Wamalawi washitukia Tanzania na maandalizi ya vita!!

Pamoja na kwamba ninaunga mkono njia za kidiplomasia zaidi katika kumaliza utata wa mgogoro wa mpaka kati yetu na malawi lakini pia mimi mtazamo wangu ni kuwa JWTZ kuhakikisha kwamba inalinda mipaka yetu ndani ya ziwa nyasa kama serikali inavyotambua kwamba ni katikati ya ziwa.

Sasa ikitokea mtu yeyote, chombo chochote, ama kampuni yoyote inayofanya utafiti ama shughuli yoyote iwe ya kiuchumi ama kijamii ndani ya ziwa nyasa imevuka/wamevuka mpaka na kuingia ndani ya eneo la Tanzania inabidi idhibitiwe/wadhibitiwe.

Kwa kufanya hivyo sidhani kwamba tutakuwa tumetangaza ama kuanzisha vita, hapo tutakuwa tunalinda mipaka yetu na sidhani kama kuna mtu ama jumuiya ya kimataifa itatushangaa ama kutucheka.
Mkuu,cha kwanza cha kutizama,ni kuona ni nani na nani wanasapoti mipaka ipi na kutambua vs kutoitambua, tuanzie hapo maybe...vijinchi kama vyetu kwenye dunia ya sasa,viongozi wake waki "bweka",lazima kuna "handlers" behind, so cha muhimu ni kufuatilia hayo kwanza.

Kwasababu mkuu siyo siri, gharama za vita tutakopa(exclude life costs), na tutakopa kutoka kwenye taifa linalosapoti "point of view" yetu kuhusiana na huo mpaka...Na taifa/mataifa ambayo yanaweza kutuback kwenye either UN ama mahakama za kimataifa nk.

Ndo dunia inavyoenda kwasasa...
 
Tukianzisha vita dunia nzima itatucheka. Hii issue lazima ipelekwe kisheria maana hata kama tukishinda vita sio lazima tutakuwa tumepata mpaka kama jamii ya kimataifa haitatambua hivyo.

kwani ardhi ya Tanzania ni mali ya jamii ya kimataifa?
 
Tanzania ni nchi huwezi kufananisha wala kuoanisha na mfano wako. Huwezi kukurupuka kwenda vitani kwa kuwa ndege zinafanya utafiti.

Ingekuwa wanachimba hayo mafuta walau ungekuwa na mahali pa kuanzia. Hivi mbona dhahabu inaibiwa kila kukicha na hatuendi vitani, tunatapeliwa kila leo na viongozi wetu tena mbele ya familia zetu mbona hatuendi vitani, wananchi wananyang'anywa ardhi na wawekezaji ndani ya nchi tena maeneo waliozaliwa mbele ya familia zao na mali zao kuharibiwa au wengine kuuwawa mbona hatuendi vitani.

Ujanja wa zamani huo kutisha watu kwa vita.

Mimi naona wewe ndiye unaye ongea mambo ya kitoto eti huwezi enda vitani kisa ndege inafanya utafiti. Hivi kwanini syria ilitungua ndege ya nchi nyingine ilipoingia kwenye anga lake kwanini hawakusema wasingeilipua kwakua haikutua?

Tanzania ni nchi haiwezekani nchi nyingine iwape kibari watu flani kufanya utafiti kwenye mipaka ya nchi yetu iwe angani, ardhini au kwenye maji halafu tusiseme eti aaah si wanafanya utafiti tu.

Ukitaka jua hilo mfano tanzania ingekuwa inafanya utafiti bila kibari kwenye mipaka ya uganda au kenya ungeona matokeo yake.
 
Nadhani Kama ukisoma bandiko utagundua kuna resolution Za kihistoria Za mipaka hiyo ambayo ilitambua kwamba ziwa sisi tunaloliita Nyasa Kwao ni ziwa Zambia ambalo kutokana Na mipaka 'hiyo' ambayo Mimi Na wewe hatukuwepo wala hatujui ukweli inshu wao wanajua ni Lao toka hizo enzi Na si kwamba wameshafungua Kesi wanaweza Kama sisi Tz tukiendelea kuling'ang'ania ndipo watapochukua hatua ya Kutaka mapatano Kwenye maamyzi ya kimataifa ..

Umesoma vizuri ulichoandika kabla ya kuposti ndugu? Ninachoona kwenye andiko lako ni mkanganyiko wa mambo yasiyoeleweka.

Mara unasema hatukuwepo wakati mipaka inachorwa - utadhani wamalawi wa sasa walikuwepo wakati mipaka inachorwa; mara unasema wao wanajua ni ziwa lao toka enzi hizo; mara unasema tunaling'ang'ania ziwa na tukiendelea watachukua maamuzi!! Inaonekana hata hujui hoja gani unayotaka kuijenga.

Suala la wao wanaamini nini kuhusu ziwa Nyasa - wewe umeliita ziwa Zambia - sio hoja kwani hata sisi tunajua kuwa nusu ya ziwa lipo upande wa nchi yetu.
 
Jamaa wanaonekana kuwa na busara sana kuliko viongozi wetu, wanaotaka kujichukulia sheria mkononi. Hivi Membe hajui kuwa kuna international court mpaka yeye achukulie vita kuwa ni suluhisho? anajua kuwa nchi yetu hapa tulipo imefilisika?

Sasa naanza kujua kuwa wapinzani wana akili sana kuliko watawala wetu. Statement ya Malawi inaonekana imetolewa na kongozi mwenye mtazamo mzuri, ile ya Membe na Lowassa ni ya walevi wa virabuni maana kwao kupigana huwa hata bila sababu.

Anajitambulisha kuwa yeye si dhaifu na hivyo upresident anauweza.
 
Ha ha haaa.. Aisee .. Na mie naongezea watanzania bora tufe kuliko kukosa twiga wanaoibiwa... Ha ha haaa.. Ngojea niongeze tena.. Bora tufe kuliko Kuwa wa mgao Wa umeme. Ha ha haaa!!! AKILI nyingine jamani,!!

Namie naongeza bora watanzania tufe kuliko kurudia kosa.kwani kosa halirekebishwi kwa kurudia kosa lingine.
 
Inabidi kupitia upya mikataba ya waloloni mapema, unaweza kukuta Kumbe na lake Tanganyika nalo si letu ni la Kongo!!

catoonist wa bongo nao kwa mkwara.....
 

Attachments

  • 20120809_001.jpg
    20120809_001.jpg
    616 KB · Views: 55
Teh teh teh...mi siogopi vita ila tukichukua kitu kisicho chetu lazima tuwe wababe kama Israel. Vinginevyo itakula kwetu.

Platoon moja iliyoko Ruvuma inatosha kuiangamiza Malawi yote ikabaki majivu,
so worry not kaka mkubwa
 
Umesoma vizuri ulichoandika kabla ya kuposti ndugu? Ninachoona kwenye andiko lako ni mkanganyiko wa mambo yasiyoeleweka.

Mara unasema hatukuwepo wakati mipaka inachorwa - utadhani wamalawi wa sasa walikuwepo wakati mipaka inachorwa; mara unasema wao wanajua ni ziwa lao toka enzi hizo; mara unasema tunaling'ang'ania ziwa na tukiendelea watachukua maamuzi!! Inaonekana hata hujui hoja gani unayotaka kuijenga.

Suala la wao wanaamini nini kuhusu ziwa Nyasa - wewe umeliita ziwa Zambia - sio hoja kwani hata sisi tunajua kuwa nusu ya ziwa lipo upande wa nchi yetu.

Sitaki kuamini kabisa kwamba umeshindwa hata ku-google historia ya Zambia.. Sidhani pia kwamba umeamua Kugoma kujifunza kiasi gani Cha eneo la Ziwa Tz tunamiliki.. Uvivu ni Kama ugonjwa Kwa watanzania wengi tu. hauko peke yako .. Tata kweli tata
 
hata hivyo Malawi ndio wanoonekana kuwa na ushahidi wa kutosha kuliko sisi. Kuna uwezekano wakatushinda endapo wataenda mbele ya sheria.
 
hata hivyo Malawi ndio wanoonekana kuwa na ushahidi wa kutosha kuliko sisi. Kuna uwezekano wakatushinda endapo wataenda mbele ya sheria.
Hilo wala usiwe na wasiwasi nalo, soma mgogoro wa Lake Chad.
 
mkuu,cha kwanza cha kutizama,ni kuona ni nani na nani wanasapoti mipaka ipi na kutambua vs kutoitambua,tuanzie hapo maybe...vijinchi kama vyetu kwenye dunia ya sasa,viongozi wake waki "bweka",lazima kuna "handlers" behind,so cha muhimu ni kufuatilia hayo kwanza.Kwasababu mkuu siyo siri,gharama za vita tutakopa(exclude life costs),na tutakopa kutoka kwenye taifa linalosapoti "point of view" yetu kuhusiana na huo mpaka...Na taifa/mataifa ambayo yanaweza kutuback kwenye either UN ama mahakama za kimataifa nk.Ndo dunia inavyoenda kwasasa...
Dhana potofu!!!!!
Vita ni biashara, tupe gas, gold, coal etc... sisi tutakupa vifaru (amphibious), guns,...whatever you want.
Biashara ya silaha ipo chini ya watu binafsi haijali urafiki hata siku moja.

Halafu, wewe mbona upo kinyume sana na watanzania??? Si uhamie Malawi kama unawaogopa??
Yaani mtu anakuja living room yako, anachukua remote yako na kukaa kwenye coach lako halafu unatuambia utampeleka mahakamani?
Ni$%@ you're soft like a twizzler!! ... Gangamala acha mambo ya kibishoo!!
 
Dhana potofu!!!!!
Vita ni biashara, tupe gas, gold, coal etc... sisi tutakupa vifaru (amphibious), guns,...whatever you want.
Biashara ya silaha ipo chini ya watu binafsi haijali urafiki hata siku moja.

Halafu, wewe mbona upo kinyume sana na watanzania??? Si uhamie Malawi kama unawaogopa??
Yaani mtu anakuja living room yako, anachukua remote yako na kukaa kwenye coach lako halafu unatuambia utampeleka mahakamani?
Ni$%@ you're soft like a twizzler!! ... Gangamala acha mambo ya kibishoo!!
Nadhani hukunielewa vyema hapo kwenye kuhusu nani anakupa sapoti,silaha haziuzwi ama kutolewa kwa kila mtu.Sasa kama akili yako wewe inakutuma kujustify "biashara" ya gold na rasilimali nyinginezo kwa silaha,then una matatizo na hujifunzi.Nieleze ni mazingira gani ya aina hiyo yamewasaidia wanaotoa rasilimali ili waende vitani na wakapata mafanikio?

Kuhusu mtu kuja sebuleni kwako na kuchukua remote halafu na wewe unasema unatakiwa umwue, hilo linategemea na wapi ulipo. Bongo ni kawaida sana hayo mambo,kwanza mtaani watu ni vitofa, mafuta ya taa, tairi na kiberiti.

Kwa wenzetu,mfano umevamiwa na mwizi, ukampiga risasi, lazima iwe proved kwamba kulikuwa na ulazima wa wewe kufanya hivyo, yani justification ya self defense, na mazingira ie kama kama na yeye alikuwa na silaha ama la, na silaha hiyo pia ni ya aiana gani, kwa mfano je ni kisu ama screw driver etc.

Na pia kama alikuwa anaku attack or not. Kama kaingia nyumbani kwako,halafu akaiba,na akawa anatoka nje anakimbia,ukimpiga risasi unashtakiwa kwa mauwaji.Kwa utaratibu wako wa kufikiri,I hope wewe si kiongozi.
 
Jamaa wanaonekana kuwa na busara sana kuliko viongozi wetu, wanaotaka kujichukulia sheria mkononi. Hivi Membe hajui kuwa kuna international court mpaka yeye achukulie vita kuwa ni suluhisho? anajua kuwa nchi yetu hapa tulipo imefilisika?

Sasa naanza kujua kuwa wapinzani wana akili sana kuliko watawala wetu. Statement ya Malawi inaonekana imetolewa na kongozi mwenye mtazamo mzuri, ile ya Membe na Lowassa ni ya walevi wa virabuni maana kwao kupigana huwa hata bila sababu.

Hapa umefikiri kwa kutumia masaburi. Kwani Malawi walivyoanza kurusha ndege walikuwa hawajui mahakama ya kimataifa. Hivi mtu anakuchukulia mali yako unasubiri sheria. Self defence inakubalika duniani kote. Ndo maana tuna majeshi. Kama ni hivyo tuvunje majeshi tutegemee mahakama
 
Back
Top Bottom