Wamasai waamua kujikita katika kilimo cha pareto.

Monasha

JF-Expert Member
Apr 2, 2011
561
422
asaipareto.jpg
KWA kawaida jamii ya wamasai ni wafugaji. Kutokana na asili yao hiyo ya ufugaji, sehemu kubwa ya maisha yao imetawaliwa na tabia ya kuhamahama toka eneo moja kwenda jingine ili kutafuta malisho kwa mifugo yao.


Kutokana na mabadiliko ya kiuchumi duniani pamoja na mabadiliko ya tabia nchi ambapo joto limeonegezeka duniani na kutokuwepo kwa mvua za kuaminika uchumi wa ng’ombe hauwezi tena kuhimili kuendesha maisha na badala yake jamii ya Wamasai imeanza kujishugulisha na kilimo ili kufidia pengo.

Wamaasai siyo tu wameingia katika kilimo pekee bali wameanza taratibu kuingia katika nyanja zote kama ilivyo kwa watanzania wengine na kuishi katika makazi ya kudumu.

Wapo ambao wamehamia mijini kufanya biashara za kazi za sanaa za mikono ikiwamo ususi wa nywele na nyingine nyingi. Hata hivyo wako ambao wamebaki kwenye maeneo yao na kuendesha kilimo cha mazao ya chakula na biashara.

“Sio kwamba tumeacha kufuga hapana, lakini pamoja na kufuga tumeamua kulima mazao ambayo tumegundua yanaweza kutusaidia kwa chakula na ziada kuuza ili kuongeza kipato mbali ya kutegemea ufugaji,” anasema Sabaya Lwelyen mkazi wa kijiji cha Engalaoni, Wilayani Arusha.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Ngorika, Mkoani Arusha, Kisoisoi Nang’enoi anasema kuwa moja ya mazao ambayo wameanza kulima siku za hivi karibuni ni pareto.

Amesewa walianza kulima pareto miaka miwili iliyopita baada ya kupata hamasa kutokana na kuwepo kwa soko la uhakika katika eneo lao ambalo pia pia linafaa sana kwa kilimo cha zao hilo la pareto.

“Walikuja kuhamasisha kilimo cha pareto, lakini mwanzo hatukukubali kiurahisi tukihofia soko lake lakini pia hatukuwa na ujuzi wa kilimo cha pareto. Hivyo tukaamua kuwaachia wenzetu wachache ambao walipojaribu kulima wamepata manufaa kutokana na kuiuza bila usumbufu,’ anasema Nang’enoi.
Anasema kufuatia mafanikio makubwa waliyopata wenzi wao kwa kulima pareto, wananchi wengi walihamasika na kukubali kutenga maeneo kwa ajili ya kuanzisha kilimo cha pareto.

Amesifu uwepo wa soko la uhakika wa pareto, ambapo mkulima analipwa mara moja na hakuna ubabaishaji kama ilivyo kwa baadhi ya wanunuzi wa mazao mengine katika eneo hilo.

“Nimetenga ekari mbili kwa ajili ya kulima Pareto. Ninachosubiri kwa sasa ni kuletewa mbegu ili nipande kwa sababu nimeona manufaa ambayo jirani yangu amekuwa akiyapata,” anasema Solomoni Loshloiza, mkazi wa Mukulate.

Hiyo ni kwa wale wamasai wanaoishi maeneo ya Arusha.
Lakini wenzao tunaoishi(jamani mwenzenu mi masai) maeneo ya Ngorongoro tunapata tabu sana hasa kwenye suala la kilimo kwani eneo hili wanadai ni la hifadhi na hivyo hakuna kilimo kinachoruhusiwa katika eneo hili.
Kweli eneo hili ni la hifadhi lakini mbona toka enzi za ukoloni wamasai hawa wa ngorongoro wamekuwa wakilima pamoja na kuishi na vivutio vyote bila ghadhabu yoyote???
Haya tumenyimwa kutumia ardhi yetu, sasa wewe unategemea tutaishije??
Wengi wetu (wamasai) wameishia mijini kutafuta kazi mbalimbali na hasa za ulinzi. Leo hii mmasai anajulikana kama "MBWA MKALI" Jamani huu ni udhalilishaji.
Na hii yote ni kutokana na serikali kushindwa kutafuta solution ya kudumu.
Kusema eneo lile hakuna kilimo kwa sababu ni HIFADHI, ni kweli lakini Hawa uliowakuta katika eneo lile utawafanyaje???

Wana JF naomba mawazo yenu
 
limeni sana tena sana, na hata kazi zingine zote fanyeni, matusi si kitu, jamii yenu ni mfano mzuri kwa afrika, mko kuanzia porini hadi mawaziri.
safi sana
 
limeni sana tena sana, na hata kazi zingine zote fanyeni, matusi si kitu, jamii yenu ni mfano mzuri kwa afrika, mko kuanzia porini hadi mawaziri.
safi sana

Lakini sasa kaka, kulima tunapenda tena sana. Tatizo ni kuwa tuna baniwa. Serikali inataka eti tuondoka katika eneo lile kuwapisha wanyama.
Lakini wanasahau kuwa toka enzi na enzi tumekuwa tukiishi na hao wanyama tena bila kuwapunguza na ndo sababu wapo mpaka leo. Chukulia tu mfano kilichotokea Loliondo, watu kuchomewa maboma na mali zao eti kwa sababu hawataki kumpisha mwekezaji (Yule mwarabu) kwenye kile walichokiita eneo tengefu.
Kwahiyo hata sasa hivi mtu akikutwa analima huku Ngorongoro moja kwa moja shamba hilo litaunguzwa au kufyekwa. Kwakweli tunakosa uhuru wa kutumia ardhi kama wengine.
 
hii pareto unavuna baada ya muda gani??

Hili zao si annual wala perenial, ila ndani ya mwaka mmoja unaanza kuvuna, mwanzoni mavuno huwa madogo, yanapanda kwa kadri mmea unavyopanuka na baadae mazao hupungua kwa kadri mmea unavyozeeka. Nakumbuka baada ya miaka mitatu hivi maua(ambayo ndio mavuno) huanza kupungua,hiyo ni ishara kuwa uanze kuandaa miche na shamba jipya.

Hili zao liliwatoa sana Wakinga miaka hiyo ya Julius,baadae vikaja viazi na siku hizi mbao, kwa mbali naona pareto inarudi. Vipi Wakinga mpo ?
 
mkuu Malila
mashukuru kwa maelezo yako mazuri ila kwa sasa soko lipo, kuna kiwanda kipo mafinga nadhani ndio soko kubwa kwa Tanzania lilipo (ingawa sijajua ukubwa wa kiwanda ukoje) na bei yake nasikia ni nzuri sana 2,000 kwa kilo moja!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom