Wametusaidia fedha, sera, utaalamu: Tumeshindwa sasa wanatekeleza wenyewe!

Gurudumu

JF-Expert Member
Feb 5, 2008
2,349
261
Uchafu, yaani namaanisha UCHAFU kweli kweli

Yaani binadamu kufurahia maisha, kula na kulala katikati ya takataka, uozo, harufu mbaya, maji yenye kinyesi na mikojo na wadudu kama inzi bila wasiwasi!

Tumeshindwa, tena tumeshindwa halafu tukashindwa kusema kwamba tumeshindwa. Tumeshindwa kufikiri, tukashindwa kupanga na kutekeleza. Yaani tumeshindwa kabisa, anayebisha anyooshe mkono.

Kwanza wahisani wanatupatia pesa kupitia mfuko mkuu wa bajeti ya serikali na miradi mbali mbali. Tunazitafuna kama mchwa!

Kisha wanatusaidia ushauri wa kisera na hata utaalamu wa hapa na pale. Hata kama ushauri wao ni mbovu basi mipango yetu wenyewe mizuri yenye tija ni ipi?

Yote yakashindikana bado hata mazingira tunamoishi ni hatari kutokana na uchafu unaotishia afya zetu na kuongeza gharama ya huduma za afya. Uchafu ambao pia unatishia maisha ya wahisani wanaoishi humu.

wakaamua basi bora wasafishe wenyewe, kama ilivyo kwenye hii picha hapa chini, na wataendelea kufanya hivyo



AIBU, tena namaanisha aibu kubwa sana mzungu kutoka ulaya kuja kusafisha mazingira yetu eti ili tusipate maradhi. Lakini bora wasafishe wenyewe kwa sababu wakitoa pesa ili tusafishe sisi tutakula pesa na hadithi ndeeefu - katikati ya uchafu wenyewe!
 

Attachments

  • Community Dvpment Picture.jpg
    Community Dvpment Picture.jpg
    461.9 KB · Views: 144


Kwa sababu viongozi wetu hawana aibu watalichukulia tukio hili kama la kawaida na maisha yataendelea kama kawa, lakini kusema ukweli hii ni aibu tosha kwa meya wa Dsm na watu wake... wangekuwa wanafanya kazi kwa vitendo namna hii tusingeweza kufedheheshwa namna hii!
 
Asante mkuu Mtemi Kazwile kunisaidia kuongeza ukubwa wa picha
 
Kinachokera zaidi ni pale viongozi wetu wanapokwenda kuwashukuru kwa kusafisha mitaa wakiwa na suti za dubai na wanatumia VX V8

Kinyaa kabisa wallahi.....

Waweza kuta waziri anakwenda kufungua kisima cha milioni saba akiwa na magari saba yenye thaman ya mamia ya mamilioni na allowances tu za timu hiyo kuzidi milioni sitini

tena kinyaa zaidi ni pale ambapo wanatuandikia sera, wanatekeleza, wanatathmini na kisha wanaturipotia, sie tuko bize na makongamano
 
Kinachokera zaidi ni pale viongozi wetu wanapokwenda kuwashukuru kwa kusafisha mitaa wakiwa na suti za dubai na wanatumia VX V8

Kinyaa kabisa wallahi.....

Waweza kuta waziri anakwenda kufungua kisima cha milioni saba akiwa na magari saba yenye thaman ya mamia ya mamilioni na allowances tu za timu hiyo kuzidi milioni sitini

tena kinyaa zaidi ni pale ambapo wanatuandikia sera, wanatekeleza, wanatathmini na kisha wanaturipotia, sie tuko bize na makongamano

Mkuu kwenye tv nilimuona mkurugenzi wa manispaa ya kinondoni akiwashukuru wahisani hawa kwa kuwasaidia kusafisha maeneo! Pia akatupiwa swali ni kwa nini Manispaa imeshindwa kusimamia usafi akajiumauma tu habari ikaisha na waandishia hapo
 
Mkuu kwenye tv nilimuona mkurugenzi wa manispaa ya kinondoni akiwashukuru wahisani hawa kwa kuwasaidia kusafisha maeneo! Pia akatupiwa swali ni kwa nini Manispaa imeshindwa kusimamia usafi akajiumauma tu habari ikaisha na waandishia hapo
ndio bongo hiyo.... yeye anashukuru badala ya kufanya nao kazi na kuwaambia next month tutafanya wenyewe hata kwa bakora
 
Hao mabalozi wamekosea, wangeenda kuanza kazi ya usafishaji pale magogoni. Mkuu wa nchi mwenyewe anaishi kwenye uchafu titiri
 
dah hii ni aibu sasa!! thanx media kwa hili..!!labda inaweza ondoa tongotongo

Mkuu ukifuatilia nyuuzi zote kuhusu hii inshu, media haikuripoti kama aibu bali kama sifa kwamba maagizo ya Makamu wa rais kufanya usafi jumamosi ya kwanza ya mwezi yametekelezwa, hata wahisani nao wamejitokeza. Ndiyo maana leo nikaona nililete hapa janvini
 
Samahani tuliowapa dhamana wanafanya kazi kwa mazoea ndo maana kazi na shughuli za maendeleo hazifanyiki,mathalani tumuulize afisa afya wa manispaa anafanya kazi gani au amekaa tu ofisini na kwenda kukamata akina mama lishe apate hapo fedha za kujikimi au
hawa viongozi yaani tuliowachagua na watendaji wa kuajiriwa wameshinda kufikiria kuhusu kesho wao wajikita tuu katika kudai posho za vikao na makongamano ambayo hayaishi ili tu wajichumie kodi zetu. Ivi zile harufu pale magogoni zitaisha lini au wenzetu wa usafi na mazingira hawazioni au wenzetu wa afya walioko takribani hatua 300 hawazisikii
ushauri wangu WENYE DHAMANA WAache semina na makongamano yanayomaliza fedha na fedha zielekezwe kwenye vitu vitakavyoleta tija kwa taifa letu, WApunguze kujifungia kwenye viyoyozi bali twende mitaani WAkafanye kazi zenye tija kwa jamii
asante
 
Hawa viongozi wetu sijui kama wako sawa,mtu uliye sawa huwezi kufurahia ujinga wa hali hii
 
CHADEMA wasusiwa uchafu Sinza B



na Efracia Massawe




BAADA ya Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda, kuwataka wakazi wa Manispaa hiyo kutunza mazingira, jitihada hizo zimepingwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Sinza (B) kwa kile kinachodaiwa sababu za kisiasa.

Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti wakazi hao walisema Aprili 9 mwaka huu walihimizana kufanya usafi wakiongozwa na viongozi wa mtaa huo kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiunga mkono jitihda za serikali kutunza mazingira.

Kwa mujibu wa wakazi hao, taratibu zote za kuufahamisha uongozi wa serikali ya mtaa huo juu ya azma yao zilifanyika lakini uongozi huo wa mtaa uliwanyima mifuko ya kuhifadhi taka watakazokusanya ili kuzipeleka maeneo husika kwa taratibu za kila siku.

"Tumekusanya uchafu huu unaouona hapa na maeneo mengine lakini gari lilipofika uongozi wa serikali ya mtaa ulituambia tuwaambie CHADEMA watutafutie gari la kuzolea taka hizi kwa kuwa wao ndio walioratibu suala hili la usafi… kwa kweli inatusikitisha sisi wananchi kuona mambo ya msingi yanashindwa kutekelezwa kwa sababu za kisiasa," walisema wakazi hao.

Katika maelezo yao walisema fedha za kuchangia kwa ajili ya usafirishaji wa taka hizo zilikataliwa na uongozi wa mtaa na kuwaacha katika hali ya kutofahamu siku uchafu huo utakapoondolewa.

Aidha Tanzania Daima ilimtafuta kwa njia ya simu mwenyekiti wa mtaa huo Dk. Kessy ambaye alikataaa kulizungumzia suala hilo kwa madai kuwa suala hilo ni la watu binafsi lakini taka zitaondolewa wakati wowote.

Naye Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mwenda alikiri kufahamu juu ya kadhia ya uchafu na kusema endapo suala hilo linafanywa kisiasa wahusika hawawatendei haki wananchi.
 
Kinachokera zaidi ni pale viongozi wetu wanapokwenda kuwashukuru kwa kusafisha mitaa wakiwa na suti za dubai na wanatumia VX V8

Ndio hao hao ila sisi tumo tunahimiza kupenda biadhaa zetu za nyumbani a lakini hakuna anayediriki kushonesha japo nguo ya kulalia kwa fundi wa mtaani au kwa desinger wa tazania. Hakuna aliyetari kuchongesha japo pair pair moja ya kiatu kutoka kwa fundi wa mtaani. teh teh teh

Waulize wabunge kama suti wanazovaa japo zimechangia ajira maimboni mwaoooo.......... Kwa hili wapinzani na wana CCM wote sawa tu.

 
uchizi mtupu, HATA KUFAGIA NA KUZIBUA MITARO TUNASUBIRI MABALAOZI? Kweli hawa watu wanahaki ya kutuona cc na WEHU, I WISH WAFUNGUE KLINIC MAALUM YA KUPIMA AKILI ZA VIONGOZI WETU
 
uchizi mtupu, HATA KUFAGIA NA KUZIBUA MITARO TUNASUBIRI MABALAOZI? Kweli hawa watu wanahaki ya kutuona cc na WEHU, I WISH WAFUNGUE KLINIC MAALUM YA KUPIMA AKILI ZA VIONGOZI WETU

Mkuu umetoa wazo zuri sana. Wasimamishe misaada ya bajeti serikali watusaidie kutibu akili za viongozi wetu kwanza. Wakipona ndo waendelee kuwapa misaada
 
Mkuu ukifuatilia nyuuzi zote kuhusu hii inshu, media haikuripoti kama aibu bali kama sifa kwamba maagizo ya Makamu wa rais kufanya usafi jumamosi ya kwanza ya mwezi yametekelezwa, hata wahisani nao wamejitokeza. Ndiyo maana leo nikaona nililete hapa janvini

kUMBE WENYEWE-SIRIKALI ILIONA HII KITU KAMA SIFA ....OMG!!IMPLICATION NA IMPACT YAKE NI KUBWA KULIKO WANAVYOFIKIRIA..!!
 
kUMBE WENYEWE-SIRIKALI ILIONA HII KITU KAMA SIFA ....OMG!!IMPLICATION NA IMPACT YAKE NI KUBWA KULIKO WANAVYOFIKIRIA..!!

Eti balozi anatuma picha na ripoti kwa rais wake kuonesha anazibua mifereji ya maji machafu tz. Mawaziri wetu wako nchini kwake wanakula bata. Kwa nini kikwete hana mshipa wa aibu?
 
CHADEMA wasusiwa uchafu Sinza B



na Efracia Massawe




BAADA ya Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda, kuwataka wakazi wa Manispaa hiyo kutunza mazingira, jitihada hizo zimepingwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Sinza (B) kwa kile kinachodaiwa sababu za kisiasa.

Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti wakazi hao walisema Aprili 9 mwaka huu walihimizana kufanya usafi wakiongozwa na viongozi wa mtaa huo kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiunga mkono jitihda za serikali kutunza mazingira.

Kwa mujibu wa wakazi hao, taratibu zote za kuufahamisha uongozi wa serikali ya mtaa huo juu ya azma yao zilifanyika lakini uongozi huo wa mtaa uliwanyima mifuko ya kuhifadhi taka watakazokusanya ili kuzipeleka maeneo husika kwa taratibu za kila siku.

“Tumekusanya uchafu huu unaouona hapa na maeneo mengine lakini gari lilipofika uongozi wa serikali ya mtaa ulituambia tuwaambie CHADEMA watutafutie gari la kuzolea taka hizi kwa kuwa wao ndio walioratibu suala hili la usafi… kwa kweli inatusikitisha sisi wananchi kuona mambo ya msingi yanashindwa kutekelezwa kwa sababu za kisiasa,” walisema wakazi hao.

Katika maelezo yao walisema fedha za kuchangia kwa ajili ya usafirishaji wa taka hizo zilikataliwa na uongozi wa mtaa na kuwaacha katika hali ya kutofahamu siku uchafu huo utakapoondolewa.

Aidha Tanzania Daima ilimtafuta kwa njia ya simu mwenyekiti wa mtaa huo Dk. Kessy ambaye alikataaa kulizungumzia suala hilo kwa madai kuwa suala hilo ni la watu binafsi lakini taka zitaondolewa wakati wowote.

Naye Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mwenda alikiri kufahamu juu ya kadhia ya uchafu na kusema endapo suala hilo linafanywa kisiasa wahusika hawawatendei haki wananchi.

Mbona hii rahisi sana, Wapeleke Nyumbani kwa viongozi wa mtaa zitakazo baki wapeleke ofisi ya mtaa na zingine hivyohivyo kwa meya nyumbani na ofisini.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom