KWa ufupi hakuna usumbufu wowote,unaponunua bodaboda ndio unasajiliwa kila kitu,inabakia wewe tu kwenda TRA kupata kadi maalum kama chombo cha biashara.GPS kuna mtu naweza kukupa number yake ila siku hizi kampuni nyingi saana wanafunga hizi stystem so unaweza ku google na ukazipata
 
Angalizo pia kwa wamiliki,hili nimekuwa nikilisema sana pia:-
Pindi unapoomba dua au maombi wakati unaenda kazini au unapoamka,basi ombea pia drivers wako au waajiriwa wako ili mungu awalinde na awape wepesi kwenye biashara yao,ikiwemo kupata wateja wengi na wenye kheir na huduma hizo.Maana Driver akipata na wewe ndio umepata.

Na kwa sie Waislam ni kwamba Mtu ukimuombea dua njema mwenzio basi mungu anakuongezea wewe zaidi,na pia hutenga malaika wa kukuombea na wewe zaidi.Ila wengi wetu kidogo hili ni tatizo.Maana hata hawa Drivers tunaowaajiri na wao pia hutuombea sie mabosi wao ila tunakuwa hatujui,maana anaomba kwamba usifilisike,na ufanikiwe zaidi,ili leo na kesho na yeye umkumbuke pindi neema zinapozidi.

Mie Drivers wangu karibia wote ni wakristo,ila katika kila sikukuu zao kwa wale nilionza nao muda wa mwaka,basi huwa natoa pesa ya sikukuu zoote kwa imani yake.Na hesabu ya siku moja au mbili za sikukuu naiacha ili na yeye aweze kuhudhuria ibada kanisani,na pia apate muda wa ku enjoy na watoto nyumbani na kuwapeleka sehem za michezo ya watoto nk.
Unapokuwa na furaha nyumbani wewe na watoto basi jua na mwenzio umkumbuke kwa imani yake.

Ila wengi wetu aisee,akiisha nunua huwa hana lugha njema,yaani ni ku force kwenda mbele,kuna jamaa mmoja yeye ni mtu wa Ulabu,basi anaweza kumstukiza Driver hata kati ya wiki ampelekee pesa bar.Asipopeleka kazi kweli.
Sasa hata hawa Drivers wanachangamoto zao nyingi sana kutoka kwa Matajiri,na ndio maana Drivers wengi hupenda kudeal na chombo anachomiliki Mwanamke.
Watu wakiwa na mtazamo kama wako,,Hakika maendeleo MAKUBWA yatapatikana
 
Asante mkuu nitakupa maelezo kwa ninavyoelewa,ila wengine watajazia,maana mie binaadam na sio mkamilifu wa kujua kila kitu,nitakapokosea watu watarekebisha.

Kwanza lazima uwe unaipenda hii biashara,sio kuona kwamba fulani anaifanya,au wengine hupenda kuitwa maboss.
Maana siku hizi ukiwa na bodabodam moja tu,basi kama Driver wako anapaki kituo fulani basi yeye anakuita boss,sasa na wenzie woote ukipita pale unasikia boss wake fulani yuleee,sasa kuna wengine wagonjwa kweli kuitwa boss wanaona rahaaa,hovyo kabisa
Sasa lazima iwe kwenye dam,na ukubali changamoto zake,ni biashara ngum sana ila nyepesi kama unajitambua.
Maduka mengi unapoenda kununua wanakusajilia pale pale kila kitu kama ukienda Mapema.Mie huwa naenda pale makao makuu ya Boxer duka lao kubwa.Na ukifika mapema wanakusajilia kila kitu an pia wanaku advise bima.So unatoka pale umekamilika,kinachofuata ni siku ya pili mwenyewe kwenda TRA ambapo ni procces fupi saana.
Unaweza haya yote ukayamaliza ndani ya siku mbili tu ukaanza kazi.
GPS system hii inategema na system ipi unatakiwa uwekewe ina specifications nyingi mno.Na kila moja ina gharama zake.zipo hadi zinaangalia mafuta yamo lita ngapi,zipo ambazo unazowez kuzima mwenyewe hata kama upo ulaya
Sasa kwa bodaboda,unaweka ila ya kawaida tu ya kuwezesha kujua chombo kipo wapi,na access ya Start and off.Halafu unapewa short training pale na consultation ya kuweza kutambua kama chombo chako kimeibiwa kutokana na speed na pia muelekeo wa chombo chako.Maana unaweza kuona kitu kinaeleke dodoma,hapo lazima utastuka,so unaweza kuwasiliana na kituo cha polisi na wakaikamata na unaweza pia kuizima ukiwa popote pale.
Ila wengi wakiibiwa na kama mwizi hajui,basi mtu huizimi,ila unawasiliana na kampuni iliyokufungia,then wao wana link a poloce wa kwenye doria kisha wanaikamata hata kama ipo Kyela huko.

KWa ufupi hakuna usumbufu wowote,unaponunua bodaboda ndio unasajiliwa kila kitu,inabakia wewe tu kwenda TRA kupata kadi maalum kama chombo cha biashara.GPS kuna mtu naweza kukupa number yake ila siku hizi kampuni nyingi saana wanafunga hizi stystem so unaweza ku google na ukazipata
Asante mkuu umenipa mwangaza, naomba nikutumie namba yangu pm ili nianze mchakato
 
Back
Top Bottom