Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
naona wanatafuta penati
Nawashauri wazee hawa wazionyeshe hisia zao kwenye sandukku la kura, siafiki Chadema kumuwekea Sioi pingamizi lolote.
Leo Mgombea wa CHADEMA Joshua Nasari,amewasilisha pingamizi kwa Mkurugenzi wa uchaguzi,dhidi ya mgombea wa CCM.Pingamizi hilo ni kuhusu uraia wa Sioi,katika fomu zake Sioi aliandika kuwa alizaliwa Thika nchini Kenya.Kwa mujibu wa sheria za uhamiaji kuna urai wa aina tatu,1.Wa kuzaliwa,2.Kujiandikisha,na 3,ni kupata uraia kwa kurithi kwa aliezaliwa nje nchi,na wazazi wote kuwa raia wa Tanzania.Kifungua cha 6 cha sheria ya uhamiaji,kinamtaka aliezaliwa nje ya nchi kuukana nchi aliyozaliwa na kukiri uraia wa Tanzania.
Sioi hakuwahi kuukana uraia huo,kwa mujibu wa barua ya Ofisi ya uhamiaji Arusha,kwenda kwa Mkuu wa mkoa,afisa uhamiaji aliyefahamika kwa jina la Namomba anamtaarifu RC kuwa wao kama uhamiaji hawana taarifa wala rekodi yeyote ya Sioi kuukana uraia wa Kenya