Wamefanikiwa kwenye sekta Binafsi kwanini hawaitwi kuiokoa serikali?

Lakini hata sisi watumishi wa umma tuna matatizo. Wanasiasa wana matatizo lakini sisi matatizo yetu ni makubwa sana. Tukishapata kazi hatufikirii ufanisi wa vitengo vyetu so long as mshahara unatoka serikalini on monthly basis. Hao hao watumishi wa umma tukiacha kazi serikalini tukaenda let say mgodini kwa mkaburu au IPP kwa Mengi tutafanya kazi kama punda. System yoyote yenye ufanisi ni lazima ifanye assessment kati ya mshahara inaomlipa mfanyakazi wake na faida anayozalisha huyo mfanyakazi. Lakini sekta ya umma Tz mzembe analipwa sawasawa na mwenye bidii kwenye kazi hiyo hiyo, we unategemea nini?

Hizi zote ni rewards systems. Zinapaswa kujengwa na mtu anayetaka kula jasho la mfanyakazi. Hamna mtu nayefanya kazi bila msukumo. Kunabaadhi wanataka mabadiliko, lakini kunawale wanaofanya kazi kutaka kutambulika, kukumbukwa - na kunawale wanaotaka uchochezi ili fikra ifanye kazi. Sasa kama reward yangu mimi ni mshahara tu - watu wengine hawafanyi ziada ambazo unaziona nchi zingine.

Cha msingi hapa kwanza lengo ni kupandisha ubora wa huduma inayotelewa - n a uafanya hivyo kwa kuwazawadia watoa huduma - maana watu wanapofanya kazi hawasukumwi na pesa tu - ila muonekana wao katika jamii zao, ama kufurahisha nafsi zao ama kuleta mabadiliko. Sasa, dhamani ya kazi inapoishia kwenye pesa tu ni tatizo
 
Nilikuwa nimepata nafasi ya kuzungumza na jamaa zangu kadhaa ambao kwa kweli wamefanikiwa katika sekta binafsi hapo nyumbani. Wengi wa hawa jamaa walikuwa serikalini na baadaye wakaenda uraiani wakashiriki kuanzisha makampuni au mashirika na wamekuwa very successful. Namkumbuka mmoja wao ambaye alipopewa kampuni kuiendesha wafanyakazi walianza kulalamika ati "amepewa Mswahili, kampuni itakufa". Miaka kama kumi baadaye ni mojawapo ya mashirika yanayofanya vizuri zaidi Tanzania na yakiwa yamefikia viwango vya kimataifa.
Sasa katika kufuatilia fuatilia nikagundua ni kweli wapo Watanzania wengi tu ambao wameweza kujionesha wanaweza kuwa viongozi, na wasimamizi vizuri na wana principles za utawala nzuri na wamefanikiwa. Yaani, unaweza kabisa kuona kazi zao kiasi kwamba wakati mwingine mtu akiambiwa anayefanya hivi ni "Mtanzania" watu wanaonekana kushangaa kana kwamba Mtanzania hawezikuwa meneja au mtawala mzuri.
Sasa, ni hapo ndio nimejikuta najiuliza hasa tukiangalia mashirika kama Reli, ATC n.k na hata taasisi nyingine ambazo zinaonekana kuwa na matatizo ya kiutawala (kama hospitali zetu). Sasa najiuliza kwanini watu hawa wenzetu waliofanikiwa katika sekta binafsi na wana rekodi za kugeuza mashirika au makampuni na kuwa bora hawapewi nafasi au kuitwa hata kwa mkataba mnono wa kugeuza mashirika yaliyoshindwa? Hivi ni kweli kabisa tunahitaji menejimenti toka nje?
Fikiria kwa mfano Chizi wa ATCL amepewa kuligeuza hilo shirika hivi ni kwa kiasi gani amejitofautisha kuwa ni mtawala na meneja mzuri? Hivi, kumpa mtu Reli wakati hajawahi kuendesha kampuni yoyote ya maana au kuonesha kuwa anaweza kugeuza a non-profitable company into a profitable one inaingia akilini kweli?
Au ni kweli hawa Watanzania waliofanikiwa kwenye sekta binafsi ni tishio kwa wanasiasa hasa kama wataletwa kuendesha mashirika ya umma? Na kama wapo ni kama watu gani ambao unafikiria wanaweza wakawa wazuri sana kwenye serikali kwa sababu wana rekodi nzuri uraiani?

MM hujataka kuwa wazi sana kuhusu hao jamaa zako labda lengo ni kutaka kuchokoza zaidi mjadala lakini kwangu ningependa ungetaja na kuonyesha ni namna gani wamefanikiwa.

Kwa sasa naona kama serikali imeanza kutekeleza mawazo yako kwani NHC inaongozwa na mdau aliyekuwa private sector!

Je kiu yako ni kuona kasi hiyoo inaongezwaa??

Ni kweli kuna watanzania wengi wanafanya vizuri private sector kama vile Dr Kimei (CRDB) ambaye huyu ndo rika moja na walio wengi kwa sasa wanaongoza mashirika na taasisi za Umma.
 
hawa ndio watanzania mungu aliotupa mwe!! na FF ka like this comment! kwa nini nyerere aligombana na banda kuwa kyela ni nchi yake! bora kyela ingekuwa chini ya malawi kuliko tanzania. ee mungu tuludishe kwetu wanyakyusa! wazungu wametugawa kwa watanzania wasio kuwa na akili bora wangetugawa kwa wamalawi

Matusi ya nini mama;na ni bora ungenitukana mimi pekee kuliko kuwatukana watanzania wote!
Halafu ni vema ujibu hoja sio kufuka tu na kumwaga upupu!
Ni kweli MMM hajaelezea mada yake vizuri,na majibu yake si kututukana watanzania kwamba hatuna akili!!!!
 
hawa ndio watanzania mungu aliotupa mwe!! na FF ka like this comment! kwa nini nyerere aligombana na banda kuwa kyela ni nchi yake! bora kyela ingekuwa chini ya malawi kuliko tanzania. ee mungu tuludishe kwetu wanyakyusa! wazungu wametugawa kwa watanzania wasio kuwa na akili bora wangetugawa kwa wamalawi

Ndipo akili yako ilipo ishia kifikiri?
 
MM hujataka kuwa wazi sana kuhusu hao jamaa zako labda lengo ni kutaka kuchokoza zaidi mjadala lakini kwangu ningependa ungetaja na kuonyesha ni namna gani wamefanikiwa.

Kwa sasa naona kama serikali imeanza kutekeleza mawazo yako kwani NHC inaongozwa na mdau aliyekuwa private sector!

Je kiu yako ni kuona kasi hiyoo inaongezwaa??

Ni kweli kuna watanzania wengi wanafanya vizuri private sector kama vile Dr Kimei (CRDB) ambaye huyu ndo rika moja na walio wengi kwa sasa wanaongoza mashirika na taasisi za Umma.

Tido Mhando is a case in point.Alifanikiwa kuigeuza TBC and guess what? Hayupo tena kwanini? Dr Kimei amefanikiwa sana na hakuna ubishi kwa hili.Kwani angepewa kuwa Gavana Benk Kuu au hata waziri wa kuteuliwa ili ashike wizara ya Fedha isingewezekana?Kuna sababu gani kuendelea ku recycle wastaafu ili waendeshe taasis za umma?Juzi tumeona teuzi kama za Tume ya Uchaguzi na Tume ya maadili zikishikiliwa na wastaafu Jaji Lubuva na Salome Kaganda.Ina maana hakuna watanzania wangeweza kushikilia nafasi hizo?
Kuna Watanzania wengi sana kwenye private Sector - makampuni ya Simu yamejaa watz wenzetu na wanafanya vizuri.Wangepewa kusimamia taasis za umma wangeweza kuiletea heshima Serikali.
 
hawa ndio watanzania mungu aliotupa mwe!! na FF ka like this comment! kwa nini nyerere aligombana na banda kuwa kyela ni nchi yake! bora kyela ingekuwa chini ya malawi kuliko tanzania. ee mungu tuludishe kwetu wanyakyusa! wazungu wametugawa kwa watanzania wasio kuwa na akili bora wangetugawa kwa wamalawi

Nani anaye bisha kwamba mwl Nyerere alikuwa na upeo mkubwa mno?
Dhambi ya ubaguzi imeanza kututafuna tayari!!!!
 
hawa ndio watanzania mungu aliotupa mwe!! na FF ka like this comment! kwa nini nyerere aligombana na banda kuwa kyela ni nchi yake! bora kyela ingekuwa chini ya malawi kuliko tanzania. ee mungu tuludishe kwetu wanyakyusa! wazungu wametugawa kwa watanzania wasio kuwa na akili bora wangetugawa kwa wamalawi


Mpumbavu,mjinga na ms**ng****** mkubwa wewe!
Nani kakwambia watanzania hatuna akili?
Kweli sisi wanyakyusa kwetu ni Malawi?
*********** WEEEEEEEEEE;Acha niishie hapa nisije kula ban;ndio kwanza nimetoka jela!!!
 
Mwanakijiji,

Hili ni tatizo kubwa sana na juzi juzi tuu nilikuwa najadiliana na MwanaJF kwenye PM. Kuna aiana tatu za wafanyakazi: regular workers, motivated workers and lazy workers. Ukilinganisha na regular workers, lazy workers wana gharama sana. Motivated workers wana-enjoy exerting effort in a public sector job lakini wanafanana kwa kiasi kikubwa na regular workers. Regular workers wao want to have the job done on time and according to the target iliyowekwa. Sort like doing a contractual job based on strictly agreed terms and conditions

Sasa katika ku-minimize costs, public sector hasa serikali ina-attract few motivated workers and many lazy workers lakini sio regular workers. Lakini kwenye private sector, kwa sababu ya market competition, ina-attract both motivated workers and regular workers, but not lazy workers. If you're lazy you cannot compete. Also, lazy workers wanapenda kufanya in public sector because the workload is relatively low and work effort is not verifiable.

Labda ni-quote mahali: "Since a contract satisfying a lazy worker's participation constraint has lower wage and lower required effort than a regular worker's contract, a lazy worker's contract is less appealing to the motivated workers. Therefore, the [public sector] can extract more motivational rents, and hence attracts motivated workers at lower cost, if it attracts lazy workers rather than regular workers."

"The [public sector] distorts both contracts in order to extract even more motivational rents. It offers lower-powered incentives to lazy workers than do private [sector]. This way, the lazy worker's contract becomes even less appealing to the motivated workers. However, to keep production at the desired level, this implies that the public [sector] has to hire additional lazy workers, which is costly.

Impact yake ni nini? Lack of motivation, job satisfaction na hata organisational commitment. Empirical studies nyingi zimekuta kuwa "civil servants have a bad reputation of being lazy" kutokana na ukosefu wa public service motivation. Kwenye public sector hakuna incentives za ku-attract the regular workers. Watu watadai posho zipo.
 
Tatizo kubwa kabisa ni usimamizi. Mawaziri, Manaibu na Makatibu wanaoteuliwa kusimamia Taasisi, Idara na mashirika ya umma yaliyo chini ya wizara zao. Viongozi hawa kwa njaa zao zisizo na kikomo wanajiingiza kwenye madili ya kifisadi na wakuu wa taasisi hizi. Taasisi hizi zinatafunwa bila huruma.
Mwingine ambaye hana msaada kwetu ni CAG. Kote huko anapita na kukagua kila mwaka. Angalia ziara ya Naibu Waziri-TAMISEMI inavyoibua mambo kwenye halmashauri zetu. Vijana wa CAG hawayaoni haya? Utashangaa Mwanri atarudi Dar basi.
Wengine wanaotuangusha ni MADIWANI na WABUNGE wetu. Wanazo kamati mbalimbali za kufuatilia mambo haya. Wanatakiwa wazisimamie serikali zote mbili, ile ya mitaa na serikali kuu kwa karibu. Hakuna kinachoendelea.
Wenzetu China wana sheria kali mno kwa wakuu wa Taasisi na vyombo vya UMMA. Tuanze na sheria kama ile. Vinginevyo hata hao wanaooneka kufaulu kwenye Private Sector wakirudi huku mambo ni yaleyale. Watanzania tumeharibika mno.
 
Binafsi bado sijaona deliverables or tangible output aliyofanya Mchechu kwa NHC, Ninachowitness toka NHC ya sasa ni matangazo mengi kwenye vyombo vya habari. Sijaona project mpya zaidi ya zilizokuwepo awali, still no new cormmercial projects, nyumba za walala hoi hakuna labda bado anatumikia waliompa madaraka na marafiki zake wapate nyumba kwanza ndio aanze kufanya kazi othersiwise bado hakuna cha kusifia kwa Mchechu. Asipoangalia naye atatoka hapo akijisifu ameweka logo mpya kama Mataka alivyofanya ATCL.

Mkuu hapo kwenye red sidhani kama unamtendea haki ndugu yetu Mchechu. nakushauri urudi kwenye website yao uone kuna project nyingi zimeisha na nyingine zinaendelea na pia kumekuwa na ukarabati maeneo mengi ya nchi. na shirika linaendelea kukarabatiwa na kukusanya fedha (kodi) kwa wingi. wanajitahidi kwa kweli
 
umenikumbusha kauli ya mwalimu nyerere alipoulizwa je nchi kwa sasa haina watu wa kua viongozi kwani wote hawafai, mwalimu aling'aka kwa hasira kabisa akisisitiza watu wako chungu mzima ktk nchi hii!
ukweli ni kwamba watu wako chungu mzima isipokua kupata ile chance kutokana na ukiritimba uliowekwa na wenye madaraka na walio na interest!
 
Shukrani mwanakijiji,
Sema kweli kampuni binafsi hasa ambazo ndani yake kuna wazungu zinafanya vizuri hata kama mwafrika ndiye kapewa rungu.
mifano ipo mingi mkuu, cheki ktk mabenki,Makampuni ya simu, Makampuni ya vileo nk.
Kuna kitu kinaitwa Accountability ktk haya makampuni maana yake ni tofauti kubwa sana Responsibility inayohubiriwa serikalini.
Kuwa Accountable ni kuwajibika na matokeo ya kitu ulichokifanya
Kuwa responsible ni kufanya majukumu-Bila kujali nini matokeo yake.

ndiyo maana serikali yetu inabaki na watu ambao hawajali lolote na bado wanakumbatiwa. Hivi mtu anaposaini au mwanasheria kutumia elimu yake kupindisha na kutengeneza mikataba ya kijinga inayoicost Tanesco na hatimae watanzania kwa ujumla ni mtu wa kuchekea? Ni sawa it was his responsibilty ingekuwa his Accountability angepay back.

Ni hayo tuu kwa uchache
 
Bahati Mbaya sana, Sera hii inatakiwa ibuniwe na kutekelezwa na wanasiasa walioko madarakani! Yaani inatakiwa madarakani wawepo watu wanaoamini kuwa kuna watanzania wanaweza (Na mara nyingi si wale wenye ma-accademic decorations, bali watu pragmatic) kwa hiyo hao wanaoweza ndo wapewe madaraka ya kuongoza Mashirika yetu; na si mashirika tu hata idara mbali mbali za serikali (like BoT, TRA, etc..).

Kwa hiyo, it boils down to those in power!! Of course wengine tunaweza kuchangia kwa kuwashauri.

Hali ilivyo ni kuwa uongozi mwingi unapatikana kupitia networking. Hata kama utaona mtu amechukuliwa kutokea kwenye private sector; ujue huyo ni mtu yuko very well connected. Kwa sababu mara nyingi key driver ya kuwapeleka watu pale walipo huwa si performance, bali kupeana ulaji.

Hali ikiwa hivyo, si ajabu ndani ya mataasisi au mashirika ya umma ukakuta wamo watu capable ila tu wamemezwa na wengi utawakuta wako frustrated tu!

Kwa hiyo core issue ni kuwa na utawala unaowajibika. Huo ndio utakaojua kuwa mambo hayaendi vizuri. Na ikiwa mambo hayaendi vizuri, inatakiwa yafanyike mabadiriko makubwa jinsi tunavyoendesha mambo yetu.

Bahati mbaya walio madarakani wengi hawaamini kuwa mambo yanaenda vibaya; wanaamini kuwa tulipo ndo tungeweza kufika hata iweje.

Kwa hiyo it boil down to those we put in power!! Basi. That is how critical our decision to put one of ours in power is!!
 
hawa ndio watanzania mungu aliotupa mwe!! na FF ka like this comment! kwa nini nyerere aligombana na banda kuwa kyela ni nchi yake! bora kyela ingekuwa chini ya malawi kuliko tanzania. ee mungu tuludishe kwetu wanyakyusa! wazungu wametugawa kwa watanzania wasio kuwa na akili bora wangetugawa kwa wamalawi

Unasikitisha sana!! no research...no data...no right to speak!!!
Mwaikambo aliyekuwa Bima (N.I.C) ni kabila gani?? inajulikana alipoifikisha bima yetu...
Serikalini walikuwepo na bado wapo wengi kutoka Kyela mbona watu bado wanalalamika??
Acha ukabila...Lawama siyo ya mtu mmoja wala kabila au dini bali ni ya mfumo...ambao tulirithi
toka kwa wakoloni na tukashindwa kuukarabati ili utunufaishe. Mfano ni tafsiri ya maneno "MALI YA UMMA"
haikuwekwa katika hali ya kila mtu ahisi kuwa ni yake na anawajibika kuilinda. Utaona watu wanasifiwa mitaani
kutokana na utajiri walioupata kutokana na wizi wa mali ya umma. Wengine wamefanikiwa kuwa watunga sheria
kupitia chama tawala na hata upinzani. wezi na waharibifu wa miundombinu mfano nyaya za umeme na simu, vyuma vya
madaraja, mabomba, alama za barabarani na nyara za serikali tunawajua, tunaishi nao mitaani, ni rafiki zetu, dada zetu, kaka
zetu na wazazi wetu, hatujajitolea kwa dhati kuilinda mali yetu. Badala yake kila jambo tumeligeuza kuwa siasa. Hakuna ukombozi wa maana tutakaoupata hata tukibadili majina ya vyama vitakavyounda serikali endapo FIKRA zetu hazitabadilika.
 
Just a simple logic mkuu,

Hakuna mtu yeyote mwenye personal integrity na ambaye ana clear dreams na anatamani kuacha legacy inaoyoeleweka atakuwa tayari kufanya kazi na vichaa au mbumbumbu tena wakiwa ndio waajiri wake!!

Hivi unawezaje kufanya kazi na daktari ambaye yeye pia ni mgonjwa wa ungonjwa fulani na wakati huo hata hajui chanzo cha ugonjwa wake??
 
Mwanakijiji umegusa kiini cha matatizo yote ya Sekta ya Umma hapa Tanzania.

Kama tungekuwa na wataalam na watendaji imara na waliokomaa, wasio sehemu ya wanasiasa wetu hakika hii nchni inge kuwa mbali sana. Hao unaowaona wamefanikiwa katika sekta Binafsi wapo wa aina mbili: -
  1. Walikuwa waadilifu na wenyewe uwezo lakini wakashindwa kuibadilisha system chafu na mbovu ambayo ndio uti wa mgongo wa wanasiasa wetu, watu hawa uitwa wanaa Serikali na ujengewa zengwe na hata kutafutiwa kila aina ya sababu ili waondoke, Hata Mrema wa TANROADS ana angukia katika group hili wengi hawajui ukweli juu yake ila walifanikiwa kumuondoa ili mambo yasonge mbele kama kawaida, wengine ni kama aliyekuwa CEO wa TBC - Mhando hakupewa nafasi, na wengineo.
  2. Aina ya pili ni wale waliofanikiwa katika Sekta Binafsi kama wafanyabiashara baada ya kuiba kutoka katika sekta ya Umma, hawa ni watu wachafu na wabovu na hata hayo tunayoona kama mafanikio yao katika Sekta Binafsi ni hujuma wanayoendelea kuifanyika Sekta ya Umma, hawa ndio wafanyabiasha wetu. Biashara za kuhujumu kodi, hujuma katika manunuzi ya Umma, n.k
Mwanakijiji watu wasafi, wenye weledi na waadilifu hawawezi kukaa ndani ya Sekta ya Umma hapa Tanzania mpaka tubadili mfumo wa Utawala hasa watoa maamuzi wetu au mfumo mzima wa siasa zetu maana wao ndio wanaoiharibu hii sekta kwa kuweka watu wao ambao wanaweza kufanya nao fraud ndani ya Serikali na sekta kwa Ujumla, wanaweka vibaraka wao na pengine hata ndugu zao wenye elimu za udanganyifu, kama wao pia walivyo na elimu za udanganyifu. Ndio maana siku zote ajira ndani ya Serikali imejaa mawingu ya giza na hakuna uwazi.

Wabia wetu katika mandeleo (Watoa misaada wetu kutoka ngambo) walikwisha kuliona hili na ndio maana walitushauri kuanzisha kitu kinachoitwa Agencies, hii ilikuwa na maana ya kupata wakala ambao watafanya kazi kwaniaba ya serikali ikijitegemea na ambazo haziingiliwi na wanasiasa hata kidogo, ambazo zingekuwa zina ajiri wataalam kwa vigezo na viwango, Agencies zote tulizo anzisha chini ya usimamizi wa Wabia wetu katika maendeleo sasa tayari zimerudi kuwa sehemu ya serikali moja kwa moja na zingine zinaingiliwa na wanasiasa hadi chumbani, Mfano TRA na wizara ya fedha, TANROADS na Wizara ya Ujenzi, EWURA na Wizara ya Nishati na Madini, n.k.

Mbaya zaidi wakati wa kuanzisha hizo Taasisi zetu Serikali ilishauriwa kuacha kuingilia ajira za Agencies ili hatua zote zifanywe wazi na kwatumia makampuni yenye utaalam kuhakikisha hizo Agencies zinapata wafanyakazi wenyewe weledi unaostahili lakini hilo pia halikwenda kama ilivyotarajiwa, ndio maana utaona Mara ghafla waziri fulani kamteuwa CEO wa Shirika fulani bila hata kutangaza nafasi na hata kueleza Umma huyo anayepewa hiyo nafasi ana nini kichwani kuliko wengine. Angalia jinsi Senate ya Amerika inavyo jadili CV na wasifu hadi wa Mahakimu wa ngazi kama za Wilaya tu huku kwetu kabla ya uteuzi wao na jinsi Umma unavyojulishwa juu ya Wasifu, Elimu na uwezo binafsi wa watu wanaoteuliwa kushikilia mamlaka katika nafasi za UMMA katika nchni ya Amerika na Uingereza! Sisi ni lini hata tumewai kuambia kwanini Mtu fulani anapewa Ujaji sembuse Ujaji Mkuu, au Mkuu wa Polisi, au Mkugenzi wa TRA, au hata Makatibu wa wakuu, kama tungelikuwa tunaangalia uwezo, weledi na uadilifu tusingepata wakina Jairo katika vyeo kama Katibu Mkuu wa Wizara!

Kwa leo nadhani hili pia linapaswa kuwa katika katiba, jinsi na namna ya kumpata Mtumishi wa Umma na kiongozi katika Sekta ya Umma. Azimio la Arusha liliainisha hili lakini sasa halipo sasa labda tuliweke katika katiba.

Asante Mkuu wangu Mwanakijiji, Alamsiki!
 
Mkuu,thread hii haifanani na upeo wako...imekaa kiudaku udaku hivi!
Hujaweka bayana hayo makampuni waliyo shiriki kuyaanzisha;mfano wa hao jamaa zako nk!
Kiufupi thread hii imesimama hapa sababu tu ni MMM aliye ianzisha;la sivyo ingekuwa moved kwenye jukwaa la UDAKU!

Mkuu Eliahkamwela, sijakuelewa hata kidogo, nadhani MM Mwanakiji ametumia hekima zaidi kutokujibu. He is right.
Back to the point.
Kwa maoni yangu tatizo la Tanzania ni katiba mbovu. Huko Serikalini mtu ye yote akianza kuchapa kazi anakatishwa tamaa na bosi wake, ambaye naye ameshakata tamaa siku nyingi kutokana na yeye pia kukatishwa tamaa. kukatishana tamaa huko kunaanzia ngazi ya kitongoji kwenda juu hadi kwa mawaziri na bosi wao Rais. Ndo maana hali mbaya ktk sekta ya umma imeanzia kipindi cha Mwinyi hadi leo. Ifahamike kuwa serikalini hakuna check and balance and there is no accountability ambayo ilipaswa kuwepo kama tungekuwa na Bunge imara na mahakama imara. Kwa hiyo, waziri anafanya atakavyo as long as Rais hajui kumfuatilia au hawezi, at the same time anajua wabunge hawawezi kumfanya kitu cho chote. Na Waziri akiwa mchapa kazi anawafanya waliochini yake wizarani hadi ngazi ya chini yake wawe kama yeye, na akiwa vise versa (mla rushwa) the opposite is true (Bahati mbaya sekta ya umma haina watu wa jinsi hiyo).
Kwa upande Sekta binafsi top management ikiwa safi ina maanisha kuwa kila mtu lazima achape kazi na taasisi hiyo itasonga mbele daima.
 
Nilikuwa nimepata nafasi ya kuzungumza na jamaa zangu kadhaa ambao kwa kweli wamefanikiwa katika sekta binafsi hapo nyumbani. Wengi wa hawa jamaa walikuwa serikalini na baadaye wakaenda uraiani wakashiriki kuanzisha makampuni au mashirika na wamekuwa very successful. Namkumbuka mmoja wao ambaye alipopewa kampuni kuiendesha wafanyakazi walianza kulalamika ati "amepewa Mswahili, kampuni itakufa". Miaka kama kumi baadaye ni mojawapo ya mashirika yanayofanya vizuri zaidi Tanzania na yakiwa yamefikia viwango vya kimataifa.
Sasa katika kufuatilia fuatilia nikagundua ni kweli wapo Watanzania wengi tu ambao wameweza kujionesha wanaweza kuwa viongozi, na wasimamizi vizuri na wana principles za utawala nzuri na wamefanikiwa. Yaani, unaweza kabisa kuona kazi zao kiasi kwamba wakati mwingine mtu akiambiwa anayefanya hivi ni "Mtanzania" watu wanaonekana kushangaa kana kwamba Mtanzania hawezikuwa meneja au mtawala mzuri.
Sasa, ni hapo ndio nimejikuta najiuliza hasa tukiangalia mashirika kama Reli, ATC n.k na hata taasisi nyingine ambazo zinaonekana kuwa na matatizo ya kiutawala (kama hospitali zetu). Sasa najiuliza kwanini watu hawa wenzetu waliofanikiwa katika sekta binafsi na wana rekodi za kugeuza mashirika au makampuni na kuwa bora hawapewi nafasi au kuitwa hata kwa mkataba mnono wa kugeuza mashirika yaliyoshindwa? Hivi ni kweli kabisa tunahitaji menejimenti toka nje?
Fikiria kwa mfano Chizi wa ATCL amepewa kuligeuza hilo shirika hivi ni kwa kiasi gani amejitofautisha kuwa ni mtawala na meneja mzuri? Hivi, kumpa mtu Reli wakati hajawahi kuendesha kampuni yoyote ya maana au kuonesha kuwa anaweza kugeuza a non-profitable company into a profitable one inaingia akilini kweli?
Au ni kweli hawa Watanzania waliofanikiwa kwenye sekta binafsi ni tishio kwa wanasiasa hasa kama wataletwa kuendesha mashirika ya umma? Na kama wapo ni kama watu gani ambao unafikiria wanaweza wakawa wazuri sana kwenye serikali kwa sababu wana rekodi nzuri uraiani?

MKJJ,
Topic nzuri lakini umeshindwa kutaja watu au kampuni zenyewe (anyway maybe privacy); je what about size of the companies, capitals/income; sector gani; wanalipa kodi kiasi gani; unajua kama mmoja alvojieleza hapo, Vx and wazee hawa-kugawiwa etc; these really are not the companies which you're trying to tell us.

Au ulitaka kutwambia watu kama Kimei, Mengi, Bakhresa, METL etc We may have hidden Steve Jobs's; what kind of innvovation hawa watu wamefanya kwenye hizo products or services, hao niliowataja hapo juu walikuwa mostly self motivated also backing. Huoni kuwa problem yetu ni kuwa usingizini?
 
Mkuu Eliahkamwela, sijakuelewa hata kidogo, nadhani MM Mwanakiji ametumia hekima zaidi kutokujibu. He is right.
Back to the point.
Kwa maoni yangu tatizo la Tanzania ni katiba mbovu. Huko Serikalini mtu ye yote akianza kuchapa kazi anakatishwa tamaa na bosi wake, ambaye naye ameshakata tamaa siku nyingi kutokana na yeye pia kukatishwa tamaa. kukatishana tamaa huko kunaanzia ngazi ya kitongoji kwenda juu hadi kwa mawaziri na bosi wao Rais. Ndo maana hali mbaya ktk sekta ya umma imeanzia kipindi cha Mwinyi hadi leo. Ifahamike kuwa serikalini hakuna check and balance and there is no accountability ambayo ilipaswa kuwepo kama tungekuwa na Bunge imara na mahakama imara. Kwa hiyo, waziri anafanya atakavyo as long as Rais hajui kumfuatilia au hawezi, at the same time anajua wabunge hawawezi kumfanya kitu cho chote. Na Waziri akiwa mchapa kazi anawafanya waliochini yake wizarani hadi ngazi ya chini yake wawe kama yeye, na akiwa vise versa (mla rushwa) the opposite is true (Bahati mbaya sekta ya umma haina watu wa jinsi hiyo).
Kwa upande Sekta binafsi top management ikiwa safi ina maanisha kuwa kila mtu lazima achape kazi na taasisi hiyo itasonga mbele daima.

The answer is CAPITALISM, government lazima itilie mkazo kwenye private sector; because these people will own their own companies they will be more responsible. Company za uma zingikwenda public, directors hawangefanya utani as long as laws are there.
 
Back
Top Bottom